Rais Samia aalikwa na Baba Matakatifu Francis Mjini Vatican kwa mazungumzo rasmi ya siku mbili

Rais Samia aalikwa na Baba Matakatifu Francis Mjini Vatican kwa mazungumzo rasmi ya siku mbili

Kufuatia mualiko wa kiongozi mkuu wa kanisa katoliki duniani na nchi ya Vatican Papa Francis, Rais Samia Hassan atafanya ziara ya kitaifa tarehe 11 hadi 12 Februari, 2024.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba amesema lengo la ziara hii ni kukuza ushirikiano kati ya Tanzania na Vatican.

Tanzania na Vatican tangu mwaka wa 1960 zimekuwa zikishirikiana katika masuala ya elimu, afya, masuala ya amani na kiroho.

"Kanisa katoliki linakadiriwa kumiliki zaidi ya shule za chekechea 240, shule za msingi 147, shule za sekondari 245, vyuo vya ufundi 110, na vyuo vikuu 5," inaeleza taarifa iliyotolewa na wizara huku takribani taasisi za afya 473 zikiendeshwa na kanisa katoliki.

Tofauti za udini hazijawafanya viongozi hawa kushindwa kukaa pamoja na kujadili maslahi ya wananchi na uendelezaji wa ushirikiano kati ya nchi hizi mbili.

=====

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Baba Mtakatifu Francis amemualika Rais Samia Suluhu Hassan Mjini Vatican kwa mazungumzo rasmi ya siku mbili baina ya viongozi hao.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba amewaambia waandishi wa habari mkoani Dar es Salaam leo kuwa mazungumzo hayo yatafanyika Februari 11 na 12 Vatican nchini Italia.

Makamba amesema kufuatia mwaliko huo, Rais Samia ameamua kuambatana na waumini wa kawaida wa Katoliki ambao pia wataonana na Papa Francis katika ziara hiyo ya kihistoria.

"Hii ni heshima kubwa kwa nchi yetu na Rais wetu, kwani mazungumzo hayo na Baba Mtakatifu ni ya heshima kubwa na watu wachache sana ndio watapata fursa ya kuhudhuria mazungumzo hayo," amesema Makamba

TEC watangulize ule Waraka....!!
 
Ila Hawa Vatican Wana nguvu Gani? Papa anaweza hata kum summon Biden chap tu
Ni kwasababu ndan ya kila serikali kuna watu waumini ya kikristo ambao ni ngumu kwenda kinyume nae kwa viapo vya imani.

Na hao watu wanafahamika na jeshi la siri la usalama wa vatican(wanaitwa Jesuit), hvyo raisi yeyote akiwa mwisho basi anaweza poteza vitu vingi ndan ya nchi yake mwenyewe na akafanya vibaya na watu wake mwenyewe .

NB: Hapa siongelei dini bali intelijensia ya JESUIT
 
Eti mazungumzo ya siku mbili 😆😆.

Biden kakaa kwa mazungumzo na papa kwa takriban dakika 75, hakuna kiongozi aliyewahi kuufikia muda huo.

Huyu wa kwetu siku mbili watakuwa wanajadili nini!
Ingekuwa kule kwingine mgesema anatoa mrejesho kwa wajomba zake.
 
Amealikwa au amejialika ,tuwekane sawa hapa , kama vipi leta ushahidi wa mwaliko , why mnachukulia watz wapumbavu sana nchi hii, kumbuka

Kikwete alijialika
Mkapa alijialika n.k ,so kipi cha msingi sana Papa amwalike ,Tueshimiane mtoa mada hauijui Dunia
Ukweli ni kwamba ameomba kwenda kuonana na papa! Acheni kulemba lemba.
 
Kufuatia mualiko wa kiongozi mkuu wa kanisa katoliki duniani na nchi ya Vatican Papa Francis, Rais Samia Hassan atafanya ziara ya kitaifa tarehe 11 hadi 12 Februari, 2024.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba amesema lengo la ziara hii ni kukuza ushirikiano kati ya Tanzania na Vatican.

Tanzania na Vatican tangu mwaka wa 1960 zimekuwa zikishirikiana katika masuala ya elimu, afya, masuala ya amani na kiroho.

"Kanisa katoliki linakadiriwa kumiliki zaidi ya shule za chekechea 240, shule za msingi 147, shule za sekondari 245, vyuo vya ufundi 110, na vyuo vikuu 5," inaeleza taarifa iliyotolewa na wizara huku takribani taasisi za afya 473 zikiendeshwa na kanisa katoliki.

Tofauti za udini hazijawafanya viongozi hawa kushindwa kukaa pamoja na kujadili maslahi ya wananchi na uendelezaji wa ushirikiano kati ya nchi hizi mbili.

=====

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Baba Mtakatifu Francis amemualika Rais Samia Suluhu Hassan Mjini Vatican kwa mazungumzo rasmi ya siku mbili baina ya viongozi hao.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba amewaambia waandishi wa habari mkoani Dar es Salaam leo kuwa mazungumzo hayo yatafanyika Februari 11 na 12 Vatican nchini Italia.

Makamba amesema kufuatia mwaliko huo, Rais Samia ameamua kuambatana na waumini wa kawaida wa Katoliki ambao pia wataonana na Papa Francis katika ziara hiyo ya kihistoria.

"Hii ni heshima kubwa kwa nchi yetu na Rais wetu, kwani mazungumzo hayo na Baba Mtakatifu ni ya heshima kubwa na watu wachache sana ndio watapata fursa ya kuhudhuria mazungumzo hayo," amesema Makamba
Pope huwa halaiki viongozi wa nchi bali viongozi huimba kutembelea/kutembelewa na pope. Hiyo taarifa ya makamba ina uchawa ndani yake
 
ieleweke white pope anayatekeleza anayoyapata kutoka kwa black pope, ambapo naye anayatekeleza anayoyapokea kutoka kwa grey pope. Shetani yuko kazini akitenda kwa siri na hila nyingi sana.


YESU NI BWANA NA MWOKOZI
 
Baada ya SATAN pale juu, tuliona zinafatia 13 EVIL SATANIC BLOODLINE FAMILIES. Shetani anazitumia kurule the World, sio binadam wa kawaida japo tunawaona ni watu. Ni malaika wa shetani na uzao wao waliozaa na binadam, wengine wakatokea kuwa reptile species na tunaishi nao humu humu.

Baada ya hizi familia Kuna NGAZI ya MAPAPA inafatia ambao wako WATATU
1. GRAY POPE
2. BLACK POPE
3. WHITE POPE
Karibu tuone wasifu wao angalau Kwa ufupi[emoji116]
 
kule kujiita tu "Baba Mtakatifu" ni kufuru. Baba Mtakatifu ni mmoja tu na ndiye Mungu. Yoh 17:11

Yesu ni Mwokozi
 
The Vatican is the richest country in the world with trillions of $ of investments thru big shares and Bonds in US, banks, churches, schools, hospitals, industries etc etc, and most dangerous silent small country that rules almost every country in the world, the Roman empire lost only its military powers, but in terms of political influence, geography, properties, investments, richness, is top of all countries in the world, Vatican is Roman empire today..!!

Safari njema..!!
 
Back
Top Bottom