Rais Samia aongeza dau, kutoa Tsh. Milioni 10 kwa kila Goli kwa Yanga na Simba (CAFF na CAFCL)

Rais Samia aongeza dau, kutoa Tsh. Milioni 10 kwa kila Goli kwa Yanga na Simba (CAFF na CAFCL)

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameamua kuongeza fedha za motisha kwa timu za Simba na Yanga kutoka shilingi Milioni 5 hadi Shilingi Milioni 10 endapo timu hizo zitafuzu kucheza nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika na Kombe la Shirikisho Barani Afrika.

Simba ambayo ina uongozi wa 1-0 kutoka mchezo wa kwanza leo Aprili 28 inarudiana na Wydad Casablanca ya nchini Morocco wakati Yanga yenye uongozi wa 2-0 ikitarajiwa kurudiana na Rivers United ya Nigeria katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam siku ya Jumapili.

Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa amesema Rais dkt. Samia Suluhu Hassan anazitakia kila la kheri Simba na Yanga na amewataka wachezaji kujituma uwanjani na kutumia maarifa yao yote kuhakikisha wanashinda michezo ya kukamilisha robo fainali ili wafanikiwe kuingia nusu fainali ambapo kila goli litakuwa shilingi Milioni 10.

Aidha, Msigwa amesema magoli yatakayolipiwa shilingi Milioni 10 ni yale yatakayofungwa katika dakika 90 za mchezo au dakika 120 na sio magoli ya penati.

Pia soma: Rais Samia kununua kila goli Tsh. Milioni 5 mechi za Simba, Yanga CAF
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameamua kuongeza fedha za motisha kwa timu za Simba na Yanga kutoka shilingi Milioni 5 hadi Shilingi Milioni 10 endapo timu hizo zitafuzu kucheza nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika na Kombe la Shirikisho Barani Afrika.

Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa amesema Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan anazitakia kila la kheri Simba na Yanga na amewataka wachezaji kujituma uwanjani na kutumia maarifa yao yote kuhakikisha wanashinda michezo ya kukamilisha robo fainali ili wafanikiwe kuingia nusu fainali ambapo kila goli litakuwa shilingi Milioni 10.

Aidha, Msigwa amesema magoli yatakayolipiwa shilingi Milioni 10 ni yale yatakayofungwa katika dakika 90 za mchezo au dakika 120 na sio magoli ya penalti baada ya mchezo kumalizika
 
Hizi pesa kama zipo kwanini zisipelekwe kwenye vituo vya kulelea watoto yatima angalau wawe wanakula chakula kizuri kila mara, badala ya kuwasubirisha mpaka siku za sikukuu ndio wapelekewe michele, mbuzi, na mafuta?

Kwasababu hizi Simba na Yanga kwasasa zina wadhamini wakutosha, zinajimudu kwenye mahitaji yao tofauti na miaka ya nyuma walipokuwa wakinywa chai na chapati asubuhi, hata kama serikali ni walezi, muhimu waangalie pazito zaidi kupeleka hayo malezi.
 
Hizi pesa kama zipo kwanini zisipelekwe kwenye vituo vya kulelea watoto yatima angalau wawe wanakula chakula kizuri kila mara, badala ya kuwasubirisha mpaka siku za sikukuu ndio wapelekewe michele, mbuzi, na mafuta?

Kwasababu hizi Simba na Yanga kwasasa zina wadhamini wakutosha, zinajimudu kwenye mahitaji yao tofauti na miaka ya nyuma walipokuwa wakinywa chai na chapati asubuhi, hata kama serikali ni walezi, muhimu waangalie pazito zaidi kupeleka hayo malezi.
Una hoja, lakini nchi haina uhitaji wa yatima tu maisha mengine nayo yanaendelea
 
Hizi pesa kama zipo kwanini zisipelekwe kwenye vituo vya kulelea watoto yatima angalau wawe wanakula chakula kizuri kila mara, badala ya kuwasubirisha mpaka siku za sikukuu ndio wapelekewe michele, mbuzi, na mafuta?

Kwasababu hizi Simba na Yanga kwasasa zina wadhamini wakutosha, zinajimudu kwenye mahitaji yao tofauti na miaka ya nyuma walipokuwa wakinywa chai na chapati asubuhi, hata kama serikali ni walezi, muhimu waangalie pazito zaidi kupeleka hayo malezi.
Kinondoni pekee ina vituo 18 vya kulelea watoto tajwa.
 
Hizi pesa kama zipo kwanini zisipelekwe kwenye vituo vya kulelea watoto yatima angalau wawe wanakula chakula kizuri kila mara badala ya kuwasubirisha mpaka siku za sikukuu ndio wapelekewe michele mbuzi na mafuta.
Unaongea haya Kama nani?, Kila Jambo lina nafasi yake...!! Kwani matatizo Nchi hii ni yatima pekee?.
 
Tuna nchi ya ajabu yenye watu wa ajabu sana:

Screenshot_20230319-081205.jpg


Tungoje wenye kukenua nao waje.
 
Angeongeza pia kuwa kila goli tunalofungwa linafuta moja tulilofunga
 
Back
Top Bottom