Rais Mwinyi, tengua Amri haramu ya kwamba Wamasai hawaruhusiwi kutembea na fimbo na Sime Zanzibar. Inahatarisha Muungano!

Rais Mwinyi, tengua Amri haramu ya kwamba Wamasai hawaruhusiwi kutembea na fimbo na Sime Zanzibar. Inahatarisha Muungano!

Huku bara wanatimuliwa maeneo yao ya asili, na kule Zenji wanakatazwa kuvaa vitu vyao vya asili.
Huku bara wanasemekana wanaharibu ikolojia ya viumbe hai, na kule Zenji wanasemekana wanahatarisha amani ya wazanzibari.
😅
Kuna ka muunganiko flani ambako kanaonesha kweli huu muungano umeungana Kuwatokomeza wamasai
 
Ule ni utamaduni wa watu, mbona nyie mnakuja na kanzu zenu huku kwetu na wakati sisi ni wakristo?
Kanzu ni vazi takatifu,Yesu pia amevaa.Mapadiri,maaskofu,
Huku bara wanatimuliwa maeneo yao ya asili, na kule Zenji wanakatazwa kuvaa vitu vyao vya asili.
Huku bara wanasemekana wanaharibu ikolojia ya viumbe hai, na kule Zenji wanasemekana wanahatarisha amani ya wazanzinari.
😅
Hawa wamasai sio wabantu,ni wakutoka pembe ya Afrika.Na hao wenye asili ya pembe ya Afrika kama wasomali,waarabu,wa Ethiopia,wameacha mila za kutembea na silaha kama sime,visu,majambia,bakora na fimbo.Mila za kutembea na silaha ni hatarishi na zimepitwa na wakati.
 
Tatizo la wanaharakati wanadakia kila kitu, imradi waonekane na kusisikika
 
Kanzu ni vazi takatifu,Yesu pia amevaa.Mapadiri,maaskofu,

Hawa wamasai sio wabantu,ni wakutoka pembe ya Afrika.Na hao wenye asili ya pembe ya Afrika kama wasomali,waarabu,wa Ethiopia,wameacha mila za kutembea na silaha kama sime,visu,majambia,bakora na fimbo.Mila za kutembea na silaha ni hatarishi na zimepitwa na wakati.
Upo sahihi kwa upande wako chief, ila utamaduni wa mtu ni jambo pana. Kuna watu leo hii wanasema mapenzi ya jinsia mbili yamepitwa na wakati 😅, zuio la ghafla kwa utamaduni wa mtu ni ukosefu wa adabu. Wapewe elimu taratibu watabadilika. Mfano mzuri ni kwenye ukeketaji
 
Wewe Yericho umekosa kazi, hawa wamasai wamekua wasumbufu sana Zanzibar, wamejazana huko bila kazi, wanauza sura beach wakitegemea kupata majimama ya kizungu wapelekwe ulaya. Ukiwakuta beach wanasumbua watalii na vikorokoro vyao, kazi za ulinzi zimewashinda sasa wamekua beach boys. Wanabeba Sime na fimbo wakati znz hakuna simba wala ng'ombe. Hawa bora warudishwe kwao kupunguza kero ZNZ. Na wanao sema Zanzibar wabaguzi basi mbona kuna watanganyika wengi sana wenye shughuli zao na hakuna anaye wabughudhi, wanapiga kazi na wanafata sheria, maisha yanaenda.
Mi ni mchagga na kwa nchi hii tuko kila mahali wengine tuna vibarua wengine hatuna tupo tu kuhangaika angalau kipatikane chochote kitu. Kusema wamasai wanazagaa ndio ubaguz wenyewe mkuu. Watu wengi wamezagaa kila mahali sema wewe unawaona wamasai zaid kwasababu ya mavaz yao nothing more bro. Wazanzibar kwa asili ni wabaguz pasee. Unaongea utafikir wamasai wamefika nchi hii jana. By the way unafikir kwanini wanazagaa. Ulishawah kujiuliza hilo swali? Nani mwenye jukumu la kuhakikisha raia wake wanaajiriwa au kusoma. Mmewatoa kwao kwa nguvu mmewatupa hapo tanga mazingira mapya hawajui chochote. wafugaji hawa life imekuwa ngumu wameamua kuja mjin kujitafuta halafu mwanaume mzima unasimama hapa unabana pua eti wamasai wamezagaa seriously. Halafu huyu mtu utamkuta msikitin anaswali. We unafikir kumtoa mtu ilipo kwa kwa asili ni Jambo jepes sio. Bro kama huna msaada kwa atleast nyamaza usiwaumize kwa kejeli zako.
 
Unataka Wazanzibar nao waanze kutembea wamebeba Majambia kama wa Oman wa kipindi kile?
Kwani wazanzibar ni waoman?? Wale ni wanyamwez..mwarabu alitia mimba tu kule wakatokea hao halfcasts, lkn wale ni watanganyika waliyoingia pale na mwingereza na mwarabu waliwakuta pale
 
Nina laani kwa nguvu zote kitendo cha vurugu za mgambo na watu wa jamii ya kimasai kwakupigana hadharani, Nina laani Masai kushambulia Mgambo, Nina laani kwa nguvu kubwa Mgambo wa Zanzibar kushanbulia watu wa jamii ya kimasai! Jambo hili halikubaliki kwa mjibu wa sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zinazokataza kupigana hadharani au kificho.

Lakini naomba nitofautiane na hatua iliyochukuliwa na serikali ya Zanzibar, Amri kwamba Wamasai hawaruhusiwi kutembea na fimbo na Sime/visu vyao, Ni Kauli Haramu na ya kibaguzi inayohatarisha muungano wa Tangabyika na Zanzibar.

Ifahamike kuwa Fimbo na Sime kwa Jamii za kimasai ni sehemu ya “vazi lao la asili”, ni Sehemu ya utamaduni wao, Ni Identity yao, na hivyo kujaribu kwa aina yoyote kuondoa kimoja wapo katika hivyo vinavyokuwa ndani ya mwili wa Masai ni kutangaza kuwafukuza Wamasi Zanzibar, Hili ni tangazo la kijinga limekurupukwa na mamlaka za Zanzibar!

Kwamiaka yote tangu kabla ya uhuru hadi leo, Jamii za Wamasai wapo Zanzibar na utamaduni wao wa visu/Sime na Fimbo, hakujawahi kuwa hatari kwa raia yoyote, Kwanini iwe leo baada ya Masai kujihami waliposhambuliwa na mgambo wa mji? Serikali ya Rais @dr.hmwinyi itafute jawabu la kumaliza mzozo huu sio kufunika kwakuwafukuza Wamasai, Tatizo liko kwa mamlaka za jiji, Tatizo liko kwa Wakuu wa Mikoa, na mamlaka zingine za jiji.

Unawazuia Wamasai wasibebe fimbo unataka Wabebe Vikapu vya Nazi na vigemeo vya Litembo? Unataka wabebe Usinga? Unataka wabebe karafuu? Noooo nooo tukatae unyanyasaji huu kwa jamii ya kimasai! Ukamilifu wa Masai ni fimbo na sime. Sasa unaka awe na shuka tu kama dera?

Kesho yataibuka Bara Wapemba watashambuliwa, Je serikali iweke amri wapemba wasizaliane kwa Wingi Bara ambao ni sehemu ya utamaduni wao? Nooo Nooo! Tukatae ubaguzi huu.

Mh Rais @dr.hmwinyi ili kunusuri maafa zaidi na kuoondoa hii taswira mbaya ya ubaguzi iliyotengenezwa na mamlaka za mji hapo Unguja, Ninakuomba na kukusihi Mh Rais, tengua hii kauli ya kibaguzi, Haifai kutolewa na kiongozi wa serikali katika ulimwengu wa leo! Madhara yake ni makubwa zaidi mbeleni.

Serikali ijifunze kutatua migogo kwa hekima na busara, Majibu ya hasira ya kiserikali yanaweza kuleta maafa zaidi kuliko kutatua, Nimeisikiliza kauli ikitolewa na yule kiongozi wa mjinibZanzibar (Unguja) ni wazi alitawaliwa na ghadhabu zaidi kuliko hekima ya kiuongozi, Amewahukumu Wamasai bila kujaribu kujua undani na kutafuta jawabu, Badala yake ametafuta jibu ambalo ni la hovyo zaidi!,

Nimesikitika sana kwa kauli hii ya serikali ya Zanzibar katika zama hizi za utandawazi na utandaridhi! Utengamano wa taifa letu ni muhimu kuliko hizi chuki zinazokolezwa na namlaka za nchi!

Na Yericko Nyerere
View attachment 2890368
Wamasai waondokane na ujinga wa miaka mingi na wakubali kubadilika kuendana na hulka za visiwani. Wabadilike wao sio serikali ya SMZ ibadilike kisa kulinda mila za wamasai, kama wao hawawezi kulinda mila na desturi zao hakuna wa kuwalindia hizo mila zao.

Unapokwenda kuishi kwa mtu jifunze zile hulka zake za kila siku ili uwe sehemu ya hapo nyumbani sio kwenda na tabia zako halafu ukikosolewa zinaanza kusikika kelele za muungano. Wapuuzi sana hao wamasai.
 
Hawezi fanya hivyo.

Ana muunnga mkono dada yake kuwatokomeza wamasai.
 
Mmeuza makazi yao ya asili Loliondo na Ngorongoro mkawafukuza , sasa wameamua kuhamia kizimkazi for good WAACHENI vinginevyo iacheni ngorongoro na loliondo yao
 
Wamasai waondokane na ujinga wa miaka mingi na wakubali kubadilika kuendana na hulka za visiwani. Wabadilike wao sio serikali ya SMZ ibadilike kisa kulinda mila za wamasai, kama wao hawawezi kulinda mila na desturi zao hakuna wa kuwalindia hizo mila zao.

Unapokwenda kuishi kwa mtu jifunze zile hulka zake za kila siku ili uwe sehemu ya hapo nyumbani sio kwenda na tabia zako halafu ukikosolewa zinaanza kusikika kelele za muungano. Wapuuzi sana hao wamasai.
Hii nchi hakuna mwenye kwao wewe unaruhusiwa kuish popote kwa utamaduni wako. Nyie ndio wale waafrica mnaoamini ukivaa kizungu umeendelea.
 
Turuhusu watu watembee na sime eti ni utamaduni wao? Upuuzi gani huu?

Wamasai sio watu special kwenye nchi hii, waishi kwa mujibu wa taratibu kama watanzania wengine.

Kila siku wamasai ni tamaduni zao na blah blah kibao, kila mtu anatamaduni zake ila haziko juu ya sheria.
 
Turuhusu watu watembee na sime eti ni utamaduni wao? Upuuzi gani huu?

Wamasai sio watu special kwenye nchi hii, waishi kwa mujibu wa taratibu kama watanzania wengine.

Kila siku wamasai ni tamaduni zao na blah blah kibao, kila mtu anatamaduni zake ila haziko juu ya sheria.
Ulishajiuliza kwanini wahadzabe wanawinda wanyama Pori na serikali haiwakamati Lakin ukiwinda wewe ni miaka 10.
 
Msitutoe nje ya reli,

Serikali ya Mwinyi Zanzibar inapitia Hali Tete.

Tueleze chanzo Cha mtikisiko kwenye baraza la mawaziri.
 
Ulishajiuliza kwanini wahadzabe wanawinda wanyama Pori na serikali haiwakamati Lakin ukiwinda wewe ni miaka 10.
Huu wote ni upumbavu tu, wote hao wanapaswa wachukuliwe hatua kama watanzania wengine.

Hatuwezi kuwa na sheria ambazo zinawabeba group la watu na zinakandamiza wengine.

Wasukuma ambalo ndilo kabila lenye watu wengi ufugaji ni sehemu ya utamaduni wao, ila wananyanyaswa kila kukicha na ng'ombe zao na wanaambiwa wauze mifugo yao Kwasababu hakuna sehemu za malisho. Ila kuna kabila limeachiwa hifadhi wanafuga bila kusumbuliwa na mamlaka.

Ifike mahali huu ujinga ufike kikomo na watanzania wote wawe na haki sawa
 
Ifike hatua huu ujinga tuuweke kando, tuishi wote kwa usawa kwa mujibu wa taratibu za nchi.

Kwa kisingizio cha utamaduni Leo hii kuna watu wanafanya uwindaji haramu, wanaua mamia ya wanyama kadri wanavyojisikia.

Ila kuna mtu anafungwa zaidi ya miaka 10 kwa kukutwa na nyamapori kilo moja.

Kwa kisingizio cha tamaduni watu wanatembea na siraha kali kama sime, ila wengine wakifanya hivyo wanakuwa wamekiuka taratibu za nchi.

Kwa kisingizio cha utamaduni watu wameachiwa hifadhi wafuge mifugo yao, ila wengine wanakosa malisho na mifugo yao inataifishwa na kupigwa mnada.

Kama mnaheshimu tamaduni za watu mbona hampigi kelele wakurya kukatazwa kukeketa? Ila mnapiga kelele wahadzabe wakinyooshewa kidole kwa uwindaji haramu? Ila mnapiga kelele wamasai wakikatazwa kutembea na siraha.
 
Wazanzibar ni wabaguzi sana, nimekuwa na routes kadhaa ila hawa jamaa hawatupendi kabisa watu wa Bara,hata ukiwa Zanzibar hujioni kama upo Tz, wakati huku kwetu wanazurula kama kuku wa kienyeji tu,kuna hatua tutaifikia kila mtu ataenda kwao
 
Ila bana, tuache utani, hizo sime kwa karne hii waachane nazo tu,
Kesho kutwa mm nikiwa natembe na AK47 mtaniruhusu kwa kuwa sipigi nayo mtu?
 
Mbona ukeketaji watu wameelimishwa, wakaacha,na ilikuwa utamaduni wa baadhi ya jamii.

Sasa kwa dunia ya artificial intelligence, hayo mafimbo na marungu, na mavisu yana faida gani? Ni sawa na kukomalia kulala porini Ngorongoro, bila nyumba eti utamaduni

Hizo fimbo ni za kuchungia ngombe, wana ngombe huko zanzibar hao wamasai? Kuna simba zanzibar kwamba watakutana naye wapambane naye kwa kutumia hizo silaha?

Utamaduni wa konyo
Tubadilike
 
Back
Top Bottom