kt the irreplaceable
JF-Expert Member
- Oct 12, 2017
- 2,375
- 4,893
Kwa nini kila azungumzapo yeye ni kulialia tunahujumiwa, hatupendwi, mabeberu wanatuonea nk nk?
Hivi tuna nini sisi hapa duniani kilicho cha kipekee hadi tushambuliwe kiasi hicho?
Tumeharibu biashara wenyewe, tumeua kilimo cha biashara chenye kuweza kubadili maisha ya watu wetu wenyewe na tumevunja mahusiano ya kijamii na kikanda kwa ubaguzi tulio anzisha wenyewe halafu tunatupia lawama za kilaghai kwa wengine?
CCM mtaacha lini usanii?
Sent using Jamii Forums mobile app
Jamani naomba mnaojua mnisaidie na mimi kuelewa jambo hili ,hivi hizi figure pointing za Magufuli zimeshamsaidia yeye na nchi yetu kwa kiwango gani hadi sasa?Kuna hujuma dhidi ya jitihada za Serikali zinazofanywa na baadhi ya wasioitakia mema Tanzania zikilenga kufifisha jitihada zetu za kujikomboa, kiuchumi kwa maslahi yao binafsi, kamwe hawataki kuona tunadhibiti rasilimali walizokuwa wakivuna na kusafirisha bila kuulizwa.
Wanaotuhujumu hawatakubali tutekeleze miradi ya kimapinduzi itakayoharakisha maendeleo, ikiwemo Bwawa la Nyerere, SGR au Kufufua Shirika la ATCL, wasingependa tutoe elimu bure n.k, wangependa tuendelee kuwategemea wao, ilihali wao wanaishi kwa kutegemea rasilimali zetu.
Wanatumia kila njia kufifisha jitihada zetu na kupenyeza ajenda zao,muda mwingine wanatumia Asasi za Kiraia na Mashirika yasiyo ya Kiserikali na kujifanya wanatufundisha Demokrasia na Haki za Binadamu, ilihali wenyewe wanavunja misingi hiyo kwa kujenga mifumo ya kinyonyaji.
Wanajifanya wanatufundisha Demokrasia ilihali wenyewe wanachochea machafuko na kuingilia uhuru wa Mataifa mengine, wanajenga hadi mazingira ya taharuki na kusema EBOLA imeingia Tanzania ili ionekane Nchi haiko salama, tusiposimama imara na kujenga uzalendo hatuwezi kushinda.
View attachment 1290479
Duuh, mie hapa nimetoka mtupu!I dont is is ahout CCM..Well we can make right all all wrong we hage done.
Hata mimi mtupu kabisa.tuvimivulane. Got that right?
Mzalendo ni shujaa ktk nchi yakeTuandamane au tufanyeje!! Mabeberu yanawajambisha Wachina,warusi, waajemi,wahindi sembuse sisi afrika akili ndogo ,,mkuu unajidanganya mchana kweupe tukubali hii dunia ni yao hivyo tushirikiane nao
“Kuna hujuma dhidi ya jitihada za Serikali zinazofanywa na baadhi ya wasioitakia mema Tanzania zikilenga kufifisha jitihada zetu za kujikomboa, kiuchumi kwa maslahi yao binafsi, kamwe hawataki kuona tunadhibiti rasilimali walizokuwa wakivuna na kusafirisha bila kuulizwa-JPM
_
“Wanaotuhujumu hawatakubali tutekeleze miradi ya kimapinduzi itakayoharakisha maendeleo, ikiwemo Bwawa la Nyerere, SGR au Kufufua Shirika la ATCL, wasingependa tutoe elimu bure n.k, wangependa tuendelee kuwategemea wao, ilihali wao wanaishi kwa kutegemea rasilimali zetu”-JPM
_
“Wanatumia kila njia kufifisha jitihada zetu na kupenyeza ajenda zao,muda mwingine wanatumia Asasi za Kiraia na Mashirika yasiyo ya Kiserikali na kujifanya wanatufundisha Demokrasia na Haki za Binadamu, ilihali wenyewe wanavunja misingi hiyo kwa kujenga mifumo ya kinyonyaji”-JPM
_
“Wanajifanya wanatufundisha Demokrasia ilihali wenyewe wanachochea machafuko na kuingilia uhuru wa Mataifa mengine, wanajenga hadi mazingira ya taharuki na kusema EBOLA imeingia Tanzania ili ionekane Nchi haiko salama, tusiposimama imara na kujenga uzalendo hatuwezi kushinda”-JPM
#JPMMwanza
We jamaa muongo sana.Waingereza walimshawishi Iddi Amin ampindue Obote hatimaye tuliona yaliyotokea, na wakamshawishi Nyerere aivamie Uganda, wakatutelekeza peke yetu, hadi uchumi wetu ukaharibika.
Leo hii wanatumia NGO na WHO kutudhibiti kwa kutumia chanjo za Polia na maradhi mengineyo, huku wachanganya dawa za kufunga uzazi, tuzizaane.
Kuna mengi yanafanywa tusiendele na wazidi kutudhibiti.
Sent using Jamii Forums mobile app
Pia ikiwezekana weka na vifungu vya biblia kuanzia mwanzo hadi kitabu cha samwel wa kwanza. Nchi ya Israel iliongozwa na Mungu mwenyewe lakini yaliyotokea bado tunashangaa waliwezaje kwenda kinyume?On the contrary kauli za namna hii si za kizalendo bali ni kibaguzi na kugawa watu, ionekane kuna kundi fulani ndiyo linaipenda nchi na lingine linahujumu nchi. Hii si kweli, when i read between lines anataka kuwafanyia ubaya kundi fulani la watu kwa kisingizio cha uzalendo.
Hakuna mtanzania asiyeipenda nchi yake, wanaokosoa wanakosoa ili taifa lisonge mbele na hii ni kawaida kwa mtu yeyote aliyepitia development studies misuguano ni jambo la kawaida. Na kwa waliosoma physics they know that there is no movement without friction. We unataka kuongoza nchi ambayo watu wametulia kama maji ya mtungi we ni nani? hakuna nchi ya hivyo, ajifunze kupanua kifua cha kupokea anayoyataka na asiyoyataka. That is what leadership entails.