Rais na Mwenyekiti wangu, usisubiri mpaka uharibifu wa Spika Ndugai ukuchafue

Rais na Mwenyekiti wangu, usisubiri mpaka uharibifu wa Spika Ndugai ukuchafue

Imefikia hatua Spika anamkosoa kila lililo jema na kukubali yasiyofaa. Ukosoaji wa namna hii si afya kwa ustawi wa nchi yetu.

Tabia hii ameanza kuonesha katika hiki cha awamu ya sita. Mbona Rais Magufuli alikuwa anafanya yanayofanywa na awamu hii lakini hakuwahi kukosoa?

Ukosoaji wa aina ya Ndugai ni moja wa ufa hatari sana katika ukuaji wa uchumi na maendeleo ya nchi. Ukiachana na nchi chache sana duniani ambazo zina uchumi imara wa kujiendesha zenyewe, nchi nyingi zinategemea mikopo ili kukamilisha ujenzi.

Spika licha ya kujua umuhimu wa mikopo yenye riba nafuu na masharti rahisi lakini bado anaona mikopo hiyo haifai. Bila kutoa njia mbadala wa kuongeza mapato ya ndani anapinga mikopo nafuu. Je, maendeleo yatakujaje?

Yawezekana Spika kaona siku zake za kukalia kiti cha uspika zimeisha au ana nia na lengo tofauti la kumkwamisha Rais na Mwenyekiti wake.

Rais na Mwenyekiti wangu, nguvu na uwezo wa kumtoa Spika unao, fanya sasa kabla uharibifu wa Spika haujaota mizizi itakayokuwa migumu kuing'oa
Wakikosoa akina mbowe mnawaweka ndani.Haya Gombaneni wenyewe huko.[emoji38]
 
Miradi yote ya nchi hii niyaupigaji wala usifikiri Kama mwananchi unapendwa sana, hiyo stiglars gorge au standard gauge ingekuwa imekamilika kila siku kughaili tarehe, tumeshapigwa sana
Mi sina shida tukipigwa ila vitu vya kuonekana vionekane basi, sio mnapigwa umeme wa shida, maji ya shida!
 
JPM alikuta deni la taifa ni 43t miaka yake mi5 kaacha deni 66t sasa Samia na miezi yake8 deni ni 70 vipi akimaliza miaka minne ?bila shaka itakuwa ni 100t ,hapa ndipo nchi itapigwa mnada na umuhimu wa katiba mpya unazidi kuongezeka
Umesema kwa miezi 8 ameshaongeza deni la tr 10, kitu ambacho si kweli.
 
Mkuu ni kweli awamu ya 5 walikuwa wanatuambia lakini walikuwa hawafanyi walichokuwa wanatuambia. Sasa hivi awamu ya 6 maneno na matendo ni sawa sawa kabisa. Hakuna mtu aliyekosa kama Magu, kwa miaka 5 kakopa more than 17trl!!!! Fanya ratio uone kila mwaka alikopa Tsh. Ngapi!!! Huyu mama yetu kakopa 1.3tln imekuwa nogwa kiasi hiki?
Wendawazimu waendelee kulala kuzimu.
Waliokuwa wakitupeleka vizuri ni awamu ya 5. Ni ngumu kumeza ukweli lakini walikuwa wakituambia ukweli. Uchumi wa kujidanganya kwa mikopo ya hovyo na kutumia hovyo ni kujidanganya ya hali ya juu sana.
 
Huyu ananuka!!! Na ni Malaya wa siasa full stop! [emoji2957]
Mh. Ndugai pia anao Uhuru wa maoni na ni vemauhuru huo uheshimiwe.
Tuzoee na tukubaliutamaduni mzuri wa kidemokradia wa kutofautiana hoja bila kugombana.

Hili litawezekana tu kama tukipata Katiba Mpya!

Tuungane kuidai!!
 
Mkuu ni kweli awamu ya 5 walikuwa wanatuambia lakini walikuwa hawafanyi walichokuwa wanatuambia. Sasa hivi awamu ya 6 maneno na matendo ni sawa sawa kabisa. Hakuna mtu aliyekosa kama Magu, kwa miaka 5 kakopa more than 17trl!!!! Fanya ratio uone kila mwaka alikopa Tsh. Ngapi!!! Huyu mama yetu kakopa 1.3tln imekuwa nogwa kiasi hiki?
Wendawazimu waendelee kulala kuzimu.
Unajua msichanganye mkopo na deni. 17T zinazozungumzwa ni deni. Maanake mkopo umeiva na riba zake na bado kuna additional ya riba za mikopo ya miaka mingine before 2015. Nimeona nikupe hiyo elimu kwanza.
Na hapa hatuna sababu ya kushindanisha hawa viongozi wetu wawili.
Hapa tuitendee haki nchi yetu na vizazi vijavyo. Tuache kuwa pure presidential keepers.
 
Hata Mzee Samwel Six aliikosoa sana serikali ya Kikwete. Ndugai anatumia haki yake ya kutoa maoni kama ambavyo kina Bulembo wanatumia.kwa
Hivi samwel sita yuko wapi jamani!! Mana simsikii kabisa. Au yuko analima bangi huko kwao tabora Mana tabora kwa kulima bangi na tumbaku hawajambo. Tujuzane jamani alipo samwel sitta
 
Imefikia hatua Spika anamkosoa kila lililo jema na kukubali yasiyofaa. Ukosoaji wa namna hii si afya kwa ustawi wa nchi yetu.

Tabia hii ameanza kuonesha katika hiki cha awamu ya sita. Mbona Rais Magufuli alikuwa anafanya yanayofanywa na awamu hii lakini hakuwahi kukosoa?

Ukosoaji wa aina ya Ndugai ni moja wa ufa hatari sana katika ukuaji wa uchumi na maendeleo ya nchi. Ukiachana na nchi chache sana duniani ambazo zina uchumi imara wa kujiendesha zenyewe, nchi nyingi zinategemea mikopo ili kukamilisha ujenzi.

Spika licha ya kujua umuhimu wa mikopo yenye riba nafuu na masharti rahisi lakini bado anaona mikopo hiyo haifai. Bila kutoa njia mbadala wa kuongeza mapato ya ndani anapinga mikopo nafuu. Je, maendeleo yatakujaje?

Yawezekana Spika kaona siku zake za kukalia kiti cha uspika zimeisha au ana nia na lengo tofauti la kumkwamisha Rais na Mwenyekiti wake.

Rais na Mwenyekiti wangu, nguvu na uwezo wa kumtoa Spika unao, fanya sasa kabla uharibifu wa Spika haujaota mizizi itakayokuwa migumu kuing'oa
Huyo Ndugai afukuzwe uanachama, hajui anachofanya. Yeye ni tatizo.
 
Hivi samwel sita yuko wapi jamani!! Mana simsikii kabisa. Au yuko analima bangi huko kwao tabora Mana tabora kwa kulima bangi na tumbaku hawajambo. Tujuzane jamani alipo samwel sitta
Duh! Huna habari kwamba alisha RIP?
 
Hii elimu wala haina maana kwangu. Hoja ya kuwashindanisha imetoka kwa huyu rafiki yako pamoja na wewe. Mlitudanganya kwamba wakati wa awamu yenu hamkukopa, ushahidi upo wa massive loans mlizochukua. Sasa kilinge kinawaka moto baada ya kukosa ulaji mnapiga kelele. Wacheni mama afanye kazi kama ambavyo wakati wenu mliachwa mkafanya kazi mpaka mkakimaliza wenyewe.
Unajua msichanganye mkopo na deni. 17T zinazozungumzwa ni deni. Maanake mkopo umeiva na riba zake na bado kuna additional ya riba za mikopo ya miaka mingine before 2015. Nimeona nikupe hiyo elimu kwanza.
Na hapa hatuna sababu ya kushindanisha hawa viongozi wetu wawili.
Hapa tuitendee haki nchi yetu na vizazi vijavyo. Tuache kuwa pure presidential keepers.
 
Waliokuwa wakitupeleka vizuri ni awamu ya 5. Ni ngumu kumeza ukweli lakini walikuwa wakituambia ukweli. Uchumi wa kujidanganya kwa mikopo ya hovyo na kutumia hovyo ni kujidanganya ya hali ya juu sana.
Walikuwa wanatuambia ukweli upi? Wakati wao ndio wameongeza deni la nchi hii kwa kiasi kikubwa sana huku wakitudanganya kuwa tunajenga miradi kwa fedha zetu wenyewe. Rudi ukasome tena mwenendo wa deni la Taifa kwa awamu zote.
 
Rais na Mwenyekiti wangu, nguvu na uwezo wa kumtoa Spika unao, fanya sasa kabla uharibifu wa Spika haujaota mizizi itakayokuwa migumu kuing'oa
Supika hawezi kuondolewa kizembe hivyo kwa kupishana kauli na mwenyekiti wa chama. Huo ndio uhuru wenyewe wa kutoa maoni

Jifunzeni kukubali mitazamo ya watu wengine
 
Lakini tunavyopotea kuendeleza kukopa kwa ajili ya sekta ya elimu, tunapotea na tunatengeneza mzigo ambao utatutesa sisi ambao bado vijana, utawatesa watoto wetu na vizazi vijavyo. Sekta ya elimu bado ni sekta inayohudumiwa kwa fedha nyingi za walipakodi kupitia elimu bure. Na hiyo ni recurrent expenditure tu maanake haitegemewi kuzalisha flow of cash back to treasury.
Na bado kuna mkopo mwingine ulioitwa mkopo wa "Higher Education Improvement for Economic Transformation"; Terminology ya Benki ya Dunia.
Imeelekezwa kwenye elimu ya juu ambayo nayo bado tunaihudumia kupitia fedha za walipa kodi kupitia mikopo ya elimu ya juu, ruzuku na stahiki mbali mbali za Wafanyakazi wa kada mbali mbali katika ngazi hiyo ya elimu
Bado tena kuna mkopo maarufu kama SEQUIP(Secondary Education Quality Improvement Programme) kwa ajili ya kuboreshea elimu ya sekondari.
Mikopo yote hiyo imetolewa na benki ya dunia kimtego kabisa. Wakijua kabisa kwamba ni pesa ambayo hairudi na hivyo kuisababishia serikali mzigo mkubwa wa madeni. Hivyo serikali kurudi kuwakamua walipa kodi wale wale ili iweze kurejesha mkopo. Na wakati wa kulipa hairudi kwa mipango yake ikiwa imetulia. Inarudi ikiwa na pressure ya kufikia kuitwa International defaulter au isiyokopesheka.
Haya yote yalisainiwa kipindi cha Jiwe, sasa hivi ni utekelezaji tu.
 
Mikopo ikifanyia hizi shughuli nakuwa sina tatizo nayo! Ila kuniambia mikopo inajenga madarasa halafu tozo nazo pia zinajenga madarasa ni wizi wa mchana kweupe!

Hamnaga kitu kama hicho...Ufisadi utakuwa wa kutisha sana
Unaujua ukubwa wa nchi hii na mahitaji yake katika Elimu?
 
Back
Top Bottom