Rais Magufuli kuondoa sherehe za Uhuru ili fedha zikajenge hospitali Dodoma si jambo la sifa, ni kuonesha Serikali haina mipango hususan ya maendeleo

Rais Magufuli kuondoa sherehe za Uhuru ili fedha zikajenge hospitali Dodoma si jambo la sifa, ni kuonesha Serikali haina mipango hususan ya maendeleo

Kwa mtu mwenye akili za chini, atamsifia Rais Magufuli kwa kutangaza kwamba mwaka huu hatutakuwa na sherehe za uhuru ili kuokoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya Dodoma. Kwa mtu mwenye akili ya kufikiria, atajiuliza, hivi inakuwaje tunakuwa hatuna mipango hususa inayotia ndani kutengwa kwa fedha kwa ajii ya ujenzi wa miundo mbinu muhimu kama hospitali Dodoma?

Naingia sana wasiwasi, kwamba inafikia mahali mambo muhimu kwa ajili ya miundo mbinu na miradi ya nchini hayapangwi kwa kufuata uratatibu maalum, bali inakuwa ni uamuzi kutokana na hisia za Rais Magufuli. Kuamua kujenga barabara ndefu ya kiwango cha lami kwa ghafla na kumpigia simu mkurugenzi wa TANROAD, au kuamua ghafla kwamba fedha za uhuru ndio zikajenge hospitali, ni wonyesho dhahiri wa udhaifu mkubwa sana katika uongozi wa Magufuli katika kuwa na mipango hususa ya miradi ya maendeleo nchini. Magufuli asifikiri hiyo inamfanya kuwa raisi bora au mzalendo. Ni udhaifu katika uongozi.

Hautuwezi kufanikiwa kufanya mambo haya kwa kutegemea Rais Magufuli siku hiyo kawaza nini kichwani, au kasukumwa na nini kabla hajachukua simu na kutoa agizo mradi fulani mkubwa nchini utekelezwe fedha atajua kwa kuzipata kwa kuwa yeye ndio raisi. Huko ni kuendesha nchi kama duka la baniani. Hayo ni mambo ya kichifu, siyo nchi iliyo jamhuri.
Tukisema Magufuli hafai kuongoza hata kijiji mafisi wa Lumumba wanabisha!
Hivi huyu Magufuli anaposema NCHI NI TAJIRI SANA huwa anamdanganya nani?FEDHA ZIKO WAPI? Maana kama nchi ina fedha ni Tajiri sana inakuweje Rais anahamisha Fedha iliyopangwa kwa kazi maalumu na kuipeleka kwengine. What is Budget???
Nini maana ya BAJETI KUU YA SERIKALI inayopangwa na Serikali kupitia Bunge lake??
Huu utawala ni wa hovyo sana kuwai kutokea Tanzania......!!!!!!
 
Intuition sharti itumike wapi na wapi? Dodoma tayari mpango wa serikali ulikuwa kwenye hospitali ya BWM. Yeye rais kaona iongezwe nyingine tena kwa pesa ambayo ingetumika siku mbili au tatu tu! Sasa hapo aliyepotea nani kati yetu.
Hilo ndio tatizo. Unaamua mambo kwa hisia. Hospitali ya Dodoma sio emergency, kwamba ghafla tumekumbwa na tatzizo lazima tupate fedha haraka kwa kuwa hatukuwa tumetenga fedha za kuijenga na tunakabiliwa na ugonjwa hatari ambao utatibiwa katika hii hospitali. Kuongeza hospitali nyingine Dodoma ni jambo sahihi sana tu, lakini kuna emegency gani huko kiasi lazima iongezwe sasa? Kwa wazo hil lisipelekwe Wizara ya Afya ili katika mipango ya budget ijayo ijumuishwe?

Intuition ni jambo zuri, lakini intuition kwenye kitu kama kujenga hospitali ambayo wala sio emergency ni kukosa tu akili ya kupanga. Intuition katika kipindi cha Magufuli imefanya ytuanze miradi mikubwa bila kuangalia tutaimaliziaje, kisha tunaanza kuhangaika kutafuta fedha. SGR, tunajadli mkopo na Standard Chartered Bank BAADA ya kuanza kujenga. Then tunakuwa desparate. Unaamua kushona koti bila kujua ukubwa wa kitambaa ulicho nacho. Akili hiyo? NI udhaifu. Kutafuta kiki za siasa.
 
Mleta maada na wenzako wa kupinga kila kitu. Saa nyingine mpunguze ujuaji. Umeanza kwa kuita akili ndogo wale watakao unga mkono uamuzi huu. Wahenga walipatia kusema "werevu mwingi mbele kiza".

Kuna kitu kinaitwa intuition. Kiongozi mzuri pamoja na kufuata taratibu zilizopo anapaswa pia kuwa na utashi wake binafsi umwongoze kuchukua hatua za hapa na pale hata ikiwa hakuagizwa kufanya hivyo.

Uamuzi wa kujenga hospitali hiyo ulikuwa utashi binafsi. Kuna wale Bharti Airtel nao waliunga mkono kwa kuchangia huo ujenzi. Sasa rais kuamua pia kufuta hizo sherehe ili kupata pesa za kununulia vifaa tiba hizo ni akili zake binafsi ambazo kupinga lazima uwe na kawendawazimu flani kichwani.

Miradi inayopangwa iko mingi sana kiasi kwamba kudai kuwa hii miradi miwili mitatu ya utashi binafsi inaakisi mwelekeo wa jamii nzima kuwa mambo yetu hayako planned ni zaidi ya ujuha! Labda kama mnaigiza.

Natambua namna vichwa vyenu viko brainwashed na mfumo wa maisha wa kiliberali ambao mamlaka pekee makubwa kiongozi wa nchi anapaswa kuwa nayo ni kutangaza vita au kuitangazia vikwazo nchi flani. Hapo ndio roho zenu husuuzika nyie watumwa.
Umenena vyema sana
Pata soda bariiidi kwanza upoze koo
 
Tatizo ni kwamba watu kama wewe hamna uwezo wa kufikiri. Unasoma lakini huelewi.

Hatukatai kuokoa fedha, tunachokataa ni kutokuwa na mipango. Tunachosema hapa ni kwamba serikali haina mipango na budget ya kujenga hospitali ndio maana inaokoteza. Haya, hospitali ya Dodoma mmeokoteza fedha za Uhuru, na ya Morogoro je, tutauza magari ya Ikulu au ndege ya raisi?
Sawa kwa watu kama wewe, mnataka Serikali ieleze "mipango" yake labda miezi sita au saba kabla ya kuutangazia umma mpango au uamuzi huo? Hivi unadhani Serikali au Rais hakuwa na mpango wa hiyo hospitali? Unadhani kafanya uamuzi tarehe 02/12/2020 na kisha kumueleza Waziri Mkuu akatangaze, kweli!? Mipango ipo na ni suala ya kuujulisha umma tu utekelezaji wake. Hizo Bilioni 2.3/= za ujenzi wa hiyo hospitali baada ya kutoa zile Milioni 900/=+ za walai za sherehe zile za kwanza zilitoka wapi, kama siyo kwenye bajeti ya Serikali na vyanzo vingine kama alivyo elezea PM!? Mbona wapinzani mnakuwa wagumu na wazito kuelewa vitu rahisi rahisi kama hivi!?
 
... nje ya mada; ina maana 09-12-2020 haitakuwa siku ya mapumziko ama?
 
Sawa kwa watu kama wewe, mnataka Serikali ieleze "mipango" yake labda miezi sita au saba kabla ya kuutangazia umma mpango au uamuzi huo? Hivi unadhani Serikali au Rais hakuwa na mpango wa hiyo hospitali?
Kama alikuwa na huo mpango na katika kupanga akaamua ataokoteza fedha mahali, basi ni kweli hafai kuwa raisi.

Angekuwa anajua uongozi huo mpango anagemwagiza Waziri wa afaya aujumuishe katika bajeti ya Wizara

By the way, hii pia ni dalili kwa nini Magufuli hataki mawaziri. Anataka kila kitu afanye yeye. Sasa ni mtu wa aina gani huyo?
 
Tofauti kubwa kati ya Tanzania na North Korea ni kuwa North Korea hakuna nyumba za matope na nyasi, serikali imejenga nyumba (flats) kwa mahitaji ya raia wote wasio na uwezo wa kujenga au kununua. Huduma zao za kijamii ni bora zaidi.
Hujazungumzia suala la uchumi.
 
Yaani walitenga fedha za kutosha za sherehe za uhuru wakaacha kutenga fedha za kutosha za ujenzi wa hospitali Dodoma hadi Rais aje kuamuru fedha za uhuru zikajenge hospitali; ajabu sana hii!

Halafu kama ni uhitaji wa mahospitali na huduma nyingine za kijamii mahitaji ni mengi; ni bora sasa kama kinachokausha hazina ya taifa ni sherehe za uhuru imefika wakati sasa sherehe hizo zifutwe kabisa ili kupata fedha za kujenga na kuboresha huduma zote za jamii.
dudus,
Well said. Hii nji kwa sasa inaongozwa na mtu asiye na maadili ya Uongozi
Bunge huwa linakaa kila mwaka na kupanga Bajeti ya Serikali kwa kila Wizara,Idara na Taasisi zake.
Inashangaza sana kusikia Rais anahamisha Fedha iliyotengwa kulingana na Bajeti na kuipeleka kule akili yake inamtuma. JE, WIZARA YA AFYA HAIKUTENGEWA FEDHA KWA AJILI YA UJENZI WA HOSPITAL HIYO???Hapa ndipo Maneno ya baba wa Taifa Mwl. Nyerere yanapo jidhihirisha wazi kuwa Rais analala na kupewa ushauri na mkewe halafu anatumia ushauri huo kutawala nji!Hatujui kesho atasema nini!!
 
Kwa mtu mwenye akili za chini, atamsifia Rais Magufuli kwa kutangaza kwamba mwaka huu hatutakuwa na sherehe za uhuru ili kuokoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya Dodoma. Kwa mtu mwenye akili ya kufikiria, atajiuliza, hivi inakuwaje tunakuwa hatuna mipango hususa inayotia ndani kutengwa kwa fedha kwa ajii ya ujenzi wa miundo mbinu muhimu kama hospitali Dodoma?

Naingia sana wasiwasi, kwamba inafikia mahali mambo muhimu kwa ajili ya miundo mbinu na miradi ya nchini hayapangwi kwa kufuata uratatibu maalum, bali inakuwa ni uamuzi kutokana na hisia za Rais Magufuli. Kuamua kujenga barabara ndefu ya kiwango cha lami kwa ghafla na kumpigia simu mkurugenzi wa TANROAD, au kuamua ghafla kwamba fedha za uhuru ndio zikajenge hospitali, ni wonyesho dhahiri wa udhaifu mkubwa sana katika uongozi wa Magufuli katika kuwa na mipango hususa ya miradi ya maendeleo nchini. Magufuli asifikiri hiyo inamfanya kuwa raisi bora au mzalendo. Ni udhaifu katika uongozi.

Labda tungemuelewa Magufuli ikiwa angesema fedha za sherehe za Uhuru zinaenda kusaidia emergency fulani, kama mafuriko, kipindupindu kimezuka mahali, nk. Lakini kupeleka fedha za sherehe kwenye kujenga hospitali, kitu ambacho kinapaswa kupangwa na kutengewa fedha toka mapema, ni udhaifu mkubwa katika kupanga. Kwa namna hii kuna siku tutauza Ikulu ili tumalizie SGR!

Hautuwezi kufanikiwa kufanya mambo haya kwa kutegemea Rais Magufuli siku hiyo kawaza nini kichwani, au kasukumwa na nini kabla hajachukua simu na kutoa agizo mradi fulani mkubwa nchini utekelezwe fedha atajua kwa kuzipata kwa kuwa yeye ndio raisi. Huko ni kuendesha nchi kama duka la baniani. Hayo ni mambo ya kichifu, siyo nchi iliyo jamhuri.
Napita tu
 
dudus,
Well said. Hii nji kwa sasa inaongozwa na mtu asiye na maadili ya Uongozi
Bunge huwa linakaa kila mwaka na kupanga Bajeti ya Serikali kwa kila Wizara,Idara na Taasisi zake.
Inashangaza sana kusikia Rais anahamisha Fedha iliyotengwa kulingana na Bajeti na kuipeleka kule akili yake inamtuma. Hapa Maneno ya baba wa Taifa kuwa Rais a analala na kupewa ushauri na mkewe halafu anatumia ushauri huo kutawala nji!
MKuu sasa unaelewa kwa nini hataki mawaziri. Kuna siku atasema BUnge lisifanye mikutano ili tuokoe fedha za kumalizia Stiegler Gorge!
 
Kwa mtu mwenye akili za chini, atamsifia Rais Magufuli kwa kutangaza kwamba mwaka huu hatutakuwa na sherehe za uhuru ili kuokoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya Dodoma. Kwa mtu mwenye akili ya kufikiria, atajiuliza, hivi inakuwaje tunakuwa hatuna mipango hususa inayotia ndani kutengwa kwa fedha kwa ajii ya ujenzi wa miundo mbinu muhimu kama hospitali Dodoma?

Naingia sana wasiwasi, kwamba inafikia mahali mambo muhimu kwa ajili ya miundo mbinu na miradi ya nchini hayapangwi kwa kufuata uratatibu maalum, bali inakuwa ni uamuzi kutokana na hisia za Rais Magufuli. Kuamua kujenga barabara ndefu ya kiwango cha lami kwa ghafla na kumpigia simu mkurugenzi wa TANROAD, au kuamua ghafla kwamba fedha za uhuru ndio zikajenge hospitali, ni wonyesho dhahiri wa udhaifu mkubwa sana katika uongozi wa Magufuli katika kuwa na mipango hususa ya miradi ya maendeleo nchini. Magufuli asifikiri hiyo inamfanya kuwa raisi bora au mzalendo. Ni udhaifu katika uongozi.

Labda tungemuelewa Magufuli ikiwa angesema fedha za sherehe za Uhuru zinaenda kusaidia emergency fulani, kama mafuriko, kipindupindu kimezuka mahali, nk. Lakini kupeleka fedha za sherehe kwenye kujenga hospitali, kitu ambacho kinapaswa kupangwa na kutengewa fedha toka mapema, ni udhaifu mkubwa katika kupanga. Kwa namna hii kuna siku tutauza Ikulu ili tumalizie SGR!

Hautuwezi kufanikiwa kufanya mambo haya kwa kutegemea Rais Magufuli siku hiyo kawaza nini kichwani, au kasukumwa na nini kabla hajachukua simu na kutoa agizo mradi fulani mkubwa nchini utekelezwe fedha atajua kwa kuzipata kwa kuwa yeye ndio raisi. Huko ni kuendesha nchi kama duka la baniani. Hayo ni mambo ya kichifu, siyo nchi iliyo jamhuri.
Ndio ishakua.
 
Kwa mtu mwenye akili za chini, atamsifia Rais Magufuli kwa kutangaza kwamba mwaka huu hatutakuwa na sherehe za uhuru ili kuokoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya Dodoma. Kwa mtu mwenye akili ya kufikiria, atajiuliza, hivi inakuwaje tunakuwa hatuna mipango hususa inayotia ndani kutengwa kwa fedha kwa ajii ya ujenzi wa miundo mbinu muhimu kama hospitali Dodoma?

Naingia sana wasiwasi, kwamba inafikia mahali mambo muhimu kwa ajili ya miundo mbinu na miradi ya nchini hayapangwi kwa kufuata uratatibu maalum, bali inakuwa ni uamuzi kutokana na hisia za Rais Magufuli. Kuamua kujenga barabara ndefu ya kiwango cha lami kwa ghafla na kumpigia simu mkurugenzi wa TANROAD, au kuamua ghafla kwamba fedha za uhuru ndio zikajenge hospitali, ni wonyesho dhahiri wa udhaifu mkubwa sana katika uongozi wa Magufuli katika kuwa na mipango hususa ya miradi ya maendeleo nchini. Magufuli asifikiri hiyo inamfanya kuwa raisi bora au mzalendo. Ni udhaifu katika uongozi.

Labda tungemuelewa Magufuli ikiwa angesema fedha za sherehe za Uhuru zinaenda kusaidia emegerncy fulani, kama mafuriko, kipindupindu mahali kimezuka, nk. Lakini kupeleka fedha za sherehe kwenye kujenga hospitali, kitu ambacho kinapaswa kupangwa na kutengewa fedha toka mapema, ni udhaifu mkubwa katika kupanga. Kwa namna hii kuna siku tutauza Ikulu ili tumalizie SGR!

Hautuwezi kufanikiwa kufanya mambo haya kwa kutegemea Rais Magufuli siku hiyo kawaza nini kichwani, au kasukumwa na nini kabla hajachukua simu na kutoa agizo mradi fulani mkubwa nchini utekelezwe fedha atajua kwa kuzipata kwa kuwa yeye ndio raisi. Huko ni kuendesha nchi kama duka la baniani. Hayo ni mambo ya kichifu, siyo nchi iliyo jamhuri.
Mleta mada uelewa wako wa mambo uko chini sana. Nenda kasome kuna kitu kinaitwa “Mid Year Review” au “Budget Reallocation” vitakusaidia kuelewa. Hivyo vitu unaweza kujisomea kwenye internet au tafuta Sheria ya Bajeti. Hayo mambo Serikali inafanya kila mwaka kama kuna uhitaji wa kuhamisha Bajeti kutoka Activity A kwenda Activity B.
 
Wewe ni Punguani kabisa, hivi hawa watoto wanaokua sasahivi wajifunze nini juu ya Sherehe za Uhuru?

Ikiwa Uhuru hawakuuona na Sherehe zake wasizione?

Inchi inayoghairi Sherehe za kitaifa kwa Mujibu wa Katiba ni Nchi mfu.
Uko sahihi kabisa. Jamani sherehe za UHURU sio japo la kisiasa ni jambo la kihistoria. Nyerere na wenziwe walipoteza nguvu nyingi kuutafuta uhuru wa nchi. Duniani sis ndo wa kwanza kubeza tukio hilo. Watawala eti wata save mil 834. Hizo ni sawa na gharama ya V8 3. Watoto wananyimwa haki yao ya kushuhudia wanachokisoma kwenye vitabu kwa vitendo. Wanaharisha kutafuta political mileage au umaarufu wa kisiasa sio kusave gharama. Tunaua historia ya nchi hii. Nyerere uko alipo anasikitishwa na uimla wa namna hii.
 
MKuu sasa unaelewa kwa nini hataki mawaziri. Kuna siku atasema BUnge lisifanye mikutano ili tuokoe fedha za kumalizia Stiegler Gorge!
Uko sahihi mkuu.
Hapo alipo anaona ataokoa mishahara kwa miezi 2-4 kwa kutoteua Mawaziri halafu mwisho wa siku atajisifu! Akili ya ajabu kabisa!
Huyu Rais ni wa ajabu sana. Huwa ana tamani ASHIKE KILA WIZARA hasa Wizara ya Fedha alikomweka mtoto wa dadake a.k.a mjomba!!!
Miaka 5 mingine tutashuhudia mahoka na vihoja lukuki!
 
Sherehe za Uhuru zinamaliza hela tu. Hongera Rais Magufuli kwa kuliona hilo. Hii nchi imepigwa sana enzi za Kikwete kupitia visherehe vya ajabu ajabu.
Na wewe uache kufanya sherehe za birth days zako. Unamaliza hela bure! Uwe mfano pia.
 
Uko sahihi kabisa. Jamani sherehe za UHURU sio japo la kisiasa ni jambo la kihistoria. Nyerere na wenziwe walipoteza nguvu nyingi kuutafuta uhuru wa nchi. Duniani sis ndo wa kwanza kubeza tukio hilo. Watawala eti wata save mil 834. Hizo ni sawa na gharama ya V8 3. Watoto wananyimwa haki yao ya kushuhudia wanachokisoma kwenye vitabu kwa vitendo. Wanaharisha kutafuta political mileage au umaarufu wa kisiasa sio kusave gharama. Tunaua historia ya nchi hii. Nyerere uko alipo anasikitishwa na uimla wa namna hii.

Kinachoonekana au kujificha kwa huyu jamaa ni Roho mbaya na Uchoyo.
Anajua sherehe za Uhuru zikifanyika watu watalipwa hela za posho kujikimu na yeye hataki!!!
Kama Rais anaweza toa kauli tata kama "....WALE WALIOKUWA WANAPATA MISHAHARA MIKUBWA NITAWASHUSHA WAISHI KAMA MWASHETWANI..." mwisho wa kunukuu.
 
Kwa mtu mwenye akili za chini, atamsifia Rais Magufuli kwa kutangaza kwamba mwaka huu hatutakuwa na sherehe za uhuru ili kuokoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya Dodoma. Kwa mtu mwenye akili ya kufikiria, atajiuliza, hivi inakuwaje tunakuwa hatuna mipango hususa inayotia ndani kutengwa kwa fedha kwa ajii ya ujenzi wa miundo mbinu muhimu kama hospitali Dodoma?

Naingia sana wasiwasi, kwamba inafikia mahali mambo muhimu kwa ajili ya miundo mbinu na miradi ya nchini hayapangwi kwa kufuata uratatibu maalum, bali inakuwa ni uamuzi kutokana na hisia za Rais Magufuli. Kuamua kujenga barabara ndefu ya kiwango cha lami kwa ghafla na kumpigia simu mkurugenzi wa TANROAD, au kuamua ghafla kwamba fedha za uhuru ndio zikajenge hospitali, ni wonyesho dhahiri wa udhaifu mkubwa sana katika uongozi wa Magufuli katika kuwa na mipango hususa ya miradi ya maendeleo nchini. Magufuli asifikiri hiyo inamfanya kuwa raisi bora au mzalendo. Ni udhaifu katika uongozi.

Labda tungemuelewa Magufuli ikiwa angesema fedha za sherehe za Uhuru zinaenda kusaidia emergency fulani, kama mafuriko, kipindupindu kimezuka mahali, nk. Lakini kupeleka fedha za sherehe kwenye kujenga hospitali, kitu ambacho kinapaswa kupangwa na kutengewa fedha toka mapema, ni udhaifu mkubwa katika kupanga. Kwa namna hii kuna siku tutauza Ikulu ili tumalizie SGR!

Hautuwezi kufanikiwa kufanya mambo haya kwa kutegemea Rais Magufuli siku hiyo kawaza nini kichwani, au kasukumwa na nini kabla hajachukua simu na kutoa agizo mradi fulani mkubwa nchini utekelezwe fedha atajua kwa kuzipata kwa kuwa yeye ndio raisi. Huko ni kuendesha nchi kama duka la baniani. Hayo ni mambo ya kichifu, siyo nchi iliyo jamhuri.
Nchi inaendeshwa kama gari mbovu
 
Back
Top Bottom