Countrywide
JF-Expert Member
- Mar 2, 2015
- 20,694
- 32,527
Ningependa kujua huo mwaka ambao motisha ilishuka, na napenda kujua pia lini motisha ilipanda. Karibu tujadiliMkulima ukishalima uza panapokupa faida ili mwakani ulime tena,kama kuna mtu anahitaji aje kununulia shambani kwa bei ya soko.
Kuna mwaka hapa wakulima motisha ya kulima kibiashara ilishuka, Vijana wengi sana waliamia kwenye bodaboda maana boda inalipa kuliko shamba.
Serikali ifunge mipaka iwapo kuna vita au njaa ya level 1.
Hii hesabu ya wapi? Yaani uuze mahindi uliyonayo nje ya nchi, alafu ikitokea upungufu uende tena kununua nje ya nchi?We hata njaa ya level one wasifunge maana tunaweza nunua nchi nyingine hata Afrika kusini nako huwa sana mahindi mengi
Mkuu, Kabla ya kutaja mwaka ww ni mdau wa moja kwa moja wa kilimo? Maana kama sio utahitaji data kutoka kwenye maghala za ununuzi ambazo sitaweza kukupatia hapa. Ila kwa kukupa picha rudi kile kipindi kulikuwa na tetesi za tatizo ka korosho maghalani.Ningependa kujua huo mwaka ambao motisha ilishuka, na napenda kujua pia lini motisha ilipanda. Karibu tujadili
Mimi sio mdau tu bali ni mwekezaji mkubwa sana kwenye kilimo, nakijua vizuri sana tena kwa mazao mbalimbali. Nimekuuliza hapo uniambie lini motisha ilishuka na lini ilipandaMkuu, Kabla ya kutaja mwaka ww ni mdau wa moja kwa moja wa kilimo? Maana kama sio utahitaji data kutoka kwenye maghala za ununuzi ambazo sitaweza kukupatia hapa.
Mimi nimeamka asubuhi kila siku na baridi Kali kulima,ww uko barbershop ukijipodoa,nikivuna uje kunipangia pa kuuza!? Kha! Yaani wanaume wa Dar buana🚮Wandugu
kuna lugha za kujirudiarudia kutoka kwa hawa viongozi wakisisitiza kwamba mkulima Lima jiwekee cha kwako na familia yako chakula kingine nenda kauze nje mipaka ya nchi mipaka imefunguliwa.
Najiuliza ina maana wananchi wengine kama Dar es salaam wanaotegemea vyakula hivyo havitawafikia kwa sababu mkulima ataangalia wapi atapata bei kubwa ya mazao na ukweli ni kwamba chakula kingi kinachukuliwa na wakenya kwa kigezo cha bei nzuri na watu Dar es salaam wanakosa chakula ndio maana kuna mfumuko wa bei mkubwa.
Kuna kitu kinaitwa food security kwa Tanzania hakuna.
Mwekezaji mkubwa? Vizuri ww huitaji data za maghala maana lazima una maghala. Ulipeleka mazao yako nchi zipi na zipi ule mwaka ambao malori yetu yalisimama sana pale mpakani mwa kenya na Tz? Na vp serikali ilipoamua kutafuta na kuuza masoko ya mahindi moja kwa moja kama nchi kutoka kwenye maghala ya taifa kupitia control namba ilikuafect vp? Mwaka 2018 waziri mkuu alipoelekeza kuuza mahindi kwa kutoa taarifa serikalini kwanza ulifuata maelekezo? Kuna urasimu wowote ulikutana nao?Mimi sio mdau tu bali ni mwekezaji mkubwa sana kwenye kilimo, nakijua vizuri sana tena kwa mazao mbalimbali. Nimekuuliza hapo uniambie lini motisha ilishuka na lini ilipanda
Kuna uongo mwingi sana kwenye huu Uzi wako. Wakulima lini waliacha kilimo?Serikali inanunua chakula cha kutosha sana chini ya NMC. Na kila mkoa unaozalisha mahindi kuna maghala makubwa tu ya chakula. Waacheni wakulima wadogo nao wanufaike.
Food security unayosemea wewe ndio aliyoifanya magufuli na mahindi yaliyo kwenye maghala mfano ghala la Songea liliopo Ruhuwiko mahindi mengi yalioza na yakatupwa kwa sababu mtaani mahindi yalikuwepo sababu mipaka mingi ilifungwa, hiyo hali ilipelekea wakulima wengi kupata midororo ya kiuchumi miongoni mwao na kuacha kilimo.
Mipaka ikifunguliwa hivi itaongeza uzalishaji sababu ya uhakika wa soko na wakulima wengi wataludi kwenye kilimo.
Cha kufanya hapa ni kuongeza thamani mazao kama mahindi kwa kuyachakata kabisa na kuuza unga na product nyingine nje ya nchi na sio kuuza mahindi kama yalivyo. Kwahiyo ufunguaji wa mipaka watanzania tuchukulie kama fursa ambayo italeta chachu ya maendeleo kwa kuongeza uzalishaji zaidi na kufungua viwanda vya uongezaji thamani mazao ya kilimo.
Mkuu nipe data za bei kwa waliouza ghalani kuanzia msimu wa 2020 mpk leo.Kuna uongo mwingi sana kwenye huu Uzi wako. Wakulima lini waliacha kilimo?
Alafu pia bei huwa haihusiani na mipaka kufungwa wala kufunguliwa. Njoo hapa tujadili, maana naona mnaanza kulisha watu uongo. Mipaka inaweza kufunguliwa na bei ikawa chini pia.
Issue ya kwanza ilikua kuhusu motisha kushuka na kupanda, nikakuuliza ni mwaka gan motisha ulishuka na kupanda Ila hujanipa jibu, anyway...Mwekezaji mkubwa? Vizuri ww huitaji data za maghala maana lazima una maghala. Ulipeleka mazao yako nchi zipi na zipi ule mwaka ambao malori yetu yalisimama sana pale mpakani mwa kenya na Tz? Na vp serikali ilipoamua kutafuta na kuuza masoko ya mahindi moja kwa moja kama nchi kutoka kwenye maghala ya taifa kupitia control namba ilikuafect vp?
Mkuu, Naomba urudie kusoma kuna maswali nimekuuliza. Ishu ya mwaka ipo wazi sana kuna jambo nataka nijue kutoka kwako kwanza ili nielewe kama kweli tutajadili au tutafanya siasa.Issue ya kwanza ilikua kuhusu motisha kushuka na kupanda, nikakuuliza ni mwaka gan motisha ulishuka na kupanda Ila hujanipa jibu, anyway...
Turudi hii issue ya pili, umesema ule mwaka malori yalikwama Kenya, ni mwaka gani? Maana hata mwaka huu pia malori yalikwama. Uwe specific kutaja mwaka ili twende sawa
Nimekuuliza lini wakulima waliacha kulima, hujanijibu.Mkuu nipe data za bei kwa waliouza ghalani kuanzia msimu wa 2020 mpk leo.
Halafu ukimaliza utanieleza kati ya miaka hiyo mwaka gani umekua na mazao machache na sababu zipi zilipelekea mazao yawe machache.
Umeniuliza nilipeleka mazao yangu nchi ipi na ipi ule mwaka ambao malori yalikwama. Mimi ndio nikauliza mwaka gani? Kwa maana hata mwaka huu malori yalikwama pia.Mkuu, Naomba urudie kusoma kuna maswali nimekuuliza. Ishu ya mwaka ipo wazi sana kuna jambo nataka nijue kutoka kwako kwanza ili nielewe kama kweli tutajadili au tutafanya siasa.
Hawa watu hawaelewi kitu, mipaka kufunguliwa haihusiani na bei kuwa juuAise viongozi wako sahihi kabisa Kama hujawahi kulima huwezi elewa acheni wakulima wajiuzie jamani Tena wauze,
Ilo swali ulilouliza ungejibu yale niliyouliza jibu lake lilikuwepo pale tatzo hujausoma uzi Mkuu ila umeanza kusoma coment na kujibu huu uzi mzima unazungumzia mazao ya chakula hasa mahindi.Nimekuuliza lini wakulima waliacha kulima, hujanijibu.
Kwanza inapaswa kuniambia hapa unazungumzia mazao ya chakula au biashara. Kama ni ya chakula ni wakulima wengi hawauzii ghalani, kama ni ya biashara wala hakuna suala la mipaka maana yanalimwa ili yauzwe nje ya nchi. Turudi kweye hili la 2020
2020 mipaka haikufungwa ilikuwa wazi, Ila Bei ilikuwa chini. Na ndio sababu ya kukueleza mipaka kuwa wazi haihusiani na bei.
Aalafu unapozungumziaa uzalishaji kushuka naomba unieleze ni uzalishaji wa zao lipi?
Swali si hilo tu nimekuuliza, naona unakazana na hilo la mwaka ambalo lipo wazi sana. Anyways naona tutafanya siasa.Umeniuliza nilipeleka mazao yangu nchi ipi na ipi ule mwaka ambao malori yalikwama. Mimi ndio nikauliza mwaka gani? Kwa maana hata mwaka huu malori yalikwama pia.
Be specific twende sawa hapa, unazungumzia mwaka gani?
Embu elezea hapa? Mkuu Una hakika ww ni mfanya biashara na muwekezaji mkubwa wa mazao? Mbona hili ni suala jepesi sana kwa wafanyabiashara maana pia huwa kunatabia ya kuzuia mzigo iwe michache sokoni ili bei ipande baada ya demand kuongezeka.Hawa watu hawaelewi kitu, mipaka kufunguliwa haihusiani na bei kuwa juu
Ukitaja mwaka shida ipo wapi? Nimekueleza wakulima wengi hawauzii ghalani, huu mbona Ni ukweli ulio wazi?Ilo swali ulilouliza ungejibu yale niliyouliza jibu lake lilikuwepo pale tatzo hujausoma uzi Mkuu ila umeanza kusoma coment na kujibu huu uzi mzima unazungumzia mazao ya chakula hasa mahindi.
Alafu unainua NMC je wakulima hawauzi mahindi kule je unaijua TFC nayo hapo ukijua utagundua nlichoongea kwenye comment ya mwanzo uliyo quote. Ila kama ulikua mkoani Ruvuma au unafatilia habari na biashara ya mahindi Sana utajua mwaka gani uzalishaji ulipungua na mwakan gani ulipanda au ukitaka data kamili ya swali nililokuuliz tembelea NMC unaweza uliza au ukitaka data naweza leta na hiyo yote ni athari ya siasa tu.
Swali la mwaka ndio linadetermine jibu, ndio maana nimekuuleza hata mwaka huu malori yalikwama. Sasa hapo hujaelewa kipi?Swali si hilo tu nimekuuliza, naona unakazana na hilo la mwaka ambalo lipo wazi sana. Anyways naona tutafanya siasa.