Uchaguzi 2020 Rais Magufuli na Tundu Lissu wote ni Wakatoliki wazuri. Je, Kanisa halioni umuhimu wa kuwapatanisha?

Imekosekana suluhu ya bunge laivu ijeipatikae sukuhu ya pyupyupyuu hatutaki suluhu
 
Lisu alilikana jina la kikatoliki la ubatizo alilobatiziwa akaamua kujipa jina la kienyeji kukufuru ukatoliki kuwa hauko sahihi kutaka watoto wapewe majina ya ubatizo ya watakatifu

Kitendo Cha Lisu kulikana jina la mtakatifu kukitumia Ni dharau kwa imani Katoliki
 
Kumbe ni mpagani? 😲
 
Hilo Kanisa kabla yakuwapatanisha lilipaswa litoe japo mstari wa neno kuhusu kupigwa risasi kwa muumini wao Bwana Lisu.
Makanisa(Viongozi wa dini baadhi) yalitakiwa yawe kipaza sauti cha wananchi lakini yamegeuka watetezi wa serekali.
 
Mwenzio jpm kwa sasa muda wote kawakusanya viongozi wa dini ili wampe kura.
Asilimia kubwa kama sio wote, viongozi wale ni wafanya biashara, wanajua fika kuwa waumini wanaowaongoza ni wafuasi wa vyama tofauti vya kisiasa. Na kama ambavyo serikali inavyojinasibu kuwa haina dini, na wao hawapaswi kuwalazimisha wafuasi wao kuchagua chama fulani cha kisiasa. Lakini kwa kulinda maslahi ya biashara zao zisijetoweka lazima wajipendekeze kwa haya ya kidunia.
 
Kwani wana ugomvi binafsi hadi kanisa kuingilia? Kila mmoja yupo kutetea maslahi ya chama chake, Kanisa linaingia vipi hapo, ni mtizamo wangu tu
 
Tangu nasoma mpaka sasa sijawahi ona hasi na chanya vikikaa sehemu moja kwa ushirikiano
 
Kwa hili, naweza kuchangia hivi:
1. Ni kweli wote ni Wakatoliki.
2. Kanisa linaweza kuwapatanisha kama ni maadui wanaotaka kupatanishwa.
3. Lakini sioni kama ni maadui, bali ni wenye itikadi, mitazamo na 'approaches' tofauti za kisiasa.
 
Hawana ugomvi ila wana tofauti za kimtizamo na kimkakati. Kama watu wana mitizamo tofauti huwezi kuwapatanisha, Kwa mfano inawezekana mmoja anaamini kuwa ana mamlaka ya kufanya lolote analoona ni jema (wewe unaweza usione kama ni jema) na kweli kikatiba anayo mamlaka, na mwingine anaona si sawa kutumia mamlaka hayo hivyo, na hivyo anafikiri katiba ifanyiwe marekebisho ili hayo mamlaka yapunguzwe au yawekewe utaratibu wa kuyatumia. Katika hali hiyo Kanisa linaweza kuingiliaje?
Kuna tofauti ambazo kanisa linaweza kuingilia na kusuluhisha kama vile ugomvi halisi, kuumizana, nk. Na ili kanisa liweze kufanya hivyo, lazima lisiwe na upande wowote iwe kwa kulaumu au kwa kusifia.
Lisu na Magufuli wakikutana kanisani watapeana mkono wa kutakiana amani ila wakipanda kwenye ulingo wa kisiasa - ni tofauti
 
Mshahamisha Goli tena???πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

Daaah!!! Lissu kweli anawavuruga Lumumba
 
Wewe vipi? Kanisa Katoliki liwapatanishe Lissu na Magufuli kwa lipi? Kwani wana ugomvi?
 
Nitagusia tuhuma za uongozaji wa kanisa Katoliki katika mauwaji ya mbari huko Rwanda 1994
Kanisa Katoliki halikusimamia mauaji ya kimbari ya Rwanda wacha kupotosha, waumini na wanaoahasimiana tena kwa sababu mbalimbali wengine hawakuwa hata wakristo walikimbimbilia kanisani

Mauwaji yalifanywa na kundi la MRND likiwa chini ya Theoneste Bagosora na Mkuu wa Redio Mille Collines mr Kabuga Felicien

Kuna baadhi ya wanaanchi waliuawa na kwenye Mto Kagera je utaulaumu Mto Akagera? kushirikianana kuuwa Wananchi wa Rwanda.

"Evil is inside us" lakini kama ilivyo hulka ya mwanadamuhuwa tunatafuta wa kumtwisha lawama

Yale mauaji ya Rwanda 1994 yalikuwa ya ni yakikabila hayakuwa ya kidini hata kidogo
 
Anayebwatuka kila siku ni Lissu, sijamsikia Magufuli kila anapoenda anataja Lissu Lissu.
Magufuli Hana muda na huyo poyoyo.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
Magufuli hawezi kukubali ataonekana anamnyenyekea ,hata hao watakaotoa wazo hilo watafakari vizuri yasije yakawakuta
 
Kupatanishwa na Lissu? Huyu mtu anayeuza nchi mchana kweupe? Labda kama kanisa halina kazi za kufanya.
Walioiuza Tanzania kwa wanaoitwa wawekezaji, huwajui ?!. Lissu alifunga nao mkataba gani mbovu ?!.
 
CCM waache kuonewa wapinzani wao kwa kutumia vyombo vya dola.

Kwanza Magufuli si aliambiwa akatubu na Askofu Kakobe ameshatubu ???

Utapatana vipi na mtu ambaye amegoma kutubu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…