peno hasegawa
JF-Expert Member
- Feb 24, 2016
- 14,255
- 23,949
Justification ya kipuuzi sana. Sijui kuwa kuna watu hapa JF wanaweza kuandika vitu vya kipuuzi namna hii.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Justification ya kipuuzi sana. Sijui kuwa kuna watu hapa JF wanaweza kuandika vitu vya kipuuzi namna hii.
Sidhani kama ni ukabila ila ni mbinu za kujijenga kisiasa japo linaleta picha mbaya.Divide and rule; katika karne ya ishirini tupande basi la ukabila !
Huo ndio upofu wa kusoma mambo nusu nusus; Cheif marealle anayezungumzwa kwenye document la zamani hilo alifariki tangu mwaka mwaka 2007 akiwa na umri takriban miaka 92. Huyu anayeitwa Chief Marealle leo ni mmoja wa wajukuu zake tu, wala hajulikani zaidi ya hapo uchagani tu. Uksioma hayo madocument hayo ya zamani utakutana pia na jinsi walivyokuwa wanamhusudu Nyerere, hata alipokwenda kutembelea Uingereza, alipokelewa na malkia mwenyewe badala ya waziri mkuu!
Chief Hangaya anataka percent yake akistaafu akale kwa utulivu huko visiwani pembaDah kumbe bibi anatuma mzigo kwenye koloni lake? Hapo sawa
Achana na hizo mambo za wazungu. Sisi huku tuendelee kuchawiana, kutoana mapepo, na kufanya sherehe, kula, kunywa, kucheza ngoma na mambo kama hayo.Huyu mama anafikiri anajijenga kiasiasa kwa kukumbatia mambo ya kishirikina yaliyopitwa na wakati, zaidi ya kufanya uganga na matambiko machifu wana jambo gani la maana kwenye jamii ya watu waliostaarabika katika karne hii ya 21..........hivi leo tunaweza kuwatumia machifu kubuni chombo cha kwenda kufanya utafiti anga za juu, au watachekecha manyanga na matunguli yao na kurusha ungo kwenda sayari ya Mars........bwahahahaaa...........chifu hangaya bhana..
Amekwama Hangaya..Atatuletea balaa. Huko tulishapita wala hatutaki kusikia machifu. Yuko desperate kutafuta political base. Nadhani 'reactionaries' wapinga maendeleo wanamshauri kwenye machifu. Uchifu unaambatana na desturi za imani za kishirikina umwinyi na kuleta ukabila na kunyanyasa wanawake. Hatutaki hiyo.
Hangaya hana uwezo kuongoza nchi hii. Ajitahidi tu ku maintain status quo hadi 2025 tuweze tafuta magufuli mpya.
Tumeona tayari yuko pro business people tofauti na desturi nchi hii tunataka kiongozi pro people... Maendeleo kwa umma sio watu wachache kuhodhi uchumi wa nchi kushirikiana na ubeberu wa kimataifa.
Toka lini tumeanza kuwapa nafasi wapiga ramli????Tangu Rais Samia ashike madaraka amekuwa busy sana kuzing'ang'ania na kuzipigia debe siasa za kuwaenzi na kuuenzi utamaduni wa machifu na watemi hapa Tanzania. Hapa nitaweka kweli kadhaa kuhusu ubaya wa siasa hizo kwa nchi yetu na vizazi vijavyo.
1. Utamaduni wa watemi na machifu ni utamaduni wa kikabila na kikoo kwa 100%. Hawa hawafanani, hawakubaliani na hawakai chungu kimoja. Unalenga kuwagawa watanzania kuliko kuwaunganisha.
2. Utamaduni wa watemi na machifu umezungukwa na mfumo dume kwa karibu 100%. Kadri unavyopaliliwa ndivyo ambavyo mfumo dume unakuzwa na kuota mizizi kwenye jamii.
3. Kwa sehemu kubwa sana tamaduni za watemi na machifu zimejikita kwenye ubagani, matambiko, ushirikina na mambo ya kale. Sioni mantiki yoyote kwa serikali kuukumbatia sasa kwenye karne ya 21.
4. Kwa sehemu kubwa utamaduni wa tawala za machifu unakinzana na mifumo ya tawala rasmi za kiserikali na kisheria. Huwa ni vitu visivyoweza kwenda sambamba. Kuimarika kwa tawala rasmi za kiserikali automatically kuliua tawala za machifu na watemi, kuzifufua upya hizo tawala za machifu sasa ni kuhatarisha uwepo wa tawala rasmi za kisheria na kiserikali.
5. Utamaduni wa tawala za watemi na machifu kwa sehemu kubwa umedhoofika, kufifia, kuparaganyika au ulishakufa kwa jamii nyingi sana hapa Tanzania. Wengi watakaoibuka sasa na kuitwa watemi au machifu huenda watakuwa waganga wa kienyeji, wazee wa kikoo, matapeli (wazee wa fursa), wajumbe wa CCM wa nyumba kumi kumi (wazee wazee). Kiuhalisia utakuta sio watu halisi wa kuwakilisha watemi na machifu wa zama zile. Kuwakumbatia watu wa namna hiyo ni kupoteza muda na rasimali.
Aliwakataa hawa waganga na mambo yao ya ujanja ujanja. Nani anawapa nafasi? Kwa manufaa ya nani? Mimi kama mtanzania, hawa machifu na mambo yao hayanisaidiiJulius Kambarage Nyerere aliona mbali sana