Rais Magufuli mtumbue Bosi wa TTCL anaihujumu kampuni

Namba hazidanganyi,

Kindamba kaikuta TTCL mahututi mbapaka sasa inatoa gawio serikalini. Tatizo kuu lilikua ni mtaji na hakupewa,anafanya maboresho kutokana na mtaji mdogo uliopo,hata awekwe mwingine hataweza kufanya zaidi ya huyu Kindamba.
Mi nashangaa wanatoa gawio serikalini huku mtandao wao ukiwa na huduma mbovu ya intaneti kuliko mitandao yote, yaani nipo Dar tu ila kufungua hata picha ya Whatsapp ni mtihani kwa TTCL

Hizo hela kwa nini wasitumie kuboresha?


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi nampongeza Sana Kindamba ameleta mageuzi makubwa Sana TTCL,kutoka kuzalisha hasara kwa miaka 18 iliyopita mpaka kutengeneza faida na kutowa gawio kwa serikali.sikatai kwamba ttcl Wana changamoto zao especially za kiubunifu mfano kwenye bando zao bado wamebase kwenye watumiaaji wadogo wa data na voice mfano kwenye data ukiangalia bando zao nyingi mb200 mb500 1gb zikizidi Sana 5gb kwa mwezi ni kweli kwamba Bei zao ziko fair ila wawalenge na watumiaji wakubwa kuanzia gb 5 na kuendelea mpaka gb 100 kwa mwezi.

Kwa Bei nzuri maana kwanza ttcl ndo wanamiliki mkonga wa taifa kwahiyo hata iyo mitandao mingine wanawauzia wao ili waweze kusafirisha data zao huko kuwafikia watumiaji wa mwisho kwahiyo ttcl bando zao zinatakiwa ziwe chini kuliko mitandao mingine ili kuvutia wateja. Kingine ttcl iongeze upatikanaji wa vocha ni kweli unaweza kununua vocha kwenye simu na mitandao mbalimbali lakini Kuna yule mtu wa kijijini kabisa hajui ilo ameshazoea vocha za kukwangua kwahiyo waliangalie na Hilo.

Pia waongeze matangazo, kindamba najua unapenda kusave Ela ili kuongeza faida lakini sio kwenye matangazo jitaidini Sana kuongeza matangazo kila mahali mf, kwenye tv,barabarani,toweni ata Ile miavuli vile vile kwenye tpesa tumieni Ile njia ya Airtel money ya hakati mtu ikisha kubalika zaidi ndo mnaweka charges kidogo.kingine Kuna Huduma nyingi za ubunifu mfano Kuna wale wateja wa uhakika watengenezeeni Huduma ya post paid na prepaid tengeneza package za uhakika za mwezi mkilenga voice na data then mnafanya ka research kadogo then mnatengeneza hiyo.mkizingatia ivyo hamna mitandao utakao wazuia The Black Godfather,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pia sijui Kama ni kwangu tu, bando zao zinaisha haraka sana kulikoni matumizi harisi
Halafu ukitumia simu kadi yao huwezi kutuma sms 2 in 1
Kujiunga baadhi ya vifurushi hadi utumie app yao
Ukipiga huduma kwa wateja unaambiwa uweke message center namba wakati sms zingne zinaenda.
Kweli hawa wanashida tu,,,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Anachojua yeye nikutoa kagiwio kwa serikali huduma mbovu.
 
Nadhani sasa TTCL ingetakiwa iwe imeshashika kila kona ya nchi.

Matangazo hawana kabisa Ukiskiliza radio au tv utamuona Tigo/Voda/Halotel wanavyochuana.

Nadhani marketing manager hamna kitu kabisa. Labda tuwape mwaka mmoja wa matazamio kama wataweza shindana na hawa wengine
 
Huu ndio Upumbavu walionishauri...... Nataka kuweka 1000... Naenda MPesa kuwaomba waniwekee Buku, buku nahamishia TTCL inakuwa tena ni Buku???


Kampuni zote wana Vocha kasoro TTCL pekee ndio hawana Vocha........

Sent using Jamii Forums mobile app
Nensa kwa wakala na Tsh 1050 tu kisha irushe kwenye Tigo Pesa yako then hamisha kutoka tigopesa kwensa T Pesa unakatwa tsh 15
 
Mimi ni mteja wa TTCL kwa miaka mingi, ninatumia simu ya mezani, natumia MI-FI na mobile
kuangalia salio kwa mobile iko standard kwa wote piga *102# kuona salio lako au kwa upande wa vifurushi piga *148*30# select number 9

Sawa kiongozi, ila procedure ndefu sana kwa TTCL unajibu maswali mengi kama vile unatuma pesa

*148*30#
  1. Jiachie
  2. T-Connect
  3. Serereka
  4. TTCL
Answer 6 Ofa maalumu 1 ...watumishi ofa
  1. bundle
  2. data
  3. huduma za sauti
Answer 3 ..
  1. Vifurushi siku
  2. Vifurushi wiki
  3. Vifurushi Mwezi >>>
Tigo wao ni *102*01hash inakupeleka kwenye salio lako
 
Hawana plan ya kujipanua na kuleta ushindani wakati kila kitu wanacho
 
Huyu Waziri Kindamba ni kada wa CCM, bado yupo yupo sana, vumilieni tu. Ila biasharaTTCL ni kubwa kuliko ubongo wake.
 
calm down man! Relax!
 
Namba hazidanganyi,

Kindamba kaikuta TTCL mahututi mbapaka sasa inatoa gawio serikalini. Tatizo kuu lilikua ni mtaji na hakupewa,anafanya maboresho kutokana na mtaji mdogo uliopo,hata awekwe mwingine hataweza kufanya zaidi ya huyu Kindamba.
Ujinga ni pale TTCL inatowa gawio kwa Serikali la Tsh 1.0 Bilion halafu baada ya siku 60 inakwend kwa Treasury Registrar kupeleka maombi ya Tsh 360 Bilion kwa ajili ya kuboresha miundombinu
 
Ujinga ni pale TTCL inatowa gawio kwa Serikali la Tsh 1.0 Bilion halafu baada ya siku 60 inakwend kwa Treasury Registrar kupeleka maombi ya Tsh 360 Bilion kwa ajili ya kuboresha miundombinu
Hujui accounts and financing ndio.maana unaona ni ujinga
Kupata faida na kutoa gawio,hakukuzuii kuomba mkopo au capital injection toka kwa shareholder kwa ajili ya investment ya miundombino
 
TTCL ilipoinuka tena ilianza vema.
Hapo kati wamejitahidi kujitangaza hata imefika kipindi kwamba wafanyakazi wengi wa serikali na sekta binafsi tumeshawishika kisajili laini za TTCL.

Tatizo kubwa ni kwamba TTCL haiko RELIABLE.

Mfano:

1. unajiunga bando ya GB 3, lakini internet iko slow kuliko konokono.
2. Unajiunga bando ya internet baada ya dakika chache inakata signal kwa masaa mengi sanaaaa...wakati mwingine hata kwa siku kadhaaa.
3. Sijatumia TPESA lakini wengi wanalalamika huduma mbovu.
4.
5.
6.

Wateja wengi tunajikuta inabidi kuachana au kutupa line za TTCL na kuhamia mitandao mingine.

Swali:

Je? ndio kusema TTCL inahujumu jitihada za wananchi tunaorudi nyumbani.

Mbona nyumbani hakujanoga ?

Kuna wakati nafikiri safari ya TTCL italingana na ya ZANTEL.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tutampa babaaako pumbafuuu
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…