Rais Samia amsimamisha kazi Ole Sabaya, Mkuu wa Wilaya ya Hai ili kupisha uchunguzi wa tuhuma dhidi yake

Sio Huyu Tu Mama Samia Hawa watu walioumiza Watu sana wako Wengi na bado wana nafasi nyeti..Tafadhali wapige hawa watu kwasababu ni watesi waongo na wazushi Wakubwa...
 
Safi sana sasa tunakutana kimtaa mtaa tuone nani ni mbabe wa kweli,lazma tumnyonyoe vinyoleo
 
Jamani hivi yule wa Mbeya na yule wa Iringa wapo kweli !!!???

Maana tangu "MWANAKWENDA ZAKE na AENDE" alipoondoka kama siwasikii tena naona wana act low profile sana

... au ilikua nguvu ya Azam Cola gesi imeisha na wao chali pressure zinapanda na kushuka

Ama kweli kila zama na Nabii wake !!!
 
Kumekuwa na malalamiko mengi kuhusu utendaji wake hata clip za wafanyabiashara mfano mmiliki wa Weruweru lodge alitamka hadharani kuhusu kulazimishwa kutoa fedha.Lema alisema sana kuhusu tuhuma mbalimbali.Tuache mkondo wa sheria na haki tuone hatma yake.Ila kikubwa " guilty until proven innocent"
 
Watu walionya sana kuhusu vitendo vya hawa wateule.
Tulijua kuwa utetezi waliokuwa wanaupata ni wa muda tu, maana vyovyote iwavyo waliapa kuilinda katiba ya Tanzania.
Acha tuone mwisho wake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…