Rais Samia aongea na Wazee wa Dar: Aahidi kutojali vyama katika teuzi zake. Serikali kutunza Haki, Demokrasia, Uhuru wa Habari

Rais Samia aongea na Wazee wa Dar: Aahidi kutojali vyama katika teuzi zake. Serikali kutunza Haki, Demokrasia, Uhuru wa Habari

Wazee wamemkomalia bi mkubwa et vijana hatuwaachii siti kwenye daladala. Aaa kwani sisi vijana tunapanda bure hizo daladala! wazee tumieni pension zenu kununua usafiri na mkiona tunawakera bakini nyumbani mcheze na wajukuu zenu. Hii si awamu ya wanyonge.
 
Amesema wazi kuwa leo hana jambo zito la kuzungumza na wazee kwa maana wazee ndio wamemuomba.
 
"Sisi pia tunakuja huko (uzeeni), hivyo tusipoandaa mazingira nasi pia yatatukuta
 
Kitendo cha Rais kuvaa barakoa ni cha kupongezwa sana utakuwa ni mfano mzuri hasa kwa wale wabishi wa kujikinga na hiki kirusi hatari ambacho kimesababisha maafa makubwa na ya kutisha dunia yote.
usikuze mambo rais katoa sababu kwa nini barakoa zimevaliwa

Rais Samia Suluhu Hassan
Naomba niwaombe radhi kwamba mtindo wa maisha umebadilika. Tumekuja na vikaba midomo ninyi pamoja na sisi

Kwasababu mkusanyiko huu ni mkubwa na Wazee ni rahisi kupata haya maambukizi, hatuwezi kujua nani anayo na nani hana. Sisi wenzenu tunazunguka sana
 
Mama swali ni hilo: na wazee wa umri mkubwa watasimama kuitwa kwa Mungu ili faida ikipatikana wagawiwe?
Kwani wazee hawana ndugu, watoto au wajukuu? Wanafaidika indirect.....
 
Wazee wamemkomalia bi mkubwa et vijana hatuwaachii siti kwenye daladala. Aaa kwani sisi vijana tunapanda bure hizo daladala! wazee tumieni pension zenu kununua usafiri na mkiona tunawakera bakini nyumbani mcheze na wajukuu zenu. Hii si awamu ya wanyonge.

Itoshe kusema ukishafika umri wa uzee ni bora ukakae nje ya mji shambani kula upepo tulivu,ukija mjini njoo na Cruiser V8 kutembelea wajukuu.
 
Kwasababu mkusanyiko huu ni mkubwa na Wazee ni rahisi kupata haya maambukizi, hatuwezi kujua nani anayo na nani hana. Sisi wenzenu tunazunguka sana
Ndio Siasa zenyewe hizi ili kuwapoza Mazezeta wa Mwendazake
 
"Ugumu wa maisha sio sababu ya mtu kuwa mwizi, kuna sababu nyingine nyingine huko. Nimesikia hapa, Dar es Salaam watu wameanza kujaribu kina cha maji, wizi na uporaji Umeanza. Nasema wasijaribu na Mkuu wa Jeshi la Polisi kalishughulikie hilo"
 
View attachment 1776541
Jamani, barakoa tele! Maendeleo hayo?
Analeta desturi za Kenya (na za dunia....)?
Ila zinasaidia kiasi tu wakati watu wanabanana ndani ya ukumbi . . .
usipotoshe siyo hivyo rais katoa sababu

Rais Samia Suluhu Hassan
Naomba niwaombe radhi kwamba mtindo wa maisha umebadilika. Tumekuja na vikaba midomo ninyi pamoja na sisi

Kwasababu mkusanyiko huu ni mkubwa na Wazee ni rahisi kupata haya maambukizi, hatuwezi kujua nani anayo na nani hana. Sisi wenzenu tunazunguka sana
 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewasili Ukumbi wa Mlimani City kuongea na Wazee wa Dar es Salaam

Tunakuletea updates hapa

Mwenyekiti wa Wazee wa Dar, Salum Matimbwa
Tumepata kadi za msamaha wa Bima, lakini Wazee hatupati baadhi ya vipimo na Dawa tukifika Hospitalini

Tunaomba Rais Samia tunapokuwa Hospitalini, tupate vipimo na dawa zote kadri ya Magonjwa yanayotusibu

Tunakupongeza kwa kusimamia Sheria na Utawala bora. Tunaomba juhudi ziendelee ili kushughulikia kero za Wananchi

Vyombo vya Ulinzi na Usalama vifanye kazi kwa Sheria, Kanuni na Utaratibu waliojiwekea. Inapobidi Wananchi washirikishwe ili kuondoa manung'uniko

Wazee tunaomba Vyombo vyote vya Usafiri wa Umma vitenge viti maalum vya kukaa wazee

Pia, vihimizwe kuhakikisha vinawabeba wajukuu zetu ambao ni Wanafunzi wanapokwenda na kurudi shuleni

Kuna uwakilishi wa makundi mbalimbali #Bungeni lakini Wazee hatuna uwakilishi

Hivyo tunaomba na sisi ikikupendeza Rais, tupewe nafasi hiyo ili tupate Watu wa kutusemea matatizo yetu kwenye Vyombo vya Mamlaka

Waziri wa Afya - Dkt. Dorothy Gwajima
Wazee wanazidi kuongezeka. Mwaka 2012 kulikuwa na Wazee milioni 2.5 sawa na asilimia 5.6 na hivi sasa wameshafika milioni 2.52.

Mauaji ya wazee yamepungua kutoka 577 mwaka 2014 hadi wazee 34 mwezi Desemba mwaka 2020.

Rais Samia Suluhu Hassan
Naomba niwaombe radhi kwamba mtindo wa maisha umebadilika. Tumekuja na vikaba midomo ninyi pamoja na sisi

Kwasababu mkusanyiko huu ni mkubwa na Wazee ni rahisi kupata haya maambukizi, hatuwezi kujua nani anayo na nani hana. Sisi wenzenu tunazunguka sana

Wazee wameona mengi na wana uzoefu mkubwa. Ndiyo maana tumeona tuje kuzungumza nanyi ili tuone mnasema nini na mnatuambia nini

Ni utamaduni, toka tumepata Uhuru Viongozi wetu wamekuwa wakikaa na kuongea na Wazee. Mimi sina jambo ila nimekuja kuwasikiliza

Mbali na Sera, Ilani ya CCM inatutaka kufanyia kazi suala la tiba ya Wazee. Waziri wa Afya ametoa ahadi nzuri lakini nataka aisimamie leo na sio kesho.

Dunia ipo kwenye Corona na wahanga wakubwa ni Wazee. Kamati niliyoiunda wanakwenda vizuri na karibu wataleta majibu

Nakubaliana nanyi kuhusu kuwawezesha kiuchumi lakini tuna Mfuko wa TASAF na tutakwenda kwenye Wilaya zote na kuhakikisha kila Mzee mwenye sifa anapata nafasi

Jambo la kutoa pensheni kwa kila Mzee tulipiga hesabu tukaona ni gumu kutokana na hali ya Uchumi

Corona imeshusha Uchumi karibu wa Dunia nzima. Pamoja na kwamba tutajitutumua tukue lakini tuna miradi mikubwa ambayo inahitaji kukamilika

Naomba mnipe muda niangalie hali ya Uchumi inavyokua halafu nitalitolea maamuzi. Tujenge Nchi kwanza halafu tutagawana faida

Wazee wanaoweza kuketi na Rais lazima ni wazee wenye uwezo, hawawezi kuwa wa kiwango cha kuomba msaada kuboreshewa kambi za wazee
 
usipotoshe siyo hivyo rais katoa sababu

Rais Samia Suluhu Hassan
Naomba niwaombe radhi kwamba mtindo wa maisha umebadilika. Tumekuja na vikaba midomo ninyi pamoja na sisi

Kwasababu mkusanyiko huu ni mkubwa na Wazee ni rahisi kupata haya maambukizi, hatuwezi kujua nani anayo na nani hana. Sisi wenzenu tunazunguka sana
Ulitegemea asema kuwa nimebadirika kuhusu barakoa? Lazima aseme hivyo ....
 
Back
Top Bottom