Rais Mwinyi, tengua Amri haramu ya kwamba Wamasai hawaruhusiwi kutembea na fimbo na Sime Zanzibar. Inahatarisha Muungano!

Rais Mwinyi, tengua Amri haramu ya kwamba Wamasai hawaruhusiwi kutembea na fimbo na Sime Zanzibar. Inahatarisha Muungano!

Serikali ya mapinduzi inapotoshwa kwa hili la wamasai. Kuna chuki kubwa za kidini dhidi ya jamii Za watanganyika
Ila kwa ajili ya siasa watakanusha , wafute tangazo lao kimyakimya dhidi ya wamasai.
hakuna Chuki Ya Kidini Hapo Wametumia Vibaya Uhuru Walopewa Wangekatazwa Kabla Ya Kupiga Polisi Hapo Sawa
 
Bro mmasai mwenyewe ni kivutio cha kitalii. The way alivyovyaa tu tembea nchi za watu ndio utajua nachokuambia. Wazungu wanataka kitu unique mzee sio aje aone sawa na kwao
Sawa ila sime ile siku ikitokea kutoelewan huoni mauaji yanawez kutokea? Zile ni silaha halisi.
 
Eti wapemba na wao waache kuzaliana, cha msingi mmasai bila fimbo na sime yaani hajakamilika watafute njia nzuri ya kutatua swala hili ule ni utamafuni wao!!!
 
Hakuna uhatari wowote kwa muungano wetu adhimu, hakuna Jamii sikivu na yenye umoja na pia isiyotaka Shari kama masai, ukiona umegombana nao basi elewa wewe binafsi ndiye mshari, ufanywe mkutano waitwe wapewe taratibu za kiusalama, case closed!, hutasikia tena tatizo lolote mbeleni. (hayo mavazi na rungu na sime ni Utamaduni wao adhimu).
Kweli kabisa ndugu tunazunguka mitaani huko tunakutana nao wengine ni rafiki zetu mpaka ahatarishe usalama kama jinsi wanavyosema wenyewe wapemba ujue ulianzisha shari!!!
 
Nitajie faida 10 za Huu muungano adimu?

Ikiwezekana taja foida za muungano Kwa upande wa Bara!
Hayo mambo yanafundishwa shuleni kwenye somo la uraia, kama wewe unaona muungano hauna faida wache wenzako wanaojua faida zake, Ndugu zetu wa pwani, wamakonde na wasukuma wanakuwa hadi viongozi huko! sote tungerundikana huku ingekuwaje? wewe wa Ngara huwezi kuona faida kwa vile familia haina miaka mingi hapa nchini!
 
Ukimsikiliza ni chuki tu za kibaguzi. Eti kama wanataka kufanya biashara wafungue maduka na wasibebe sime wala marungu. Hiv nchi hii wamasai wamewakosea nini. Maana porin kwao wamefukuzwa na huku mjin wanakojitafuta hawatakiwi. Mnataka wafanye nini waende wapi.
Wanawalazimisha wawe magaidi sasa
 
Hata Kanuni ya adhabu(Penal Code) ya Tanzania bara(acha zanzibar), nadhani ni sura ya kumi na sita (Cap 16.R.E. 2019) pia hairuhusu.

Na zanzibar kama nchi wana haki ya kuwa na utaratibu wao. La msingi tu, wakae nao wawaelimishe. Wasiweke matumizi makubwa ya nguvu
Na Zanzibar kama nini?

Sent from my ZTE T1002 using JamiiForums mobile app
 
Wawaelimishe kuacha utamaduni wao? We mzima? Kwani utamaduni wao ni sababu ya kukosa elimu? Kuna machizi mengi sana Tanzania.
Kuna mambo lazima yatabaki kama historia tu na kumbukumbu hayawezi kuendelea kwa muda mrefu. Ni suala la mfumo.

Kwani Suala la Tohara kimila kwa wamasai limeishia wapi? Walikuwa wakishakatwa wanatembea kwa makundi na fimbo na huruhusiwi kuwatazama usoni, ukiwatazama unachapwa. Umeshasikia hii tamaduni ikiwa maarufu tena kwenye miji mikubwa? Inajifia.

Kama wanajichanganya na dunia hii inayokwenda kwa kasi watu wanahamia kwenye AI, ni suala la muda tu wataadupt na kuna mambo yatabaki historia kuwa ilikuwa hivi. Kama huko USA tu red indian walivyobaki historia, walikuwa wanatembea na mishale.

Njia sahihi ni kuishi katika maeneo ambayo yanaruhusu mfumo wa tamaduni zao kama nje ya miji mikubwa, vijijini na maporini.
 
Nina laani kwa nguvu zote kitendo cha vurugu za mgambo na watu wa jamii ya kimasai kwakupigana hadharani, Nina laani Masai kushambulia Mgambo, Nina laani kwa nguvu kubwa Mgambo wa Zanzibar kushanbulia watu wa jamii ya kimasai! Jambo hili halikubaliki kwa mjibu wa sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zinazokataza kupigana hadharani au kificho.

Lakini naomba nitofautiane na hatua iliyochukuliwa na serikali ya Zanzibar, Amri kwamba Wamasai hawaruhusiwi kutembea na fimbo na Sime/visu vyao, Ni Kauli Haramu na ya kibaguzi inayohatarisha muungano wa Tangabyika na Zanzibar.

Ifahamike kuwa Fimbo na Sime kwa Jamii za kimasai ni sehemu ya “vazi lao la asili”, ni Sehemu ya utamaduni wao, Ni Identity yao, na hivyo kujaribu kwa aina yoyote kuondoa kimoja wapo katika hivyo vinavyokuwa ndani ya mwili wa Masai ni kutangaza kuwafukuza Wamasi Zanzibar, Hili ni tangazo la kijinga limekurupukwa na mamlaka za Zanzibar!

Kwamiaka yote tangu kabla ya uhuru hadi leo, Jamii za Wamasai wapo Zanzibar na utamaduni wao wa visu/Sime na Fimbo, hakujawahi kuwa hatari kwa raia yoyote, Kwanini iwe leo baada ya Masai kujihami waliposhambuliwa na mgambo wa mji? Serikali ya Rais @dr.hmwinyi itafute jawabu la kumaliza mzozo huu sio kufunika kwakuwafukuza Wamasai, Tatizo liko kwa mamlaka za jiji, Tatizo liko kwa Wakuu wa Mikoa, na mamlaka zingine za jiji.

Unawazuia Wamasai wasibebe fimbo unataka Wabebe Vikapu vya Nazi na vigemeo vya Litembo? Unataka wabebe Usinga? Unataka wabebe karafuu? Noooo nooo tukatae unyanyasaji huu kwa jamii ya kimasai! Ukamilifu wa Masai ni fimbo na sime. Sasa unaka awe na shuka tu kama dera?

Kesho yataibuka Bara Wapemba watashambuliwa, Je serikali iweke amri wapemba wasizaliane kwa Wingi Bara ambao ni sehemu ya utamaduni wao? Nooo Nooo! Tukatae ubaguzi huu.

Mh Rais @dr.hmwinyi ili kunusuri maafa zaidi na kuoondoa hii taswira mbaya ya ubaguzi iliyotengenezwa na mamlaka za mji hapo Unguja, Ninakuomba na kukusihi Mh Rais, tengua hii kauli ya kibaguzi, Haifai kutolewa na kiongozi wa serikali katika ulimwengu wa leo! Madhara yake ni makubwa zaidi mbeleni.

Serikali ijifunze kutatua migogo kwa hekima na busara, Majibu ya hasira ya kiserikali yanaweza kuleta maafa zaidi kuliko kutatua, Nimeisikiliza kauli ikitolewa na yule kiongozi wa mjinibZanzibar (Unguja) ni wazi alitawaliwa na ghadhabu zaidi kuliko hekima ya kiuongozi, Amewahukumu Wamasai bila kujaribu kujua undani na kutafuta jawabu, Badala yake ametafuta jibu ambalo ni la hovyo zaidi!,

Nimesikitika sana kwa kauli hii ya serikali ya Zanzibar katika zama hizi za utandawazi na utandaridhi! Utengamano wa taifa letu ni muhimu kuliko hizi chuki zinazokolezwa na namlaka za nchi!

Na Yericko Nyerere
View attachment 2890368
Acha kutetea ujinga. Unaruhusu vipi watu watembee na silaha katika nchi iliyostaarabika kama Zanzibar? Visu na marungu vya nini Zanzibar? Kama wanataka kutembea na visu na marungu yao warudi huku Bara ambako wamezoeleka na siyo kwenye nchi za watu.
 
Sawa ila sime ile siku ikitokea kutoelewan huoni mauaji yanawez kutokea? Zile ni silaha halisi.
Kwan mmasai ameaza kukaa na sime leo mzee. Hakuna watu poa kama wamasai hawana shida na mtu. Kingine mnatakiwa mzingatie hawa watu walikuwa wanaish porin huko bila shida mkaja kuwalazimisha kuhamia maeneo tofauti so hizo ndio athari zake. Na watajaa mijin balaa maana mmewatoa kwenye uhalisia jiandaein na gharama zake
 
Kwamiaka yote tangu kabla ya uhuru hadi leo, Jamii za Wamasai wapo Zanzibar na utamaduni wao wa visu/Sime na Fimbo,
siyo kweli kuwa wamasai walikuwepo zanzibar kabla ya uhuru , wameanza kufika zenj kwa kuanza kuuza madawa yaho kwenye miaka ya tisini.
 
siyo kweli kuwa wamasai walikuwepo zanzibar kabla ya uhuru , wameanza kufika zenj kwa kuanza kuuza madawa yaho kwenye miaka ya tisini.
So kwa muda wote huo wameua wangapi kwa hizo sime na marungu yao. Chuki ni ushetan kabisa
 
Rais anatakiwa kujua kua matumizi yoyote ya silaha yanakuja baada ya mtu kuonewa au kunyang'anywa haki yake na uvumiiivu ukafika mwisho.Hao masai wametumia nyenzo walizonazo kwasababu mojawapo kati ya hayo mawili kuna ambayo wamefanyiwa.Mimi sitembei na silaha yoyote zaidi ya akili yangu ila siwezi kukubali kua mnyonge kwa yoyote atakayetaka kunionea au kuninyima kile ninachoamini ni haki yangu lazima nijitete.Kwahiyo inawezekana hao masai nao wametumia kanuni hiyo hiyo.chakurekebisha ni jamii nzima iishi kwa haki badala ya kuwanyanyasa alafu muwanyang'anye wanachobeba kwasababu hiyo wala haisaidii endapo uonevu utaendelea, kwasababu mtu uonevu ukizidi silaha inaweza kua kitu chochote.
 
STOP THE GENOCIDE

Hivi watajisikiaje wakiambiwa waache kuvaa makobazi na Kanzu....tena utamaduni wa kuletwa, watajisikiaje?

Wanzanibari wanaweza kuacha kucheza mduara?

Wazanzibari wanaweza kuacha kula rojo?

Wanaweza kuacha supu la pweza?
Nyinyi waporipori msiojuwa historia ya nchi yetu mtatusumbua sana, tamaduni za kuvaa kanzu, makobadhi barakashia, kula ulojo na hata supu ya pweza zinahusisha pia tamaduni za watu wa pwani/waislamu huku kwetu ama 'MDUARA' sawa!
 
Nina laani kwa nguvu zote kitendo cha vurugu za mgambo na watu wa jamii ya kimasai kwakupigana hadharani, Nina laani Masai kushambulia Mgambo, Nina laani kwa nguvu kubwa Mgambo wa Zanzibar kushanbulia watu wa jamii ya kimasai! Jambo hili halikubaliki kwa mjibu wa sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zinazokataza kupigana hadharani au kificho.

Lakini naomba nitofautiane na hatua iliyochukuliwa na serikali ya Zanzibar, Amri kwamba Wamasai hawaruhusiwi kutembea na fimbo na Sime/visu vyao, Ni Kauli Haramu na ya kibaguzi inayohatarisha muungano wa Tangabyika na Zanzibar.

Ifahamike kuwa Fimbo na Sime kwa Jamii za kimasai ni sehemu ya “vazi lao la asili”, ni Sehemu ya utamaduni wao, Ni Identity yao, na hivyo kujaribu kwa aina yoyote kuondoa kimoja wapo katika hivyo vinavyokuwa ndani ya mwili wa Masai ni kutangaza kuwafukuza Wamasi Zanzibar, Hili ni tangazo la kijinga limekurupukwa na mamlaka za Zanzibar!

Kwamiaka yote tangu kabla ya uhuru hadi leo, Jamii za Wamasai wapo Zanzibar na utamaduni wao wa visu/Sime na Fimbo, hakujawahi kuwa hatari kwa raia yoyote, Kwanini iwe leo baada ya Masai kujihami waliposhambuliwa na mgambo wa mji? Serikali ya Rais @dr.hmwinyi itafute jawabu la kumaliza mzozo huu sio kufunika kwakuwafukuza Wamasai, Tatizo liko kwa mamlaka za jiji, Tatizo liko kwa Wakuu wa Mikoa, na mamlaka zingine za jiji.

Unawazuia Wamasai wasibebe fimbo unataka Wabebe Vikapu vya Nazi na vigemeo vya Litembo? Unataka wabebe Usinga? Unataka wabebe karafuu? Noooo nooo tukatae unyanyasaji huu kwa jamii ya kimasai! Ukamilifu wa Masai ni fimbo na sime. Sasa unaka awe na shuka tu kama dera?

Kesho yataibuka Bara Wapemba watashambuliwa, Je serikali iweke amri wapemba wasizaliane kwa Wingi Bara ambao ni sehemu ya utamaduni wao? Nooo Nooo! Tukatae ubaguzi huu.

Mh Rais @dr.hmwinyi ili kunusuri maafa zaidi na kuoondoa hii taswira mbaya ya ubaguzi iliyotengenezwa na mamlaka za mji hapo Unguja, Ninakuomba na kukusihi Mh Rais, tengua hii kauli ya kibaguzi, Haifai kutolewa na kiongozi wa serikali katika ulimwengu wa leo! Madhara yake ni makubwa zaidi mbeleni.

Serikali ijifunze kutatua migogo kwa hekima na busara, Majibu ya hasira ya kiserikali yanaweza kuleta maafa zaidi kuliko kutatua, Nimeisikiliza kauli ikitolewa na yule kiongozi wa mjinibZanzibar (Unguja) ni wazi alitawaliwa na ghadhabu zaidi kuliko hekima ya kiuongozi, Amewahukumu Wamasai bila kujaribu kujua undani na kutafuta jawabu, Badala yake ametafuta jibu ambalo ni la hovyo zaidi!,

Nimesikitika sana kwa kauli hii ya serikali ya Zanzibar katika zama hizi za utandawazi na utandaridhi! Utengamano wa taifa letu ni muhimu kuliko hizi chuki zinazokolezwa na namlaka za nchi!

Na Yericko Nyerere
View attachment 2890368
Acha kukuza mambo yaonekane makubwa.

Jambo la wamasai ni dogo sana na linatatulika.

Unataka ku score points za bure!

Serekali ipo kazini kitambo
 
Ule ni utamaduni wa watu, mbona nyie mnakuja na kanzu zenu huku kwetu na wakati sisi ni wakristo?
Acha kutuchafua, nchi hii hatuna 'mkristo' mjinga wa kushindwa kutambua kuwa, kanzu pia ni vazi la watu wa pwani/ Waislamu huku Tanganyika. unataka kutuambia akina Kikwete, january makamba, Kassim majaliwa na wengine walikuja kutoka zanzibar?
 
Back
Top Bottom