Rais Samia aondoka Nchini kwenda DR Congo leo Agosti 16, 2022

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiagana na Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa pamoja na viongozi mbalimbali katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (Terminal 1) Dar es Salaam wakati akielekea Jamhuri ya Kidemokraisa ya Kongo, tarehe 16 Agosti 2022.

Rais Samia anaenda kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

Kujua safari zingine za Rais soma hapa.

Picha: Ikulu
 
Atukumbuke na sisi tunaoidai serikali maana kama ni kufa tumekufa moyo siku nyingi lakini alipoingia madarakani akatukumbuka!
 
Atukumbuke na sisi tunaoidai serikali maana kama ni kufa tumekufa moyo siku nyingi lakini alipoingia madarakani akatukumbuka!
Watu si walisema Mama atamwaga pesa, imekuwaje tena?
 
Ila jamani watalaam wa afya wa Rais muwe makini kidogo isije kuwa mheshimiwa Rais anahitajika pia kupumzika Safari huwa zinachosha Sana kazi hizi zipo tu na zitaendelea kuwepo Mimi naanza kumuonea huruma ila kazi anachapa
Wewe unaongeza nn aseeee? Hapa kazi tu amepokea kijiti mwacheni amalizie mbio zake na hii ndio inakamilisha msemo wa mama anaupiga mwingi, atapumzika baadae.
 
Ila jamani watalaam wa afya wa Rais muwe makini kidogo isije kuwa mheshimiwa Rais anahitajika pia kupumzika Safari huwa zinachosha Sana kazi hizi zipo tu na zitaendelea kuwepo Mimi naanza kumuonea huruma ila kazi anachapa
Hao hao wataalamu wa afya, wamshauri pia awe anapitapita Gym mara moja moja, kwa afya pia.
 
πŸ™†πŸ™† Khaaa πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Mh Rais anachapa kazi bila kupumzika, Huyu Ni zawadi kwetu watanzania, Tumuunge mkono mh Rais wetu, maana Ni katika mikutano hiyo anakutana na watu, mashirika na taasisi mbalimbali, ambapo Ni katika mikutano hiyo mh Rais anapofanya mazungumzo nao ya kuwaeleza fursa mbalimbali zinazopatikana hapa nchini ili waje wawekeze hapa nchini

Nikupitia uwekezaji huu tunapoongeza ajira na hata mapato ya nchi kupitia kodi.

Hongera Sana mh Rais na pole Sana kwa kazi kubwa uifanyayo ya kuijenga nchi hii kwa ajili yetu watanzania

Kila la Heri mh Rais katika mkutano huo, Watanzania Tunakuombea mh Rais uende salama na kurejea salama hapa nchini.

Watanzania tunaendelea kukuunga mkono Rais wetu katika juhudi zako za kuijenga nchi yetu.
 
90% ya petrol station ni mali za makada wa CCM, usitegemee muujiza
Na tatizo kubwa lipo hapa,mpaka Jana mafuta yanashuka siku zaidi ya 60 kwetu yanapanda tu,Mimi naona hata hiyo ruzuku ni changa tu hakuna kitu,tunadanganywa sana.,Au sisi mafuta yetu tunanunua sehemu tofaut na nchi nyingine?
 
Maskini Mpango amekuwa wa kusindikiza kila siku na kumpokea...utafikir familia flani anaposafiri baba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…