Rais Samia apandisha kiwango cha Posho ya Kujikimu ya Safari za Ndani ya Nchi na Malipo ya Kazi Maalum kwa Watumishi wa Umma

Rais Samia apandisha kiwango cha Posho ya Kujikimu ya Safari za Ndani ya Nchi na Malipo ya Kazi Maalum kwa Watumishi wa Umma

Huyu mama kila ushauri anaopewa anakubali tu,,, .atamaliza muda wake hakuna alichofanya...
Unataka tukuonyeshe alivyofanya? Wenye chuki binafsi nawachungulia tuu mnavyoumia 🀣🀣🀣🀣🀣

Haya twende Kazi πŸ‘‡
 

Attachments

  • Screenshot_20220527-123220.png
    Screenshot_20220527-123220.png
    91.9 KB · Views: 24
  • Screenshot_20220524-120244.png
    Screenshot_20220524-120244.png
    159.4 KB · Views: 21
  • Screenshot_20220524-202142.png
    Screenshot_20220524-202142.png
    166.4 KB · Views: 17
  • Screenshot_20220524-202353.png
    Screenshot_20220524-202353.png
    161.9 KB · Views: 18
  • Screenshot_20220524-221526.png
    Screenshot_20220524-221526.png
    115.9 KB · Views: 16
  • Screenshot_20220525-192603.png
    Screenshot_20220525-192603.png
    105.5 KB · Views: 15
  • Screenshot_20220525-225828.png
    Screenshot_20220525-225828.png
    174.7 KB · Views: 18
  • Screenshot_20220525-225904.png
    Screenshot_20220525-225904.png
    253.1 KB · Views: 21
  • Screenshot_20220526-125408.png
    Screenshot_20220526-125408.png
    178.1 KB · Views: 21
Wameongezwa 20,000 kutoka 80,000-100,000 madereva na wahudumu viongozi 120,000-250,000
Viongozi ilikuwa 120, maafisa wa kawaida 100 na kada nyingine 80 kwa safari za kikazi ktk mikoani, Sasa Kama viongozi watakula 250, maafisa wa kawaida wanakula ngapi maana watumishi kada nyingine mpya inakuwa 100
 
Mbona hakuna uwiano kati ya kiwango cha chini na kiwango cha juu
 
Mapesa yanaishia tumboni tu.

Awamu hii madaraja na maflyover yataishia matumboni.
 
Acha watu wamalizie zile nyumba zao zilizoishia kwenye rinta na madirishani wakati wa JPM
 
RAIS SAMIA SULUHU HASSAN APANDISHA KIWANGO CHA POSHO YA KUJIKIMU YA SAFARI ZA NDANI YA NCHI NA MALIPO YA KAZI MAALUM KWA WATUMISHI WA UMMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ameendelea kuupiga mwingi kwa kutoa kibali cha kurekebisha posho ya kujikimu ya safari za ndani ya nchi kwa Watumishi wa Umma na kiwango cha malipo ya kazi maalum (Extra Duty) kwa Watumishi wa Umma nchini ambapo utekelezaji wake unaanza rasmi tarehe 01 Julai, 2022.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro jijini Dodoma wakati wa Kikao Kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo vya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma chenye lengo la kutathmini utendaji kazi na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Dkt. Ndumbaro amesema kutokana na kibali hicho cha Mhe. Rais, posho ya kujikimu ya safari za ndani ya nchi kwa Watumishi wa Umma kwa kiwango cha juu imepanda kutoka shilingi 120,000/= hadi 250,000/= na kiwango cha chini kutoka shilingi 80,000 hadi 100,000/=.

Ameongeza kuwa, kiwango cha malipo ya kazi maalum (Extra Duty) kwa Watumishi wa Umma kimeongezeka kwa ngazi zote, ambapo kwa ngazi ya chini kimepanda kutoka shilingi 15,000/= hadi 30,000/=, kwa ngazi ya kati kimeongezeka kutoka shilingi 20,000/= hadi 40,000/= na kwa ngazi ya juu kimeongezeka kutoka shilingi 30,000 hadi 60,000/=.

Dkt. Ndumbaro amesisitiza kuwa, viwango hivyo vipya vitalipwa na Serikali kupitia bajeti iliyoidhinishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023, hivyo taasisi zisiombe nyongeza ya bajeti ili kuwalipa viwango hivyo watumishi wake.

Kufuatia ongezeko hilo, Dkt. Ndumbaro ametoa wito kwa Watumishi wa Umma wote nchini kufanya kazi kwa bidii, maarifa, weledi na nidhamu ya hali ya juu ili kuunga mkono kwa vitendo jitihada za Mhe. Rais za kuboresha masilahi wa Watumishi wa Umma.

β€œWatumishi wa Umma tuwajibike kwa hiari bila kushurutishwa, tuwe wabunifu zaidi ili kutoa mchango katika maendeleo ya taifa na ustawi wa nchi kwa ujumla ikiwa ni pamoja na kuhakikisha tunatatua kero zinazowakabili wananchi,” Dkt. Ndumbaro amesisitiza.
 
Back
Top Bottom