Rais Samia ameahidi kujenga msikiti wa kisasa wenye hadhi ya Rais katika Kitongoji cha Migude, Kijiji cha Milo, Kata ya Vigwaza Wilaya ya Chalinze Mkoani Pwani.
Hayo yamesemwa na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Sheikh Walid Alhad Omary wakati alipotembelea msikiti huo ambao hali yake haidhirishi katika kufanya ibada jambo ambalo lilikuwa ni kilio cha muda mrefu kwa wakazi wa Kijiji cha Milo.
Mara baada ya kuuona msikiti huo Sheikh Alhad Walid Omary amewatoa wasiwasi wakazi wa eneo hilo kwamba msikiti huo utajengwa na Rais Dkt Samia ili wakazi hao waweze kufanya ibada zao katika mazingira yaliyo bora.
Kwa upande wake Sheikh wa Kata ya Vigwaza, Shaban Haroun Mshauri amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan huku wakimuombea kila lenye heri yeye pamoja na wasaidizi wake.
Chanzo cha ahadi ya kujengwa kwa msikiti huo katika kijiji cha Migude kilitokana na video iliyosambaa mitandaoni kupitia kwa Mwandishi wa habari nchini Mbarouk Khan.
Sio kwa ubaya ila nauliza tu,kwanini ndg zetu waislamu hawawezi kujichanga wakajenga nyumba za ibada nzuri kama wakristo wanavyojenga makanisa?
Tena kwa maeneo kama ya Dar na pwani matajiri kibao waislamu lakini utakuta wanavizia mtu mmoja ndio ajenge msikiti
Sio kwa ubaya ila nauliza tu,kwanini ndg zetu waislamu hawawezi kujichanga wakajenga nyumba za ibada nzuri kama wakristo wanavyojenga makanisa?
Tena kwa maeneo kama ya Dar na pwani matajiri kibao waislamu lakini utakuta wanavizia mtu mmoja ndio ajenge msikiti
Kiongozi wa nchi ni vizuri akawekeza nguvu zake nyingi kwenye ujenzi wa vitu vyenye tija kwa wananchi wote. Mfano vituo vya utafiti, uvumbuzi, nk.
Hizi mambo za kuwekeza hela kwenye ujenzi wa misikiti, makanisa, kuwahonga hela manabii feki ili wakuombee, kuwahonga hela wachungaji na maaskofu ili kuwafunga midomo, nk. Haina tija yoyote ile kwenye karne hii ya 21.
Rais Samia ameahidi kujenga msikiti wa kisasa wenye hadhi ya Rais katika Kitongoji cha Migude, Kijiji cha Milo, Kata ya Vigwaza Wilaya ya Chalinze Mkoani Pwani.
Hayo yamesemwa na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Sheikh Walid Alhad Omary wakati alipotembelea msikiti huo ambao hali yake haidhirishi katika kufanya ibada jambo ambalo lilikuwa ni kilio cha muda mrefu kwa wakazi wa Kijiji cha Milo.
Mara baada ya kuuona msikiti huo Sheikh Alhad Walid Omary amewatoa wasiwasi wakazi wa eneo hilo kwamba msikiti huo utajengwa na Rais Dkt Samia ili wakazi hao waweze kufanya ibada zao katika mazingira yaliyo bora.
Kwa upande wake Sheikh wa Kata ya Vigwaza, Shaban Haroun Mshauri amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan huku wakimuombea kila lenye heri yeye pamoja na wasaidizi wake.
Chanzo cha ahadi ya kujengwa kwa msikiti huo katika kijiji cha Migude kilitokana na video iliyosambaa mitandaoni kupitia kwa Mwandishi wa habari nchini Mbarouk Khan.
Sio kwa ubaya ila nauliza tu,kwanini ndg zetu waislamu hawawezi kujichanga wakajenga nyumba za ibada nzuri kama wakristo wanavyojenga makanisa?
Tena kwa maeneo kama ya Dar na pwani matajiri kibao waislamu lakini utakuta wanavizia mtu mmoja ndio ajenge msikiti
Kwani hata hasipojenga, unaweza kumfanya hasipate urais kwa njia yeyote ile ?
Hizi commenents zenu zimejaa chuki tu ya kwanini waislam wanajengewa msikiti. Samia kwa upande wamarais ndio ambae amechangia kujenga makanisa kuliko Rais yeyote yule, hata ukifanya uwiano kati ya makanisa aliyechangia kujengwa au kutoa misaada kanisani ya kifedha ni mingi kuliko aliyetoa kwa ndugu zake waislam. Acheni chuki.
Kama rushwa basi huko kanisani ndio wamekula kweli kweli kuliko hata waislam,kwa haraka haraka naamini wote kutoka upande huo watampa Samia uchaguzi ujao.