Anamaanisha kuvunja halmashauri ya jijiYan akivunja maana yake kutakuwa hakuna Dar es Salaam. Au nimeelewaje! Badala yake ilala ndo itakuwa jiji kama sasa tunavosema jiji la dar es salaam. Niko sahihi au.
Ukiangalia kwa makini ni kweli hawakuchaguliwa na wananchiNimependa hapo hawakuchaguliwa na wananchi.
Uzuri wa huyu Mjomba huwa hanaga siri kabisa.
Wale madiwani wanaokaa vikao vya jiji hawamwakilishi yeyote pale tofauti na madiwani wa manispaa.He! Kwahiyo kinondoni, temeke, kigamboni ziwe manispaa alafu Ilala ndio jiji?
So jina la Dar Es Salaam ndio litakuwa kwishney?
Shetani hana rafiki , Mambosasa alipotetea kura za mabegi Kawe tulimpinga lakini watu hawakutuelewa , pembe la ng'ombe halifichiki , leo aliyewatuma karopoka mchana wa jua kali !'kwanza hawakuchaguliwa na wananchi' Kaanza kutoboa siri
Nafikiri unaweza kusoma post yangu. Miji mingi duniani inakua na mambo mawili. Jambo la kwanza ni kuteua Urban proper na kuifanya ni Jiji na pembezoni wanaipa Metropilitan Areas. Nilitoa mfano wa Maputo, Maputo ni Jiji kuu la nchi ya Msumbiji lakini pia kuna Jimbo la Maputo, ambalo mji mkuu wa jimbo ni Matola, lakini ni hapo hapo Maputo pembezoni na hawaingiliani kiutawala na jiji la Maputo, na umbali kutoka Maputo kama hakuna foleni ni dk 30 tu unakua umeingia Jijini Maputo. Hii pia ipo Jiji la Kinshasa(Gombe) na jimbo la Kinshasa, vyote vikiwa mji mmoja lakini Mamlaka tofauti.hapana amesema Dsm itabaki kuwa jiji lkn kutakuwa na halmashauri moja tuu ndiyo itakayobeba jiji haalmashauri nyingine zote zitaondolewa hadhi ya jiji
binafsi sijaelewa itafanyikaje
Napongeza uamuzi wa kulivunja Halmashauri ya Jiji maana lilikuwa redundant.Katika hali ya mh rais kuonesha anafaham jinsi ambavyo uchaguzi uliendeshaa na amechukizwa sana aliamua kuwapasulia ukweli madiwani ambao wamekaa tu wanaotesha vitambi hawana wanalowaza sababu hawakuwa na mipango yoyote.
Tupate habari kamili.
View attachment 1710962
😷 😷 😷 😷 😷Shetani hana rafiki , Mambosasa alipotetea kura za mabegi Kawe tulimpinga lakini watu hawakutuelewa , pembe la ng'ombe halifichiki , leo aliyewatuma karopoka mchana wa jua kali !
Shanwe kwa rais ambae ni juzi tu hapa amesimama na kusema siku ina masaa 48! Clip inasambazwa kwa kasi mno na watu wanapata sababu ya kucheka na kufurahi!Akiwa katika uzinduzi wa daraja la juu Ubungo amesema atalivunja jiji na kuipa Ilala hadhi ya jiji na wilaya zingine zibaki kuwa Manispaa.
----
Rais Magufuli ameyasema haya
Nategemea Jiji la Dar es Salaam kulivunja na hii nawaambia hapa ili tutengeneze jiji la eneo fulani, tunaweza tukaifanya Ilala ndio ikawa jiji, ita-depend na mambo yatakavyoenda lakini kuwa na madiwani ambao wanakaa hapa juu, wanachangiwa hela, hawana miradi ya maendeleo, wanakula posho na hawakuchaguliwa na watu, hili nitalikataza.
Kwa hiyo ninalizungumza hapa, wale wanaojiandaa kuwa Mameya wa jiji la Dar es Salaam na wanakaa hawana maeneo wajue hicho kimekwisha. Tunataka Manispaa moja katika jiji la Dar es Salaam ndio ipandishwe hadhi iwe jiji halafu nyingine ziwe manispaa, ni kama ilivyo katika majiji mengine.
Kwahiyo mjiandae kisaikolojia wale waliokuwa wanataka umeya wajiji la Dar es Salaam, meya atapatikana kutoka Ilala au kutoka manispaa mojawapo ya hapa, huu ndio ukweli na ukweli utabaki kuwa ukweli na draft nimeshaletewa na mheshimiwa Jafo, nafikiri nikitoka huku nitakwenda kuisaini.
Ili turahisishe mambo, bajeti ya jiji ambayo haipo, fedha zilikuwa zinapotea ndugu zangu waheshimiwa wabunge, jiji la Dar es Salaam litaendelea kuwepo lakini tutachukua eneo fulani nafikiri Ilala inafaa kuwa jiji, ndio katikati ya jiji la Dar es Salaam, wewe Ubungo utasubiri kwanza kwasababu hata barabara bado hazijatengenezwa tengenezwa lakini nafanya haya ndugu zangu kwa kuangalia matumizi mazuri ya fedha zetu. Mwiso wa Nukuu
is it?Ukitaka kula hela peke yako hasa katika kipindi chako cha mwisho cha madaraka , dhibiti jiji la DSM lenye mapato mengi , hivi ndivyo alivyofanya Mkapa , alivunja halmashauri ya Jiji na kumweka rafiki yake Keenja kuwa Mkurugenzi , baada ya muda mfupi wote wakawa matajiri wa kutupwa .
Wakati mwingine ni vizuri kuficha ujinga badala ya kuleta hadharani kwa kuwa mnaunga mkono ujinga. New York City na New York, kama ilivyo Washington DC na Washington ni vitu viwili tofauti, mawili ni Majiji na mawili ni Majimbo Kati ya Majimbo 50 ya Marekani ndo maana ukitaja au kuulizia Jiji la New York lazima uongeze City vivyo hivyo Washington DC (District of Columbia) ni Makao Makuu ya Marekani na Majiji yote yako karibukaribu mashariki mwa Nchi. Majimbo ya Washington na New York yako karibukaribu Magharibi mpakani na Bahari ya Pacific lakini yako mbali sana na hayo Majiji yaliyopo karibu na Bahari ya Atlantic. Waunga mkono juhudi wasingekuwa vilaza wangekuwa wanajua vizuri Jimbo la New York maana ndiko yanatengenezwa madege ya Magufuli ya Dreamliner ambayo wanatuimbia na kuturingia kila siku yakiwa yamepark tu kama ya maonyesho. Greater Manchester (au Jiji lolote) ni eneo lote ndani ya mipaka iliyotengwa kwa ajili ya Jiji lililopo na upanuzi wa baadaye. Someni muachane na ujinga!Exactly!
New York City inside New York.
Manchester City inside (Great) Manchester.
Cairo inside (Great) Cairo.
Hebu kumbuka Keenja alivyoteuliwa kuwa Mkurugenzi wa jiji , hiki ndicho anachokitaka jiwe , kuna mtu mmoja wa kitengo alishanivutia uzi kunidokeza .is it?
Tutakuwa na Dar Metropolitan. Ikiwa na jiji la Ilala, Manispaa ya Kino, Ubungo, TMK na Kiga.Kwahiyo madiwani walichaguliwa na nani? (Anathibitisha wizi wa kura kufanyika?)
Kwahiyo jiji la Dar Es Salaam linaenda kuwa historia? (Dar inakuwa ya "mikoani")
Ikiwa Jiji la Dar linaenda kufa, jiji kubwa kuliko yote Tz linaenda kuwa Mwanza.... (ok ok ok inaeleweka)
Ukienda kutafuta majiji makubwa East Africa, Nairobi anakosa mpinzani rasmi.
Mimi na wewe nani wakuficha ujinga?!Wakati mwingine ni vizuri kuficha ujinga badala ya kuleta hadharani kwa kuwa mnaunga mkono ujinga. New York City na New York, kama ilivyo Washington DC na Washington ni vitu viwili tofauti, mawili ni Majiji na mawili ni Majimbo Kati ya Majimbo 50 ya Marekani ndo maana ukitaja au kuulizia Jiji la New York lazima uongeze City vivyo hivyo Washington DC ni Makao Makuu ya Marekani Majiji yote yako mashariki mwa Nchi.
Ambalo tofauti yake na hili la sasa ni nini?Tutakuwa na Dar Metropolitan. Ikiwa na jiji la Ilala, Manispaa ya Kino, Ubungo, TMK na Kiga.
Madiwan wa jiji la Dar wanatoka kwenye manispaa zotë nadhan kila manispaa inachagua madiwan watano kuingia kwenye jiji hio ndo concept ya mh rais. Hawachaguliw moja kwa moja na wananchi kwenda jijiHawakuchaguliwa na wananchi ?Hapo sijaelewa. Au kwenye udiwani kuna viti maalum ?Pia Ilala kuwa Jiji sababu ni nini?
Ikishakua hivyo impact yake ni ipi hasa kiujumla? Kwenye nyanja ya uchumi na social services..... wala usipate tabu, ni concept rahisi sana. Ili uipate vizuri, tuchuke mji ambao jina lake sio jina la mkoa mfano Moshi.
Moshi iko katika mkoa wa Kilimanjaro na ina hadhi ya manispaa. Moshi na Kilimanjaro ni ipi kubwa? Ni Kilimanjaro; Moshi ni mji/Manispaa ndani ya Kilimanjaro kama itakavyokuwa jiji la Ilala ndani ya mkoa wa Dar-es-Salaam.
Ukiacha Moshi, Kilimanjaro ina halmashauri nyingine kadhaa ambazo ziko katika wilaya ngingine nje ya Moshi - Halmashauri ya Wilaya ya Same (ndani ya Wilaya ya Same); Halmashauri ya Wilaya ya Hai (ndani ya Wilaya ya Hai); Mwanga, Siha, Rombo, n.k. kama ambavyo kutakuwa na Mainspaa ya Temeke (ndani ya Wilaya ya Temeke), vivyo hivyo Ubungo, Kinondoni, n.k. katika Mkoa (sio jijji) wa Dar-es-Salaam.