Rais Samia amerithi nchi iliyofilisika kifedha na kiuchumi

Rais Samia amerithi nchi iliyofilisika kifedha na kiuchumi

hii propaganda haijakaa vizuri bwashee.
unaweza kuwa na ukweli lakini tumia akili ueleza ukweli wako.

Baada ya MAGUFULI kulala usingizi wa milele, yameibuka mengi.TOZO lukuki.kwamba hali ya uchumi iko mbaya ndiyo maana SGR na BWAWA la umeme wa NYERERE haviwezi kujengwa ??? hahahhaaa.unafiki bana.tunajua kuna wafanyabiasha wenye maloli hawataki SGR ijengwe ,unafikiri hatujui? tunajua kuna makapuni ya kufua umeme kwa njia ya upepo unajua hatujui?acha kumharibia mama ,na kama ni TISS wamekutuma kupima upepo wambia mmenidanganya aisee,tena mnamharibia mama. uchumi umeharibika huku mishahara ikiongezwa ,posho zikiongezwa,perdiem zikiongezwa,safari za kila siku zikipamba moto nk . Yani wewe mwenye thread hii nikikwita mwehu nafikiri nitakuwa sijakosea .

sisi wananchi siyo kwamba hatutaki kulipo kodi na tozo mbali mbali.kama kodi na tozo mbalimbali zinaenda kujenga SGR,Bwawa la umeme,fyeover,vivuko ,kununua dawa za hospitali,kujenga vituo vya afya ,kuboresha elimu nk mbona hatuna shida kuliko kutuambia upumbafu ati hayati Magufuli aliharibu uchumi?? Kama umetumwa na CCM kwa hakika tumerudi nyuma kwa kasi ya ajabu .unakumbuka 2014 -2015 ukivaa kofia au nguo ya CCM ulivyoonekana jangili fulani? 2025 siyo mbali
 
Pamoja na kwamba rais aliyepita Kuna mambo aliharibu , isiwe ndiyo excuse ya mambo jinsi yanavyoenda mama,, kusema ule ukweli mchungu ni kwamba rais amekosa watu ambao ni think tank ambao wangemsaidia kuufufua uchumi unaoelekea shimoni, yani hauwezi kukuza uchumi kwa kukwangua pesa za walalahoi na kuzilundika hazina na kwenye ma account ya serikali kwakua haitaongeza thamani, Sasa waziri wa fedha analeta double taxation kwa watu ambao vipato vyao havijaongezeka!!! Zaidi zaidi anasababisha purchasing power ya raia wake ipungue, then what next, ?hiyo Wizara ampe mtu ambaye atakua na maono thabiti Ila siyo huyu anayekuja na solution ya kwamba kama mtu hataki tozo ahamie Burundi, what the Joke?
 
Wewe ndo mpumbavu kwa Nini usidadavue kwa hoja Kama mleta mada? Unakuja na vijimaneno viwili vitatu halafu unatukana.
Tumia akili boya wewe huyo mnayemsema kakopa sana ni shilingi ngapi na ndani ya muda gani na kumbuka alikuwa anafanya project gani na ngapi,compare na huyu shangazi yako amekopa 10 T ndani ya mwaka mmoja na bado anaendelea kutuumiza wananchi na vitozo vya kithenge na hakuna project yoyote aliyoanzisha zaidi ya matundu ya choo achana na hela za covid,mchukieni magufuli, lakini mazuri yake ni mengi kuliko hayo mabaya mnayo yasambaza kwa nguvu zenu zote.....pamoja na hayo yote watanzania hapo na nyie mafisi wenye uchu na mali zao.
 
Yaani sitasahau sekta ya kilimo alivyoivuruga bwana yule! Unatumia 2.5m kwa kilimo unakuja kuuza less than 1m dah sitasahau..pembejeo juu, mbolea juu halafu unapangiwa Bei ya kuuza! Halafu wale wa ntwara koro show iliishia wapi?
Wewe ni mjinga mpumbavu na unajifunza uchawa kutoka kwa machawa wenzako, unasema pembejeo kipindi cha magufuli bei ilikuwa juu shilingi 47000 mpaka 52000 kwa 50 kg na vocha kama zote kwa wakulima utalinganisha na sasa hivi mfuko wa kg 50 unauzwa 140000 mara tatu ya bei kwa jpm ,na kibaya zaidi pembejeo zimepanda kabla ata rusia na ukraine hawajaanza chokochoko na kuanza kupigana ,
Usiongee vitu kama vile watanzania walikuwa wameenda burundi wakati ule na wamerudi sasa nchini mwao.
 
kupitia MIKOPO ,Shirika la Ndege na Ndege zikaonekana.... SGR, JNHEPP, Sengerema Sasa imeunganishwa na Barabara .


KWA UFUPI, NI TAHIRA TU KAMA WEWE AMBAYE HUONI KILICHOFANYWA NA JPM.



Haya niambie, zaidi ya kuruhusu Upigaji, nakusifia Ndoa za wanaume walooa wake wengi wengi kama yeye kua mtara,. Na kuchochea Mimba za wanafunzi .


Kipi amekifanya Kwa MaTrilioni ya Pesa alizokopa Mama yenu ??.
Akikujibu niite mbwaa nimekaa pale.
 
Tumia akili boya wewe huyo mnayemsema kakopa sana ni shilingi ngapi na ndani ya muda gani na kumbuka alikuwa anafanya project gani na ngapi,compare na huyu shangazi yako amekopa 10 T ndani ya mwaka mmoja na bado anaendelea kutuumiza wananchi na vitozo vya kithenge na hakuna project yoyote aliyoanzisha zaidi ya matundu ya choo achana na hela za covid,mchukieni magufuli, lakini mazuri yake ni mengi kuliko hayo mabaya mnayo yasambaza kwa nguvu zenu zote.....pamoja na hayo yote watanzania hapo na nyie mafisi wenye uchu na mali zao.
Unajilisha upepo siyo? Hizo project za mfukoni ndo zimetufikisha hapa! Unajua biashara ngapi aliua huyo mtu wenu? Sekta binafsi zilikuwa hoi bin tete...ikaja kubainika mashirika ya umma yalijiendesha kwa hasara halafu bado yalitoa gawio kwa bwana yule. Ila sisi watanzania aliyeturoga alaaniwe kabisa alichofanikiwa yeye ni kutushikisha adabu na kutuziba midomo. Huwezi ukaua biashara za watu kwa kuwabambikizia mikodi ya ajabu ajabu...hivi huwa unasoma hata ripoti za CAG wewe?
 
kupitia MIKOPO ,Shirika la Ndege na Ndege zikaonekana.... SGR, JNHEPP, Sengerema Sasa imeunganishwa na Barabara .


KWA UFUPI, NI TAHIRA TU KAMA WEWE AMBAYE HUONI KILICHOFANYWA NA JPM.



Haya niambie, zaidi ya kuruhusu Upigaji, nakusifia Ndoa za wanaume walooa wake wengi wengi kama yeye kua mtara,. Na kuchochea Mimba za wanafunzi .


Kipi amekifanya Kwa MaTrilioni ya Pesa alizokopa Mama yenu ??.
Na wewe pia ni wa Chato
 
Wewe ni mjinga mpumbavu na unajifunza uchawa kutoka kwa machawa wenzako, unasema pembejeo kipindi cha magufuli bei ilikuwa juu shilingi 47000 mpaka 52000 kwa 50 kg na vocha kama zote kwa wakulima utalinganisha na sasa hivi mfuko wa kg 50 unauzwa 140000 mara tatu ya bei kwa jpm ,na kibaya zaidi pembejeo zimepanda kabla ata rusia na ukraine hawajaanza chokochoko na kuanza kupigana ,
Usiongee vitu kama vile watanzania walikuwa wameenda burundi wakati ule na wamerudi sasa nchini mwao.
Wewe lofa Mimi nimeingia field siyo kilimo Cha mtandaoni unajua kiazi kimeuzwa Bei gani 2019? Au kisa unakula chipsi kavu za buku jero hapo mzizima unahisi umeyapatia maisha? Nenda kaone vilio vya wakulima walivyolia huko mikoani ndo uje uharishe hapa. Anyway mungu fundi alituamulia
 
umepewa buku ya bando unakuja kuharaaa mtandaoni!acha unafki na maisha huna.
Uzuri ni kwamba wapiga kura hawapo jf Wala Twitter ingekuwa hivyo sawa. Ila tuliopo field ndo tunajua. Sasa hivi tuna amani na hata transparency ipo hivi bwana yule alivyokuwa kamanda kwelikweli ...hata angeanzisha hizi tozo unadhani Kuna nyumbu ingethubutu kuhoji?
 
We Kweli una wazimu sasa Samia ye alikua si makamo wa Rais au ye alikua uraia !!!!fala weeh [emoji38][emoji38][emoji38]
Ujinga wako ungekuja kuandika kama serikali nyingine imechaguliwa sasa serikali si ile ile chama kile kile [emoji3] lipi jipya hapo wakati mwengine kabla ya kuandika uishirikishe akili yako vizuri na ubongo wako
IM DONE [emoji736]
Hivi wewe ulikuwa wapi kipindi MAGUFULI anatawala? Mbona mnapenda mambo ya kijinga. Nani asie jua kama FASHISTI MAGUFULI alikuwa ashauriki samaia angefanya Nini? Yule Jamaa alikuwa Zaid ya shetani....
 
Unajilisha upepo siyo? Hizo project za mfukoni ndo zimetufikisha hapa! Unajua biashara ngapi aliua huyo mtu wenu? Sekta binafsi zilikuwa hoi bin tete...ikaja kubainika mashirika ya umma yalijiendesha kwa hasara halafu bado yalitoa gawio kwa bwana yule. Ila sisi watanzania aliyeturoga alaaniwe kabisa alichofanikiwa yeye ni kutushikisha adabu na kutuziba midomo. Huwezi ukaua biashara za watu kwa kuwabambikizia mikodi ya ajabu ajabu...hivi huwa unasoma hata ripoti za CAG wewe?
Nitajie biashara tano alizoua jpm namimi nikutajie project kumi ambazo zilikuwa zinaendelea vizuri pasipo mwananchi kubebeshwa zigo la tozo wala kuwepo na mfumuko wa bei .
 
Wewe lofa Mimi nimeingia field siyo kilimo Cha mtandaoni unajua kiazi kimeuzwa Bei gani 2019? Au kisa unakula chipsi kavu za buku jero hapo mzizima unahisi umeyapatia maisha? Nenda kaone vilio vya wakulima walivyolia huko mikoani ndo uje uharishe hapa. Anyway mungu fundi alituamulia
Ndo maana nasisitiza wewe ni mpumbavu pro na kibaya zaidi uchawa hauwezi ndo unajifunza baby class hivyo viazi unavyo vizungumzia vililimwa mbolea iko na bei gani? Je unajua supply ya viazi mwaka huo ilikuwa ni kubwa kiasi gani mpaka tukawa tunazuia viazi visiingie kutoka kenya,wenzako wanalima kwa ramani weee unalima kwa kujidanganya kijiweni fala wewe
 
Nitajie biashara tano alizoua jpm namimi nikutajie project kumi ambazo zilikuwa zinaendelea vizuri pasipo mwananchi kubebeshwa zigo la tozo wala kuwepo na mfumuko wa bei .
1. Efatha
2.Covenant Bank,
3. KILIMANJARO COMMUNITY BANK
4. Njombe Community Bank,
5. Kagera Farmers’ Cooperative Bank, and
6. Meru Community Bank
7. Federal Bank of the Middle East
8. Tanzania Investment Bank (TIB)
9. China Commercial Bank Limited
10. Bank M
11. Twiga Bank
12. Mbinga Community Bank

Hizo ni bank tuu ngoja nifanye miamala nilipe tozo tujenge nchi ntarudi na sekta zingine
 
Ndo maana nasisitiza wewe ni mpumbavu pro na kibaya zaidi uchawa hauwezi ndo unajifunza baby class hivyo viazi unavyo vizungumzia vililimwa mbolea iko na bei gani? Je unajua supply ya viazi mwaka huo ilikuwa ni kubwa kiasi gani mpaka tukawa tunazuia viazi visiingie kutoka kenya,wenzako wanalima kwa ramani weee unalima kwa kujidanganya kijiweni fala wewe
Brother hiyo biashara sikuianza huo mwaka.. inflation ilikuwepo Ila siyo ya kiasi kile. Kwani hao Kenya walikuwa hawalimi toka zamani? Haya na korosho, mbaazi, kahawa nk. Nani aliua? Kuna mengi JPM alifanya Ila kwenye sekta ya kilimo na elimu alifeli vibaya...kipindi chake ndo tuliona 60% ya wanafunzi shule fulani wanapata div one 7pts halafu ndo kipindi chuo kikuu wamedisco Sana.
 
Unaandika huku unatetemeka.
Yah natetemeka kwa hasira. Ila tuacheni utani lipa tozo zote ishakuwa Sheria huna namna, mlimpigia makofi Sana marehemu alipopora uchaguzi Sasa hakuna wa kuwatetea tunalipa pamoja...hutaki chukua ushauri wa Mwigulu hamia hata Burundi tu 😀😀ukawatumikie hata waasi
 
Rais Magufuli alirithi nchi yenye mzunguko wa pesa imara na Ukuaji ulioimarika toka kwa Jakaya Kikwete, Uchumi wa Jakaya Kikwete wa kuajiri maelfu ya watu kila mwaka, na kulipa malimbikizo, Kuongeza mishahara, Kulipa wastaafu kwa wakati, Biashara na wawekezaji kushamiri. Ilituchukua zaidi ya miaka ishirini kufika uchumi wa Jakaya Kikwete.

Faida aliyoipata Jakaya Kikwete hakuvuruga miundo mbinu na matajiri ambao Rais Mkapa aliwajenga ambao ndio wazalishaji wakubwa Nchini bali aliboresha na Kutengeneza mazingira bora zaidi ya kuajiri na kulipa kodi.

Rais Magufuli aliamua Yeye kuvuruga na kufilisi nchi, Hakuishia kuvuruga akaamua na kujaza wasukuma ili waongee kisukuma kwenye sekta muhimu, Bora ingekuwa wasukuma smart wenye ABC za uchumi bali aliwajaza chawa wa kusifu, kuimba na Wengine kama kangi Lugola na Kabudi wakaamua kukufuru kabisa kuwa Rais Magufuli Yeye ni Alfa na Omega.

Rais Samia amepokea nchi ambayo haina uwezo wa kujenga miradi ya SGR na Bwawa la umeme la Nyerere.

Magufuli alikopa pesa za miradi ya SGR na Bwawa la Nyerere kwa pesa ambayo hata nusu ya miradi haiwezi kukamilika, Wakati watu wanahoji kuhusu gharama za mikopo hii na itakuaje baadae waliitwa hao watu sio wazalendo na Wanatumika na Mabeberu, Alipoulizwa Bwawa la zaidi ya Trilioni tano pesa za kumalizia zitatoka wapi alijibu pesa za ndani na nchi ni tajiri huku akishindwa kulipa wastaafu na malimbikizo.

Nani yupo tayari tukakope pesa zingine matrilioni ya pesa kumalizia Bwawa la umeme ambalo maji yake hayana uhakika na mabadiliko ya tabia nchi tayari yanaonekana kwa mkoa wa Dar es Salaam kuwa na baridi ya kutosha na watu kuvaa makoti asubuhi na jioni kama tupo Iringa au Mbeya.

Chawa wakuu walikuwa hawajasoma uchumi wala hawajui maana ya Demand and Supply, Chawa kama Bashiru Ally na Humprey Polepole hawakuwa na ABC za uchumi au mambo yanayohusu mikopo lakini hawa ndio waliaminiwa kama wa shauri wa kujenga SGR.

Rais Magufuli baada ya kuona uchumi ni imara na wawekezaji wanaiamini Tanzania akaanza kuvuruga mifumo ya demokrasia na uwekezaji.

Rais Magufuli alifilisi viwanda na kufilisi wamiliki wa hivyo viwanda walioajiri watu wengi kwa ahadi yake Wataishi kama mashetani.

Ni kweli wazalishaji wakubwa kwenye uchumi wetu waliishi kama mashetani wakati wa Magufuli, Kodi inaongezeka kutokana na uzalishaji, Sasa kama miaka mitano unatumia kuua uzalishaji wa nchi baadae ukimaliza muda wako au ukaondoka kama alivyo Ondoka tunapata wapi kodi.

Leo ameacha nchi yenye madeni kila kona kuanzia madeni ya ndani kwa wastaafu wa PSSf na NSSF, Wazee wastaafu walilimia meno awamu ya tano.

Wafanyakazi waliishia pia kama mashetani kwa kuamua kutolipa malimbikizo yao baada ya kuona uchumi unaporomoka na Yeye ndie Chanzo akabaki anaimba Tazara Interchange na Kijazi Interchange wakati hayo ni madaraja ya kawaida ambayo hakuifuata ramani halisi ya ujenzi kama ilivyotakiwa.

IMF na World Bank waliionya awamu ya tano kuhusu Ukuaji wa uchumi, Lakini Rais aliyekuwepo kushirikiana na ofisi za Takwimu hapa Tanzania waligoma kuhusu Ukuaji wake wakaja na data zao feki kuwa uchumi unakuwa kwa asilimia 7 kuelekea 8%, Takwimu za IMF na Bank ya dunia zilionyesha uchumi wetu umeporomoka na kufika asilimia 4%.

Baadae awamu ya tano kupitia Spika Ndugai wakatunga sheria bungeni kudhibiti utoaji wa Takwimu ili kuwafunga mdomo wachambuzi kama Zitto Kabwe.

Zitto Kabwe alimuonya Rais Magufuli na hata kumuandikia barua kuhusu Madhara ya anachokifanya kwenye uchumi wetu kuwa itachukua miaka zaidi ya kumi tena kujenga Uchumi aliouacha Jakaya Kikwete.

Tutapata wapi pesa za kuendesha nchi tena, Ni miaka mingapi itatuchukua tena kurudisha uchumi aliouacha Jakaya Kikwete wa asilimia 6.5%-7.5%

Rais Samia ana mapungufu yake lakini suala la kutuweka wazi anatuweka wazi kila kitu kinachoendelea, Suala la ushauri, Rais Samia anapokea ushauri na amewaacha watanzania waongee wanavyotaka.

Tunamlalamikia Mama Tozo lakini ukweli watu waliovuruga nchi hii kwa Mamlaka waliyopewa ni kiongozi wa awamu ya Tano yaani Rais.

Kwa principal za uchumi mkubwa itatuchukua miaka zaidi ya kumi tena nchi kukaa sawa na hata Rais Samia atamaliza muda wake uchumi wa Kikwete hatutaufikia kabisa.

Rais Samia anahangaika na nchi ambayo uzalishaji umeshuka, Uwezo wetu wa kuuza nje umeshuka, Rais Samia atakusanya wapi kodi wakati uzalishaji ndani ya nchi umeshuka?

Hussein Bashe anajitahidi kumsaidia Rais Samia uzalishaji ukue kwa kuja na mbinu mbalimbali lakini Kumbuka uchumi ulivurugwa na tukarudi hatua zaidi ya miaka kumi nyuma.

Rais Samia na Hussein Bashe watapambana kwenye kuboost uzalishaji lakini wataondoka bado uchumi wetu hautafika asilimia alizoziacha Jakaya Kikwete.

Katiba ni muhimu sana ili kudhibiti watawala wanaoturudisha nyum jpm alichukiwa kwa usili na kuto kuwa muwazi samia atachukiwa kwa uwazi na ukweli juu ya mapungufu ya mtangulizi wake jpm IKO WAZI KWAMBA INCH ILIACHWA PATUPU na kibaya zaidi wanao jua walimuachia nchi pabaya huyu mama Samia ndiyo wanao ongoza kwa kumbeza mitandaoni kwa katuni sauti nk.NIME WAHI JIULIZA kivipi mama Samia akubali kudhalilika juu ya vilio vya tozo na ili Hali Ana uwezo was kulifanyia kazi BASI NIKA NOTE HUENDA HALI NI MBAYA na anaogopa kuwa weka WAZI watu kwa hofu KWAMBA ataulizwa ulikuwa wapi kumshauli? Samia amebeba mzigo mzito kiukweli.BINAFSI NAMWOMBEA NA NAMPONGEZA KWA KUKUBALI AIBU YA MTU MWINGINE
 
We Kweli una wazimu sasa Samia ye alikua si makamo wa Rais au ye alikua uraia !!!!fala weeh [emoji38][emoji38][emoji38]
Ujinga wako ungekuja kuandika kama serikali nyingine imechaguliwa sasa serikali si ile ile chama kile kile [emoji3] lipi jipya hapo wakati mwengine kabla ya kuandika uishirikishe akili yako vizuri na ubongo wako
IM DONE [emoji736]
Kwamtu aliye kuwa anamfaham vizuri jpm si Hilo si swali la kuuliza
 
Back
Top Bottom