Rais na Mwenyekiti wangu, usisubiri mpaka uharibifu wa Spika Ndugai ukuchafue

Rais na Mwenyekiti wangu, usisubiri mpaka uharibifu wa Spika Ndugai ukuchafue

Tupo na Ndugai mama aache kukopa kopa hovyo pasipokuwa na malengo nchi hii inaweza jiendesha pasipo mikopo siku alitoka madarakani atatiuachia deni la trillion mia maana sio kwa kasi hii miezi tisa ya uongozi wake kakopa si chini ya trillion 10 hadi sasa…
Hivi hayo madeni, mimi kama mwananchi yananidhuruje? Naomba kufahamishwa!! Binafsi nadhani hayana "IMPACT" kwa ustawi wa familia yangu!! hata usingizi sijawahi kukosa eti nawaza deni la taifa
 
Lakini mikopo ni hatari. Serikali inayosisitiza kukopa sio serikali ya kuishabikia hata kidogo. Sera zako za kiuchumi zitavurigika sana kama utategemea uchumi. Itafika mahali sera za kiuchumi utapangiwa ili uwezw kuserve debt.
Mbona unaongea na kujijibu mwenyewe??
 
Miradi kama ya Maji ni huduma ambazo moja kwa moja zinalipiwa kupitia mamlaka za maji za mijini na vijijini. Ni miradi ambayo cash flow yake inajulikana. Kwa hiyo mikopo kama ule wa Arusha wa 520B unajulikana kabisa jinsi mkopo utakavyorudi.
Mikopo kwa ajili ya miradi ya nishati mfano tukikopa kwa ajili ya kuharakisha ujenzi wa bwawa la Julius Nyerere Hydroelectric Power Plant, inaeleweka kabisa jinsi mkopo utakavyorudi kwa sababu ni huduma ya kulipiwa moja kwa moja.
Tukikopa kwa ajili ya kuharakisha ujenzi wa SGR, inajulikana kabisa jinsi flow of cash kwenye hiyo sekta. Hivyo mkopo unajulikana utakavyorudi.
Mikopo ikifanyia hizi shughuli nakuwa sina tatizo nayo! Ila kuniambia mikopo inajenga madarasa halafu tozo nazo pia zinajenga madarasa ni wizi wa mchana kweupe!

Hamnaga kitu kama hicho...Ufisadi utakuwa wa kutisha sana
 
Lakini mikopo ni hatari. Serikali inayosisitiza kukopa sio serikali ya kuishabikia hata kidogo. Sera zako za kiuchumi zitavurigika sana kama utategemea uchumi. Itafika mahali sera za kiuchumi utapangiwa ili uwezw kuserve debt.
Kwani taifa hili lini liliacha kukopa?hadi awamu hii ndio isemwe?kuna awamu iliyokopa zaidi ya awamu ya 5? Huku tuliaminishwa kuwa ni pesa zetu!!alikuwa wapi , na mala ngapi mbungeni ukuaji wa deni la taifa ulijojiwa sana na wapinzani, lakini walikuwa wanapewa tu majibu ya ki MIPASHO?!!hayo ma miradi aliyoyaacha meko unafikiria yataendeleaje wakati yeye alikopa kuyaanza?!!si bora hata huyu ana sema ukweli kuwa ana kopa?na yule aliyekuwa ana kopa hadi kwenye ma bank ya biashara?
 
Imefikia hatua Spika anamkosoa kila lililo jema na kukubali yasiyofaa. Ukosoaji wa namna hii si afya kwa ustawi wa nchi yetu.

Tabia hii ameanza kuonesha katika hiki cha awamu ya sita. Mbona Rais Magufuli alikuwa anafanya yanayofanywa na awamu hii lakini hakuwahi kukosoa?

Ukosoaji wa aina ya Ndugai ni moja wa ufa hatari sana katika ukuaji wa uchumi na maendeleo ya nchi. Ukiachana na nchi chache sana duniani ambazo zina uchumi imara wa kujiendesha zenyewe, nchi nyingi zinategemea mikopo ili kukamilisha ujenzi.

Spika licha ya kujua umuhimu wa mikopo yenye riba nafuu na masharti rahisi lakini bado anaona mikopo hiyo haifai. Bila kutoa njia mbadala wa kuongeza mapato ya ndani anapinga mikopo nafuu. Je, maendeleo yatakujaje?

Yawezekana Spika kaona siku zake za kukalia kiti cha uspika zimeisha au ana nia na lengo tofauti la kumkwamisha Rais na Mwenyekiti wake.

Rais na Mwenyekiti wangu, nguvu na uwezo wa kumtoa Spika unao, fanya sasa kabla uharibifu wa Spika haujaota mizizi itakayokuwa migumu kuing'oa
Unapendekeza afavywaje spika? Huo ni mhimili pamoja na kwamba yuko chini ya chama kinachoongozwa na rais!!! Hawezi kumtoa

Mhimili wa pili umeshatoa dukuduku lao, bado mhimili mahakama nao wana mambo yanayowaudhi kisheria kulazimishwa kuyatenda; kisha funga kazi jeshi ndio litakalo mwacha hoi mkuu wa nchi kwamba akifanyacho kitamgharimu.

Rais hamfanyi chochote spika na jaji mkuu pamoja na mkuwa majeshi.

Aache kujibizana na watu wanaotumia haki yao ya kutoa maoni kama anavyyeye, majibizano kama taarabu kwenye masuala ya msingi hayana afya kwa taifa anatakiwa kukubali udhaifu wake wa kutokuwa na uwezo kutafuta vyanzo vya ndani maana tuna rasilimali za kutosha

Hii kauli ya kusema "tutaendelea kukopa..........", Mungu amsamehe mhajui alitendalo; hakuna Mtanzania anayempenda kwa sasa labda wansiasa wezi
 
Tusitengeneze job seekers, tuwe na majob creators, sasa mfumo wenyewe wa elimu ndio tabu tupu, kinachotakiwa ni kubadilisha mfumo wote wa elimu ili wasomi wapate ujuzi na sio kutegemea elimu kupata kazi, watu wengi ambao ni wasomi je wanaweza pata ajira wote?
Tutengeneze vitu vya maana kama electric plants hio ya Nyerere ili treni ianze kazi viwanda vya magari electric cars tuvianzishe nchini uchumi uende kasi tuachane na biashara ya kuagiza mafuta kwa wingi kupoteza pesa!
 
Ndugai anaweza kuzisukuma kete?....hao Msoga Inc wanasukuma kete balaa, muulize EL na ulipo tupo....Ndugai kaa mkao wa kula hao jamaa watalaam wa fitina, jifunze kwa Mzee Six na uwaziri mkuu....
Bila kujua watu wanaanza kujichekecha...Mara team wazalendo na team ma deal wataanza mpambano...The author is watching from a far...
 
Mh. Ndugai pia anao Uhuru wa maoni na ni vemauhuru huo uheshimiwe.
Tuzoee na tukubaliutamaduni mzuri wa kidemokradia wa kutofautiana hoja bila kugombana.

Hili litawezekana tu kama tukipata Katiba Mpya!

Tuungane kuidai!!
 
Unapendekeza afavywaje spika? Huo ni mhimili pamoja na kwamba yuko chini ya chama kinachoongozwa na rais!!! Hawezi kumtoa

Mhimili wa pili umeshatoa dukuduku lao, bado mhimili mahakama nao wana mambo yanayowaudhi kisheria kulazimishwa kuyatenda; kisha funga kazi jeshi ndio litakalo mwacha hoi mkuu wa nchi kwamba akifanyacho kitamgharimu.

Rais hamfanyi chochote spika na jaji mkuu pamoja na mkuwa majeshi.

Aache kujibizana na watu wanaotumia haki yao ya kutoa maoni kama anavyyeye, majibizano kama taarabu kwenye masuala ya msingi hayana afya kwa taifa anatakiwa kukubali udhaifu wake wa kutokuwa na uwezo kutafuta vyanzo vya ndani maana tuna rasilimali za kutosha

Hii kauli ya kusema "tutaendelea kukopa..........", Mungu amsamehe mhajui alitendalo; hakuna Mtanzania anayempenda kwa sasa labda wansiasa wezi
Soma katiba uone spika anatokaje, mchakato wa kumtoa madarakani Rais ndio mgumu na pengine ni impossible
 
Hata Mzee Samwel Six aliikosoa sana serikali ya Kikwete. Ndugai anatumia haki yake ya kutoa maoni kama ambavyo kina Bulembo wanatumia.
Kwani mzee Ulimwengu alitumia haki yake ya nini akamtisha tisha
 
Tupo na Ndugai mama aache kukopa kopa hovyo pasipokuwa na malengo nchi hii inaweza jiendesha pasipo mikopo siku alitoka madarakani atatiuachia deni la trillion mia maana sio kwa kasi hii miezi tisa ya uongozi wake kakopa si chini ya trillion 10 hadi sasa…
Acha uongo!
 
Hajatoa njia mbadala ya nini kifanyike? Si kuna tozo?
Mkapa alipingwa na CCM wenzake
Kikwete alipingwa na CCM wenzake akiwemo sitta ndio maana sitta hakurudi awamu ya pili
Magufuli alipingwa na CCM wenzake
Mama Samia anapingwa na CCM wenzake
Hakuna suala la kusema sijui kwa kuwa mwanamke au sijui anaonewa
Acheni ujinga
Hahahaha kumekuchaaaaa
 
Tutengeneze vitu vya maana kama electric plants hio ya Nyerere ili treni ianze kazi viwanda vya magari electric cars tuvianzishe nchini uchumi uende kasi tuachane na biashara ya kuagiza mafuta kwa wingi kupoteza pesa!
Miradi yote ya nchi hii niyaupigaji wala usifikiri Kama mwananchi unapendwa sana, hiyo stiglars gorge au standard gauge ingekuwa imekamilika kila siku kughaili tarehe, tumeshapigwa sana
 
Dharau tu naona enzi za jiwe kila mtu aliufyata kuanzia kina Mbowe walikuwa kimya over sudden wote wameota mapembe, ndugai yeye alikuwa anasifia tu kila kitu Hadi vya kijinga
Ukisema Mbowe alikuwa kimya wakati wa Magufuli unamaanisha nini exactly? Manake uhalisia ni kwamba alikuwa anaongea hadharani Magufuli akiwepo hai,kumpinga alipokosea hasa kuhusiana na madudu ya uchaguzi mkuu
 
Imefikia hatua Spika anamkosoa kila lililo jema na kukubali yasiyofaa. Ukosoaji wa namna hii si afya kwa ustawi wa nchi yetu.

Tabia hii ameanza kuonesha katika hiki cha awamu ya sita. Mbona Rais Magufuli alikuwa anafanya yanayofanywa na awamu hii lakini hakuwahi kukosoa?

Ukosoaji wa aina ya Ndugai ni moja wa ufa hatari sana katika ukuaji wa uchumi na maendeleo ya nchi. Ukiachana na nchi chache sana duniani ambazo zina uchumi imara wa kujiendesha zenyewe, nchi nyingi zinategemea mikopo ili kukamilisha ujenzi.

Spika licha ya kujua umuhimu wa mikopo yenye riba nafuu na masharti rahisi lakini bado anaona mikopo hiyo haifai. Bila kutoa njia mbadala wa kuongeza mapato ya ndani anapinga mikopo nafuu. Je, maendeleo yatakujaje?

Yawezekana Spika kaona siku zake za kukalia kiti cha uspika zimeisha au ana nia na lengo tofauti la kumkwamisha Rais na Mwenyekiti wake.

Rais na Mwenyekiti wangu, nguvu na uwezo wa kumtoa Spika unao, fanya sasa kabla uharibifu wa Spika haujaota mizizi itakayokuwa migumu kuing'oa
Manyang'au sasa yanatafutana ndani; Nyerere alisema dhambi ya ubaguzi mkishaifanya haitawaacha salama...mtagundua kumbe nyinyi siyo wamoja, siyo ccm, kuna ccm wenye mikia na waliokatwa mikia
 
Back
Top Bottom