Rais Samia amsimamisha kazi Ole Sabaya, Mkuu wa Wilaya ya Hai ili kupisha uchunguzi wa tuhuma dhidi yake

Achana na huyo hahitaji hata kuwa na elimu ya Darasa la saba kuhoji kwa nini anachukiwa. Matendo ya mtu huendana nae
 
Tanzania ilitupwa kwenye mikono ya shetani. Mungu alimuua shetani Mkuu na sasa sisi tuwaue vishetani vilivyosalia.
 
Mungu katenda lililo jema kwa mwendazake. Aliharibu na kunajisi mifumo yote ya Uongozi kwenye Nchi yetu. Angeendelea kwa miongo mingine sijui Nchi ingekuwa ktk hali gani???
 
Mie nasubiri uchunguzi, lakini kawaida siridhiki na chunguzi au mihemko. Sheria zibadilishwe suala la DC/RC kuwa na uwezo wa kumueka mtu ndani 48 ni sawa na kumpa chizi rungu mbele kuna vioo. Sioni sababu ya kuwa na mahakama ikiwa kuna njia za mkato za watu kutoa hukumu!
 
Mtu kama huyu bado kuna watu wanamkingia kifua lakini sio ajabu kwani hata Hitler alikuwa na wapambe. Kama huyu hatafungwa jela basi hakuna hata sababu ya hizo jela kuwepo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…