Rais Samia achana na siasa za watemi na machifu, ni hatari, hazikusaidii na hazilisaidii taifa

Ulipotaja Magufuli ndo ulipoharibu, kwa dunia ya wasitaarabu na yenye usitawi haiwezi kulilia kuongozwa na sadist Kama JPM. Taja mwingine plz, Kama Taifa tulikosea sana awamu ya tano, na Mungu akaamua kutuponya, usiturejeshe huko.
Mmnadhani watanzania tulio wengi hatujajua haswa tunataka NN ktk maisha yetu haya,hatujui tulikotoka ,tulipo natunakokwenda,hatujui kudefine maendeleo,nahasa NN kifanyike ili tuwe namaisha Bora,ndio manaa kila kiongozi kwetu nimbaya,nawao washatujua kwahyo hufanya vile wanavyoona inafaa,inasikitisha snaa
 
Nimewahi kuishi Moshi miaka mingi sana. Nawafahamu kwa kiasi fulani wachaga. Wakiwa mikoa mengine tofauti na kwao wachaga ni kama wamoja hivi lakini ukiwa kwao Kilimanjaro aisee hawa jamaa kila moja na kwao utasikia tu mimi mmarangu, mkibosho, mrombo, mmachame, mnarumu, muoldmoshi, muuru, msiha, mkiruwa n.k. Na kwa kiasi kikubwa hayo maeneo yote yana machifu/mangi/viongozi wao japo siku hizi hawana nguvu sana nje ya maeneo yao toka serikali ilipofuta hayo mambo ya machifu.

Maswali ya msingi hapa
1. Je hao mamangi/viongozi wa kila eneo walikaa lini na wapi wakakubaliana kuwa Mareale ndio mkuu wao?
2. Kuna kipindi si muda mrefu sana huyo Mareale alikuwa na kesi mahakamani na ndugu yake ya kugombea uchifu, je ilishaiisha na maamuzi
yalikuwaje
3. Na kama machifu wote wa Moshi walikubaliana kumualika mgeni rasmi mbona kwenye tangazo anatajwa tu Marealle kwa nini isiwe "chifu
mkuu Marealle kwa pamoja na machifu wenzake fulani na fulani wa Kilimnjaro wanamwalika mgeni rasmi ........... kwenye tamasha?
4. Shughuli nyingi za machifu huwa zinaambatana na shughuli za kishirikina na uganga wa jadi kwa kiasi fulani hili kila mtu anajua, je kwa mtu
ambaye ana imani na hofu ya Mungu kushiriki shughuli za hawa watu si kuchanganya mambo kweli?

Ni mtizamo tu.
 
Siyo kweli kusema makabila yamepitwa na wakati kwenye karne ya 21. Kabila ya wayahudi (Israelites) bado lipo na lina maendeleo makubwa sana leo. Nyerere ndiye alidhoofisha utawala wa machifu ili awalaghai watu na kuwalisha sumu ya Ujamaa. Halafu kila siku watu wanapiga kelele kwamba hiyo unayoita tawala rasmi ya kisheria na kiserikali inakiuka haki za binadamu na kuwakandamiza watu. Hiyo tawala rasmi ya kisheria na kiserikali ina majeshi ya vamizi Zanzibar. Miaka 60 ya tawala rasmi za kisheria na kiserikali unazozisema wamefanya nini?
 
Huyu alisema Zanzibar hakuna makabila ni unzanzibar tu..
Huku mbona anatafuta credit kwa kutumia makabila.
Ni lini Zenji watampa uchief?
 
Rais Samia, Pamoja na kuupalilia uchief bado kizazi cha sasa hakiwezi kuusikiliza na kuuheshimu huo uchief. kizazi cha sasa hakiwezi tena kusikiliza utabiri wa kichief, hakiwezi kwenda kulima kwa cheif ama kupeleka chakula, kizazi hiki hakiamlishwi tena na uchief. kwa kifupi hiki ni kizazi cha sayansi ya teknolojia.
 
Hapo kwenye kutafuta MAGUFULI mpya, umechemsha. Siasa za Magufuli za kumiliki bunge,na mahakama na kuwa Mungu mtu hazifai.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Huyu mama namwonea huruma wanavyompeleka puta, huu upuuzi si aukatae, kama vipi awaachie uraisi wao,

Wanamfanya aonekane kituko kisa uraisi 2025
Kama anajua kuvaa nguo safi badala ya chafu manake anajielewa kwahiyo hii kusema anapelekeshwa ni porojo tupu
 
Nigeria ilikuwa na nafasi ya kuwa ni taifa kubwa na lenye kuogopeka kuliko lilivyo sasa sababu mojawapo inayokwamisha ni siasa za machifu.

Wameendekeza sana siasa za bei rahisi za upambe na mambo ya jadi na zimewagawa vilivyo. Labda Rais Samia anayo mahesabu ya mbali ya kuzitumia siasa hizi pasipo kuharibu umoja wetu wa kitaifa uliojengwa kwa gharama ya kuvumiliana na kupendana.
 
Mtafute mungu wako na siyo huyo mungu wa wazungu
Mimi ninavyoelewa Mungu ni moja na ndiye aliyeumba vyote vilivyomo katika dunia hii, mimi siamini kama kuna Mungu wa wazungu na Mungu wa waafrika, kwa kifupi siamini ktk uwepo wa hao miungu unaosema.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…