Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kampein zake aliwaponda sana wawekezaji wa kichina. Kenya kwanza. Ujue Ruto kura nyingi kazipata kwa mama ntilie, boda boda na wafanyabiashara ndogondogo.Wachina wataisoma namba katika nini ?
Mlimpigia kura hadi mtegemee kitu kutoka kwake?!Eti wajuzi wa mambo ya kikanda. Rais mteule wa Kenya ni mtu wa aina gani? Tanzania tutegemee nini kutoka kwake?
Kauli ya kijasiri sana hii. Uhalisia TZ masikini ni wengi sana
Nu mwizi na tapeli mkubwaEti wajuzi wa mambo ya kikanda. Rais mteule wa Kenya ni mtu wa aina gani? Tanzania tutegemee nini kutoka kwake?
Jinsi ulivyoiongelea,natamani sana ingekuwa kubwa kiasi hiko.Tanzania haihitaji kutegemea hisani ya raisi yoyote wa nchi jirani.
Infact Tz ni nchi pekee inayoweza kuiwekea vikwazo vya kiuchumi Congo DR, Rwanda, Burundi, Kenya, Uganda, Comoro, Malawi, Zambia na Sudani ya kusini zote kwa pamoja na isiathirike pakubwa.
Tz ni nchi kubwa. Hakuna nchi nyingine yeyote kusini mwa jangwa la Sahara yenye uwezo huu.
Tz is the United State of Sub Sahara - Africa.
Umejitahidi kuzungumzia personalities zake.Mtegemee jino kwa jino. Uhamasa utaongezeka kwasababu si mtu wa kupenda Amani na hekima. Issues zikitokea usitegemee atakuja kuwapigia magoti au kumaliza Mambo kwa hekima, project nyingi zinazokuja ukanda huu na utalii pia mtegemee fitina. Ni mtu wa maneno matamu lakini nyuma yake ni mtu wa fitina Sana. Kenyatta alijitahidi Sana kuwa na hekima na mkweli. Tunza hii message iko siku utakuja kuelewa nachoandika.
Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Unajua sababu ya Vita ya Uganda 1978/79Umejitahidi kuzungumzia personalities zake.
Lakini yanapokuja mahusiano baina ya nchi na nchi it is very rare matakwa ya mtu binafsi yaka prevail.
Chicken sellerIla jamaa atatawala nchi kwa mbinde sana,maana hiyo njaa waliyonayo Wakenya na yeye alisema atashusha Bei ya unga.
Alafu Baba naye akiamua kumchezesha sijui itakuaje?mwenzake Uhuru alikuwa na akili alijitahidi kumteka Baba na akamaliza ngwe yake salama,sasa ndugu Ruto anaomekana kwanza haelewani na Uhuru,rafiki wa karibu wa Baba na alafu Baba anaonekana hamkubali sana Ruto.
Ruto ana kazi kubwa sana,alafu Malofa wa Kenya Wana Imani naye kubwa sana,yeye anajiita "Hustler"!
Maneno ya siasa usiwekwe kwa moyo utaumia, weka kwa mapafu ukitoa hewa inaenda nayo....ile hustler na wheelbarrow ilikuwa ni mbinu tu hakuna kitu atafanya....Kampein zake aliwaponda sana wawekezaji wa kichina. Kenya kwanza. Ujue Ruto kura nyingi kazipata kwa mama ntilie, boda boda na wafanyabiashara ndogondogo.
Kwahiyo miaka yote Wakenya wanaangaika na mahindi ya Bongo hayo yake alikuwa akiyafanyaje?