#COVID19 Rais Museveni: Mungu ana kazi nyingi, hawezi kuwa tu hapa Uganda akiwaangalia wajinga

#COVID19 Rais Museveni: Mungu ana kazi nyingi, hawezi kuwa tu hapa Uganda akiwaangalia wajinga

Ni kitu gani unachofanya M7 ambayo Mataifa yaliyoanza kuathirika na Corona hayakukifanya yaani Italy, Spain, China, France hata USA wenyewe??

Waziri mkuu wa Italy alitoka mbele ya hadhara akakiri wanamuhitaji Yesu tu ili awaponye na huo ugonjwa
Leo tumegeuka na kudai kuwa scientific measures na porojo za kisiasa zinaweza kuzuia huu ugonjwa

Jaman mimi ninayoona Rais kama alipewa ufunuo tu, huu ugonjwa kwa nchi zetu huku ni Mungu tu ametuhurumia. Kiukweli bila Yesu Kristo mwokozi wa Ulimwengu huu tungezikwa Africa nzima.

Sasa huyo mlevi wa madaraka M7 ni miongoni mwa watu waliochanganyikiwa tu wanadhani kila kitu kwenye maisha yake ni Urais tu wa Uganda.

Yesu Kristo ni mwokozi na katika hili ametuhurumia bara la Africa ni kumshukuru na kuendelea kumuomba atuponye. Magufuri katimiza wajibu wako na wewe timiza wako.

Yesu atamlinda Magufuri katika hili amemtia Mungu na ndio maana wengine linawauma
 
Watanzania wengi wana ugonjwa wa akili,walalamishi,wajinga mara leo wanamshobokea kagame,kesho kenyatta,mtondogoo museven.
 
Capture.PNG


Cha ajabu kuna Watu wamefikiri huu ujumbe ameuelekeza Tanzania

Capture.PNG
 
Well said. Leo huku kwetu Tanzania Idiots wametangaziana Kesho wanakwenda Karmjee kuambukizana tena. Kama namwona Coronavirus anavyofurahia kesho kupata host wapya.
Tumevuka herd instincts, tupo kiwango cha death wish.
 
View attachment 1425361

Cha ajabu kuna Watu wamefikiri huu ujumbe ameuelekeza Tanzania

View attachment 1425369
Mh. Rais yuko sahihi, kwamba Mungu hashughuliki na wajinga, ila hayuko sahihi kwa kusema Mungu yuko busy unless Mungu ana akili yenye upeo sawa na wa mwanadamu.

Sifa pekee za Mungu zinazomtofautisha na kiumbe kingine chochte kile ni hizi hapa:

1. Ni wa milele-hana mwanzo, hana mwisho.

2. Ni muumbaji- hakuna kiumbe kingine chenye uwezo huo.

3. Yupo kila mahali- hakipo kiumbe kingine ambacho kina uwezo wa kuwa kila mahali. Shetani amekuwa akiigiza tabia hiyo lakini yeye kama kiumbe ambaye ni "individual personality", hayupo kila mahali isipokuwa malaika zake tu ndiyo wametapaka kila mahali.

Shetani alikuwa malaika mbinguni na anaendelea kuwa malika hadi leo, ila aliyeasi, na hivyo malaika hana uwezo wa kuwa kila mahali. Tuchukulie kwa mfano siku Malaika Gabriel alivyotumwa na Mungu kwenda kwa Bikra Maria kumweleza kuwa atamzaa mtoto Yesu, wakati Malaika Gabriel akiwa anaongea na Mariam nyumbani kwake, malaika huyu hakuwepo mahali pengine popote duniani au mbinguni, except nyumbani kwa Mariam

4. Anajua yote
5. Anaweza yote

Na kwa post hii sasa, nashauri wale wote ambao wamekuwa wakisema kuwa Mungu hayupo, na kama yupo basi awaue, natoa wito sasa watu hao wajitokeze humu jukwaani, halafu wakiri tena maneno hayo sasa hivi,

Kiranga akiwa ni kiongozi wao. Wakikaa kimya nitashangaa sana. Wajitokeze sasa, huu ndiyo muda ambao wanaweza kuhakiksha vizuri sana tena very precisely!
 
Kwanza kabisa, thibitisha Mungu yupo.

Tusije kujadiliana mengi sana kabla ya hilo.
 
Kwanza kabisa, thibitisha Mungu yupo.

Tusije kujadiliana mengi sana kabla ya hilo.
Reversal of burden of proof! Mimi nikisema kuwa Mungu yupo na nikakupa facts za uthibitisho wangu lakini wewe ukazikataa, unayetakiwa kuthibitisha the opposite (kuthibitisha kutokuwepo Mungu) unakuwa ni wewe (because it's your assertion) kwa ku-supply facts ambazo zita-refute zile za kwangu.

Kwa hiyo unayetakiwa kuthibitisha kuwa Mungu hayupo, ni wewe,..., let's say hata kwa kusema tu kuwa kama yupo basi akutandike na corona, as simple as that.

Hatuwezi kuendelea kuwa na debate hiyo hiyo miaka karibu 20 sasa, mwishowe tuatonekana kuwa kama idiots
 
Back
Top Bottom