Rais Samia amsimamisha kazi Ole Sabaya, Mkuu wa Wilaya ya Hai ili kupisha uchunguzi wa tuhuma dhidi yake

Amulike Tanga jiji maana mkurugenzi nae anatumia ofisi vibaya. Ummy anamlea huyu rafiki take. RC na DC hawana hata uwezo wa kumhoji mkurugenzi Hugo Mh. Rais saidia kuondoa mnynyasaji,mvunja maadili,mbadhirifu na mtoa rushwa.
 
Uyo kashapigwa chini mkuu,,Sabaya ni jambazi hakuna asiyemjua,
 
Kazima tayari tukio la mechi ya Yanga na Simba kuhairishwa watanganyika bwana kha!!
Kwahiyo alitakiwa asitangaze uteuzi/utenguzi wowote ule mpaka hatma ya tukio la yanga na simba ijulikane? Aisee Rais ana kazii nchi hii.
 
Pole sana Sabaya. Mawimbi ni sehemu ya tabia nchi baharini! Kama ulitenda uovu unajua na nafsi yako lakini wajibu wangu ni kukuombea [emoji120]
 
Aaaah aah wanazi wa CHADEMA watafurahi sana!

Lakini kazi aliyofanya kwa wananchi wa kawaida ni ya kutukuka!pamoja na uwezekano wa kuteleza hapa na pale!

Bravo Sabaya!,

Mengine yanatazamika, yanatafsirika, yanajadilika, na yanasubirika. Muda utatoa maana Pana ya yanayotukia sasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…