Rais Mstaafu Kikwete ashangaa kuibuka kwa Machifu Tanzania "Uchifu ulishakufa"

Rais Mstaafu Kikwete ashangaa kuibuka kwa Machifu Tanzania "Uchifu ulishakufa"

Naona yeye amesahau kuwa aliwahi kutawazwa kuwa chifu wa uluguru, chifu wa Missenyi, na huko usukumani aliitwa chifu Masanja. Mbona hakuhoji wakati huo? Anamuonea wivu rais Samia kupewa uchifu.
 

Zilongwa Mbali, Zitendwa Mbali

kudos Kikwete kwa hili!
Wivu tu wa JK kw Samia kwa vile anaupiga mwingi. Mbona yeye hapo October 2013 alitawazwa Chifu wa Wabena?
Screenshot_20220609-055949.png
 
Dar es Salaam. Rais mstaafu wa awamu ya nne wa Tanzania, Dk Jakaya Kikwete ameshangazwa na mikutano ya machifu inayofanyika nchini, akisema utawala huo ulishafutwa nchini.

Hayo ameyabainisha Dar es Salaam leo Juni 8, 2022 akiwa mgeni rasmi kwenye kongamano la 13 la Kigoda cha Mwalimu Nyerere cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), ambapo amesema Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere alipinga ukabila na kuwaaunganisha Watanzania kutumia lugha moja.

“Sikuhizi nasikia kuna mikutano ya machifu siajua wanaitoa wapi? Sijajua akina Mangi Mkuu watarudi tena na watemi wale, na babu yangu ni mkuu wa kabila langu lakini akinialika kwenye mikutano hiyo sivutiwi nayo,” amesema Kikwete.

Amesema anachojua yeye suala la uchifu lilishakwisha nchini na kwamba hajui hata wakikutana huwa wanaenda kujadiliana kitu gani, huku akieleza kwamba hatamani kuona watu wanarudi nyuma na kuanza kufikiria kuhusu masuala ya ukabila.

Kikwete ambaye pia ni mkuu wa Chuo hicho Kikuu cha UDSM, amesema ili kufanikiwa kuishi katika misingi aliyoishi Mwalimu Nyerere, kuna umuhimu wa kizazi cha sasa kujifunza historia yake.

Awali akizungumzia kongamano hilo, Makamu Mkuu wa UDSM, Profesa William Anangisye amesema chuoni hapo wataendelea kuchapisha mashapisho mbalimbali kuendeleza falsafa za kiongozi huyo ili wanafunzi wanaokwenda kusoma waelewe.

“Vijana wengi wanakuja kusoma hapa na wanasambaa nchi nzima kwakutambua hilo tutaendelea kutoa elimu kwao kwa kuchapisha matangazo yatakayokuwa yanaelezea kazi aliyofanya baba wa taifa wajifunze kwa sababu tunawategemea kuwa viongozi wa baadae,”amesema Profesa William Anangisye

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa HakiElimu, Dk John Kalage amesema Mwalimu Nyerere mambo mengi aliyokuwa anayazungumza falsafa zake bado zinaendelea kuakisi maisha ya sasa huku akibainisha aliweka mkazo kwenye kuhakikisha vijana wanapata elimu

Source: Mwanachi
 
Ila kama kuna kitu tunajivunia kama Watanzania ni kutokuwa wakabila na wadini.

CHADEMA wanajitahidi sana kuturudisha huko, kamwe tusiwaruhusu aisee.

Tusione dini na kabila kwenye kila kitu.
Ukabila wa CHADEMA uko wapi? Kuna chama mbadala kimesambaa nchi nzima zaidi ya CHADEMA? Hivi unajua CHADEMA ilikua na wabunge wengi kutoka Kanda ya ziwa kuliko kaskazini since 2010?

Acheni kukuza ukabila wakati chama kipo nchi nzima, kilizoa 40% ya kura 2015 na mgombea alikua mkaskazini? Ina maana hizo kura zote ni za wachagga pekee? Tuweni serious
 
Je chifu ...... nanitena nasahau jina hahaaa chifu WANZAGI [emoji23][emoji23]
 
Ukabila wa CHADEMA uko wapi? Kuna chama mbadala kimesambaa nchi nzima zaidi ya CHADEMA? Hivi unajua CHADEMA ilikua na wabunge wengi kutoka Kanda ya ziwa kuliko kaskazini since 2010?

Acheni kukuza ukabila wakati chama kipo nchi nzima, kilizoa 40% ya kura 2015 na mgombea alikua mkaskazini? Ina maana hizo kura zote ni za wachagga pekee? Tuweni serious

Kwanza Kanda ya ZW ipo Kaskazini mwa Tanzania kama ulitaka kumaanisha Mkoa wa Kilimanjaro ulipaswa uweke uwiano wa population pia kusema tu Kanda ya Ziwa chadema ilipata Wabunge wengi klk Kilimanjaro bila ya kuweka idadi ya watu KZ vs Kilimanjaro ni udanganyifu.

Hakuna Mkoa ambao chadema inashinda kwa kura nyingi kuliko Kilimanjaro, na tofauti ni kubwa sana, kiasi kwamba ni sahihi kusema chadema ni Chama cha Mkoa wa Kilimanjaro ni kama ilivyokuwa sahihi kusema cuf ni chama cha Waislamu, kwa maana wapigaji kura na wanachama wa cuf ni Waislamu, ni kama wote.

Hivyo weka uwiano kwa population halafu ndiyo utajua ni wapi Tanzania chadema ina Wabunge wengi na siyo kutaja tu namba!
 
Unajua kuna baadhi ya makabila uchifu uli survive hata kama ulifutwa kwa sababu ulikuwa strong ,lakini baada ya kuuuibua ki siasa hata maeneo ambao ulikuwa very dormant washaamka sasa uko active. Alokuwa chief wa eneo langu alikuwa hata hatajwi sasa juzi nimeona Yuko kwenye tv wakionyesha himaya yake something which wasn’t a case before . Hangaya is terribly dragging us back
 
Nyerere aliwalisha watanzania propaganda sasa wanazikana mila na desturi zao hadharani. Nyerere aliwafunga midomo machifu ili wasimsumbue akitawala kidikteta na kujenga ujamaa wake. Siyo machifu tuu lakini hata viongozi wa dini na wapinzani wa kisiasa aliwanyamazisha.
 
Kwanza Kanda ya ZW ipo Kaskazini mwa Tanzania kama ulitaka kumaanisha Mkoa wa Kilimanjaro ulipaswa uweke uwiano wa population pia kusema tu Kanda ya Ziwa chadema ilipata Wabunge wengi klk Kilimanjaro bila ya kuweka idadi ya watu KZ vs Kilimanjaro ni udanganyifu.

Hakuna Mkoa ambao chadema inashinda kwa kura nyingi kuliko Kilimanjaro, na tofauti ni kubwa sana, kiasi kwamba ni sahihi kusema chadema ni Chama cha Mkoa wa Kilimanjaro ni kama ilivyokuwa sahihi kusema cuf ni chama cha Waislamu, kwa maana wapigaji kura na wanachama wa cuf ni Waislamu, ni kama wote.

Hivyo weka uwiano kwa population halafu ndiyo utajua ni wapi Tanzania chadema ina Wabunge wengi na siyo kutaja tu namba!
Acha uongo, dar es salaam CHADEMA whether Lissu or Lowassa kwa mujibu wa NEC walipata kura nyingi Dar kuliko mkoa wowote ule. Back in 2010 tulikua na wabunge 4 pekee Arusha na Kilimanjaro ila Kanda ya ziwa more over mkoa wa shinyanga pekee tulikua na wabunge 4!! Then Mwanza na Mara tukapata combined 5 MPs so wabunge 9 kutoka mikoa 3 ya Kanda ya ziwa alafu unasema Kilimanjaro what??

Uwiano ni kazi ya NEC wao ndio wanapanga majimbo mfano Dar ilikua chini ya CHADEMA kwa wingi wa madiwani, wabunge na kura za Urais alafu Ina wapiga kura zaidi ya 2 Million, sasa kura za Kilimanjaro zinazidi kura za Dar?? CHADEMA kupata 40% ni kura za Kilimanjaro pekee?

Punguza chuki Chadema imesambaa sana Ina nguvu Songwe/Mbeya kuliko hata Kilimanjaro. Morogoro 2015 tulizoa majimbo 3, Mbeya/Songwe tulizoa 4. Huku kwetu Kigoma CHADEMA Ina nguvu sana na kama sio Zitto kugawa nguvu CCM ilikwishafunikwa na CHADEMA so hizo ajenda za ukabila sijui uchagga watu hawana habari nazo huku.
 
Back
Top Bottom