Rais Mwinyi msimamishe kazi DC wa mjini unguja , kukaa kimya ni kuidhinisha kauli yake ya kibaguzi

Rais Mwinyi msimamishe kazi DC wa mjini unguja , kukaa kimya ni kuidhinisha kauli yake ya kibaguzi

Stroke

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2012
Posts
37,630
Reaction score
47,434
DC wa Wilaya ya Mjini Unguja amepiga marufuku kwa watu wa jamii ya kimasai kutembea na rungu na sime akiviita kama silaha.


View: https://youtu.be/W-xkQJRDO0c?si=AFIG5omTxVoCeNyZ

Kauli yake si tu inavunja katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, bali inakiuka mikataba mbali mbali ya kimataifa ambayo Tanzania imeiidhinisha inayolinda haki ya raia kushiriki katika mambo ya kitamaduni.

Rejea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 13.

Rejea, Universal declaration of Human Rights, 1948.

Rejea, International Covenant on Economic, Social and Cultural rights.

Sheria zote hizo zinaipa serikali wajibu wa kulinda na kutengeneza mazingira kwa raia wake kuishi wakiwa na uhuru wa kufuata tamaduni zao.

Rungu na sime ni moja wapo ya utambulisho wa tamaduni ya wamasai inayokwenda pamoja na vazi la Rubega.

Kuwapiga marufuku wamasai kufuata tamaduni zao si tu kwenda kinyume na haki za binadamu bali ni kukiuka misingi yote iliyowekwa na jamii za kistaarabu katika kuhakikisha kuwa binadamu anafurahia uwepo wake duniani bila kunyanyapaliwa na mwenzake.

Kauli hii ya DC si tu ya kibaguzi bali inahatarisha ustawi wa Muungano na amani katika nchi.

Ni jambo la kukemewa na kila mwenye nafasi ya kufanya hivyo.

Nakuomba Rais Mwinyi usiache kumchukulia hatua DC huyu au la itatafsiriwa kuwa haya ni maagizo yako na itaingia katika historia ya Taifa kuwa katika utawala wako uliwahi kukandamiza haki za wengine.

Usione aibu kuchukua hatua.
 
Kwani Zanzibar sasa imekuwa Airport!
Umeelewa??

Yaani hao wamasai wanaotetewa kua sijui utamaduni unalindwa na bra bra kibao airports wanaendaga na sime??
Sheria hizo za kimataifa zinawaruhusu wapande na sime??

NB: Zanzibar ni taifa huru.
 
Vipi akienda airport anaweza kuruhusiwa kupanda ndege akiwa na sime??

Tusiwaendekeze sana, ndo yaleyale ya magu na wamachinga.
Wamasai sio wamachinga.

Ni Raia wa Tanzania kama wewe mwenye haki ya kuishi akifuata utamaduni wake.

Zanzibar sio Airport.
 
Upuuzi ni kutoheshimu tamaduni za wengine.

Wamasai sio wahalifu ni raia kama wengine.

Jambo hili limetia doa kwenye CV ya Mwinyi.
sio wahalifu na wamedunda mtu huko zenji??
tena kwa kuwachangia na marungu yao.
 
Wamasai sio wamachinga.

Ni Raia wa Tanzania kama wewe mwenye haki ya kuishi akifuata utamaduni wake.

Zanzibar sio Airport.
Kwani wamachinga sio watanzania??

sheria ya nchi inaruhusu mtu kua na silaha sehemu ya starehe??

Tamaduni ni huko porini kwao sio mjini mzee.
 
sio wahalifu na wamedunda mtu huko zenji??
tena kwa kuwachangia na marungu yao.
Ni kabila limepiga mtu au ni mtu wa kabila la kimasai kapiga mtu.

Tumia akili kama unazo kama huna kaa kimya.
 
Kwani wamachinga sio watanzania??

sheria ya nchi inaruhusu mtu kua na silaha sehemu ya starehe??

Tamaduni ni huko porini kwao sio mjini mzee.
Kuwa na consistence kwenye arguments andika jambo halafu uwe na kumbukumbu ulichoandika hapo awali.
 
DC wa Wilaya ya Mjini Unguja amepiga marufuku kwa watu wa jamii ya kimasai kutembea na rungu na sime akiviita kama silaha.


View: https://youtu.be/W-xkQJRDO0c?si=AFIG5omTxVoCeNyZ

Kauli yake si tu inavunja katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, bali inakiuka mikataba mbali mbali ya kimataifa ambayo Tanzania imeiidhinisha inayolinda haki ya raia kushiriki katika mambo ya kitamaduni.

Rejea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 13.

Rejea, Universal declaration of Human Rights, 1948.

Rejea, International Covenant on Economic, Social and Cultural rights.

Sheria zote hizo zinaipa serikali wajibu wa kulinda na kutengeneza mazingira kwa raia wake kuishi wakiwa na uhuru wa kufuata tamaduni zao.

Rungu na sime ni moja wapo ya utambulisho wa tamaduni ya wamasai inayokwenda pamoja na vazi la Rubega.

Kuwapiga marufuku wamasai kufuata tamaduni zao si tu kwenda kinyume na haki za binadamu bali ni kukiuka misingi yote iliyowekwa na jamii za kistaarabu katika kuhakikisha kuwa binadamu anafurahia uwepo wake duniani bila kunyanyapaliwa na mwenzake.

Kauli hii ya DC si tu ya kibaguzi bali inahatarisha ustawi wa Muungano na amani katika nchi.

Ni jambo la kukemewa na kila mwenye nafasi ya kufanya hivyo.

Nakuomba Rais Mwinyi usiache kumchukulia hatua DC huyu au la itatafsiriwa kuwa haya ni maagizo yako na itaingia katika historia ya Taifa kuwa katika utawala wako uliwahi kukandamiza haki za wengine.

Usione aibu kuchukua hatua.

Ccm oyeeeeeeeee
 
Upuuzi ni kutoheshimu tamaduni za wengine.

Wamasai sio wahalifu ni raia kama wengine.

Jambo hili limetia doa kwenye CV ya Mwinyi.
Mbunge wao akienda bungeni huchukua sime na fimbo?
 
Kesho mtawaambia Wavue RUBEGA kuwa wanatembea uchi na wavae makanzu ya kiarabu kama mnavyovaa ninyi
 
Back
Top Bottom