Rais Samia akutana na kufanya mazungumzo mfanyabiashara Alhaj Aliko Dangote

Rais Samia akutana na kufanya mazungumzo mfanyabiashara Alhaj Aliko Dangote

Kuna uwezekano mkubwa, Ikulu ya Chamwino haitaendelea kutumika.
Chamwino kuna makafara mchanganyiko. Yapo ya John Malecela yapo na ya Mwendazake. Hakukaliki wala hakukaliki.

Mwacheni Mama Samia aendelee kula upepo wa bahari
 
... we don't care Ikulu iko wapi; tunachohitaji ni UPENDO, FURAHA, HAKI, na AMANI vitamalaki nchini; that's priority #1. Mengine yanafuata.
Unajua gharama ya kuwa na nyumba ndogo? Gharama ya kuendesha serikali yenye shughuli dar na dom?
 
Huyu Dangote wakati anapigania kupata gas ya Mtwara, ni Magufuli aliyempigania mpaka kuagiza ajengewe bomba lake mpaka kiwandani,

alipoona vile vile wanamzingua kuhusu makaa ya mawe alimruhusu mpaka awe na eneo lake mwenyewe achimbe,

leo mnamsema kwamba alikuwa anamfanyie mizengwe,?!

kweli kama umemchoka mbwa mpe jina baya.

nyie watu man roho mbaya sana.
Mkuu, upo kazini (kulinda legacy na upotoshaji) au hujui? Bomba lake mwenyewe la gesi ni plan ya msoga boy iliyokuwepo. Jiwe akaja kubadilisha hayo kwa kuamua eneo lililoelekezwa bomba liwe ni eneo la viwanda na serikali yenyewe ndiyo izalishe nishati na kumuuzia Dangote kama mteja tu (wa nishati) sambamba na wateja wengine watakaowekeza eneo hilo. Hii ingeongeza gharama kwasababu angepaswa kununua nishati kutoka kwa "middle man". Ndicho hicho alicholalamika kutotekelezwa walichokubaliana. Sasa unaposema jiwe ndiye aliyepush ajengewe bomba lake ni upotoshaji wa hali ya juu.
 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassani amekutana na kufanya mazungumzo na Mfanyabiashara maarufu kutokea Nigeria Alhaji Aliko Dangote

Mazungumzo hayo muhimu yalifanyika leo Mei 24, 2021 Ikulu Jijini Dar es salaam

Alhaji Dangote ni mfanyabiashara mkubwa duniani aliyewekeza nchini Tanzania kwenye sekta mbalimbali ikiwemo Kiwanda cha kuzalisha Saruji Mkoani Mtwara

Alhaji Dangote amemshukuru sana Rais Samia kws kuboresha mazingira ya Uwekezaji nchini na ameahidi kuwa ataendelea kuwekeza Tanzania kwenye maeneo tofauti ikiwamo ujenzi wa Kiwanda cha Mbolea

Rais Samia aliahidi kuwa Serikali yake itaendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji nchini kwa faida ya pande zote na alwaagiza Mawaziri husika kushughulikia changamoto zinazoikabili Kampuni ya Dangote

Taarifa zaidi kutolewa na Mamlaka husika

Kazi Iendelee
Asante kwa taarifa hii, huu ni muendelezo wa mwanzo mzuri wa Mama Samia, to restore confidence kwa investors ni hatua muhimu sana kwa investiment climate yetu.

Hongera sana rais Mama Samia for healing the nation.
Pasco
 
Unajua gharama ya kuwa na nyumba ndogo? Gharama ya kuendesha serikali yenye shughuli dar na dom?
Ila nyumba tatu haikuwa shida, si ndivyo? Maana mtangulizi wake alikuwa na nyumba ndogo 2 na hivyo kufanya awe na nyumba 3; Magogoni, Dodoma na Chalton.
 
Naomba media zote leo Wahariri mtoe habari ya Dangote vizuri. Mtangazeni mama kwa mazuri na makubwa anafanya kwa nchi kwa muda mfupi mno mwanga umerudi kwa speed ya radi. Mungu mlinde Rais wetu, #The Madam President#HerExcellency

MONDAY MAY 24 2021​

Dar es Salaam, Tanzania

Aliko Dangote impressed by dramatic change in Tanzania's business environment​

Dar-es-Salaam, Tanzania



Video courtesy of Global TV online

Dangote pic

President Samia meets Nigerian businessman Aliko Dangote at State House, Dar es Salaam.


Aliko Dangote, Africa's richest man, has praised Tanzania's President Samia Suluhu Hassan, saying that the business environment in the country had changed "dramatically" under her leadership.
Read more : Source : Dangote impressed by dramatic change in Tanzania's business environment
 
Msigwa naye anatuchanganya ivi Waziri wa viwanda na biashara ni nani au kuna mabadiliko
 
Sema Dangote naye ni mtu asiweza kabisa figisu. Biashara zake nyingi ustawi wake unategemea sana kulelewa na serikali. Hata Nigeria iko hivyo.

Ingawa ndio kazi ya serikali kulea sekta binafsi lakini ukipata mtawala roho mbaya kama Magu mambo yanayumba sana.
Nchi yoyote makini, uhusiano wa sekta binfasi na serikali uko kwenye taratibu sahihi za kufanyabiashara, siyo kudekezwa ambako ndo naona sasa kunatafutwa kwa kisingizio cha ajira.
 
Huyu Dangote wakati anapigania kupata gas ya Mtwara, ni Magufuli aliyempigania mpaka kuagiza ajengewe bomba lake mpaka kiwandani,

alipoona vile vile wanamzingua kuhusu makaa ya mawe alimruhusu mpaka awe na eneo lake mwenyewe achimbe,

leo mnamsema kwamba alikuwa anamfanyie mizengwe,?!

kweli kama umemchoka mbwa mpe jina baya.

nyie watu man roho mbaya sana.
Pls if possible Tupe SABABU ZA MSINGI,KWA NINI ALISITISHA UZALISHAJI HAPA TANZANIA.
ILI NDUGUZO TUFAHAMU.
 
... huyu Mama PR iko juu sana kuliko mtangulizi! Chama kingekuwa makini, kama ilikuwa ni lazima wawili hawa washike madaraka ya juu, basi mtangulizi aliitakiwa awe msaidizi wa Mama toka mwanzo kabisa.
Hakuna cha PR! Ameitoa wapi wakati hajawahi interact na dunia? Hapa sisi tunajua kinachotafutwa. Marais wa kiafrika wanazuzuliwa na vitu vya kishenzi tu! Hata kuambiwa wewe ni zaidi ya wote, inampa kichwa kikubwa. Iliwahi sikika JK alipewa suti na ikatosha kutoa upendeleo. Sasa endeleeni kuamini huyu anajua mambo kumbe wao wameshajua udhaifu wake. Ndo kazi ya ofisi za ubalozi zilizoko hapa nchini, kujua udhaifu wa viongozi wetu.

Baadaye ataalikwa uchina na kupigiwa Tanzania Nakupenda kwa moyo wote kama tunavyowaona wengine, akirudi anasimulia kama spika kwamba alifanyiwa presentation nzuri saaana!
 
Pls if possible Tupe SABABU ZA MSINGI,KWA NINI ALISITISHA UZALISHAJI HAPA TANZANIA.
ILI NDUGUZO TUFAHAMU.
Huyo ni kutoka Nigeria boss! Lini ulisikia muwekezaji mwaminifu toka Nigeria? Tangu rais hadi mwananchi ni utapeli mtindo mmoja.
Kwani Dangote ni wa kwanza kuwa na kiwanda nchini? Twiga Cement unawasikia wakijikomba Ikulu? Tanga cement unawasikia? Huyu ana lake na huenda ni mambo ya kipuuzi yanatafutwa hapo!
 
Hujui chochote kuhusu hill Dogo. Katika mambo ambayo JPM alikuwa smart lilikuwa ni jinsi alivyo deal na Dangote. Utanielewa kesho!


13 Nov 2020

Billionare Dangote Talks About His Relationship With Tanzania's Magufuli​



Aliko Dangote speaks about investment situation in Tanzania.

Aliko Dangote points on flaws of investment policies and hope for better days in the future as for now Tanzania has scared alot of investors to go in there or from doing more.

Also for Tanzania sometimes it is about communication hurdles too on top of unclear stable investment policies.
Source : The Bridge Tal
 
Huyo ndio Mh SSh anaweka mambo sawa,mambo ya ubabe ubabe ya kuharibu diplomasia awamu hii hakuna.
 
Huyu Dangote wakati anapigania kupata gas ya Mtwara, ni Magufuli aliyempigania mpaka kuagiza ajengewe bomba lake mpaka kiwandani,

alipoona vile vile wanamzingua kuhusu makaa ya mawe alimruhusu mpaka awe na eneo lake mwenyewe achimbe,

leo mnamsema kwamba alikuwa anamfanyie mizengwe,?!

kweli kama umemchoka mbwa mpe jina baya.

nyie watu man roho mbaya sana.
Magufuli alikuwa mwongo na msahaulifu
 
Back
Top Bottom