Pre GE2025 Rais Samia aamsha shangwe baada ya kuwalipia tiketi abiria wote waliosafiri kwa treni ya kisasa

Pre GE2025 Rais Samia aamsha shangwe baada ya kuwalipia tiketi abiria wote waliosafiri kwa treni ya kisasa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Juha kalulu umerudi na vihoja vyako vya kusifu na kuabudu 🤣🤣🤣
Hapo majinga yanayojidai yanajua propaganda ndiyo yanamshauri huo ujinga kutafuta popularity... Anaacha kusaidiwa wagonjwa,yatima,wazee nk. anataftia kiki wasafiri alafu juha anakuja resi kumrusha humu!! Huku watu wanajitambua hawapongezi uzwazwa'
 
Tujitahidi kusoma magazeti. Hasa magazeti makubwa
Screenshot_20240613_092659_Chrome.jpg
 
Ndugu zangu Watanzania,

Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi cha Watanzania Daktari Samia Suluhu Hasssan ameibua shangwe na kuteka hisia za watanzania wengi sana, baada ya Rais wetu mpendwa kwa moyo wake wa upendo, huruma, ukarimu na unyenyekevu.

kuamua kwa dhati ya Moyo wake na kwa pesa zake binafsi zinazotokana na jasho lake. Kuamua kuwalipia tiketi abiria wote waliokuwa wamefanya safari kwa mara ya kwanza na treni ya kisasa kabisa kutoka Dar kwenda Morogoro na Morogoro kwenda Dar.

Rais wetu anafanya hivyo kuwapa hamasa Watanzania kutumia usafiri huo wa kisasa, mzuri,salama,nafuu,wa haraka na wenye utulivu wa hali ya juu sana .ambao watu watakaa vizuri pasipo kuchoka wala uchovu wala bughudha wala hofu huku wakifurahia mazingira mazurii ya njiani na hali ya hewa nzuri na safi sana kwa afya ya Mwanadamu..

Rais wetu Anaendelea kugusa na kuteka mioyo ya Watanzania ,kwa matendo yake ya huruma na upendo kwa watu wote . Niambie ni kiasi gani furaha waliyo nayo abiria hao ambao wamepewa ofa hiyo buree kabisa na mama yao mpendwa mwenye moyo wa huruma kwa watu wake. Wameokoa kiasi gani cha pesa ndugu zangu Watanzania?

Hii ndio raha ya kuongozwa na Mama, raha ya kuwa na kiongozi mwenye upendo na ukarimu kwa watu,raha ya kuwa na kiongozi anayewajali na kuwathamini watu wake. Najisikia fahari sana na mwenye bahati sana kuongozwa na Rais Samia .ni historia kwagu nitakayoisimulia miaka ya baadaye panapo majaliwa ya Mwenyezi Mungu.

Imefika wakati watanzania raha zimewazidi mpaka wakifika mahali na wakiona mabango ya Rais wetu njiani yenye picha yake ,wanasimama kwa bashasha na tabasamu na kujipiga picha mbele ya mabango hayo huku wakifurahia na kumuombea Maisha marefu yeye heri na baraka tele kwake..

Kazi iendelee, mama ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Ni uungwana uloje kiongoz mkubwa wa taifa kuwashika wananchi wake mkono.
Nawish na mm ningelikuwa miongoni mwa hao abiria ila bahati ya mwenzio usiilalie mlango wazi
Pongezi kwa maono ya washauri wa rais
 
Ni upumbavu wa masikini huo
Huwezi kukuta Sunak anawatolea tickets watu wanaoenda mwezini kisa uchaguzi ni mwezi wa 7

Haya unayakuta afrika tu ipo siku mtatolewa na mahari
 
Hospital dawa hakuna, na viongozi wake wanalawiti mabinti mwambie
 
Ni upumbavu wa masikini huo
Huwezi kukuta Sunak anawatolea tickets watu wanaoenda mwezini kisa uchaguzi ni mwezi wa 7

Haya unayakuta afrika tu ipo siku mtatolewa na mahari
Naona umeumia sana na kuona wivu sana.unatamani na wewe ungekuwa miongoni mwao.
 
Hospital dawa hakuna, na viongozi wake wanalawiti mabinti mwambie
Dawa za hospitalini zitanunulia kwa kodi zetu kama ambavyo zimeendelea kununuliwa wakati wote .hata hivyo Rais wetu kutumia pesa zake ambazo ana uhuru nazo na pia hazuiliwi kutoa na kusaidia watu.pia kuna watu hapo walikuwa wanakwenda hospitali na kupitia kulipiwa nauli maana yake wataweza kupata hela ya kununua dawa kwa pesa walioweza kuokoa
 
Juha kalulu umerudi na vihoja vyako vya kusifu na kuabudu 🤣🤣🤣
Hapo majinga yanayojidai yanajua propaganda ndiyo yanamshauri huo ujinga kutafuta popularity... Anaacha kusaidiwa wagonjwa,yatima,wazee nk. anataftia kiki wasafiri alafu juha anakuja resi kumrusha humu!! Huku watu wanajitambua hawapongezi uzwazwa'
Wewe ndio hujitambui,lakini wanaojitambua na wasio vipofu wa akili na macho wanashuhudia mapinduzi makubwa sana katika Secta ya Afya.ambapo Secta ya Afya kwa miaka mitatu tu imeweza kupokea zaidi ya Trilioni sita.
 
Wewe ndio hujitambui,lakini wanaojitambua na wasio vipofu wa akili na macho wanashuhudia mapinduzi makubwa sana katika Secta ya Afya.ambapo Secta ya Afya kwa miaka mitatu tu imeweza kupokea zaidi ya Trilioni sita.
Sidhani kama unamuda wa kumsifu Muumba wako wewe nikusifu mavi ongozi mchana usiku!!
Sema ukikuwa utaacha labda maana machawa yakizeeka huwa ...
 
Sidhani kama unamuda wa kumsifu Muumba wako wewe nikusifu mavi ongozi mchana usiku!!
Kama una hasira basi pasuka tu ndugu yangu. Maana utakufa tu kwa sababu matendo mema na kazi njema za Rais Samia zinaendelea kwa kasi.
 
Mambo mengine ni kusoma na kupita kimya tu. Watu wameamua kuwa kunguni ili waishi, ajira hakuna.
 
Mambo mengine ni kusoma na kupita kimya tu. Watu wameamua kuwa kunguni ili waishi, ajira hakuna.
Naishi kwa jasho langu kwa kazi ya mikono yangu kwa kuchapa kazi ya kilimo kwa nguvu na bidii pamoja na maarifa.
 
Back
Top Bottom