Rais Samia apokea Ripoti za CAG na TAKUKURU za Mwaka 2021/2022
Rais anajopo la washauri inavyoonekana mwanzoni hakuwa anawaamini ndiyo maana walimuacha aamue kila anapowabishia, sasa kaanza kujionea mwenyewe na bado inawezekana akaja kuwa mkali zaidi ya Dkt Magufuli na Tanzania itashangaa. Tumpe nafasi Mama
 
Rais anajopo la washauri inavyoonekana mwanzoni hakuwa anawaamini ndiyo maana walimuacha aamue kila anapowabishia, sasa kaanza kujionea mwenyewe na bado inawezekana akaja kuwa mkali zaidi ya Dkt Magufuli na Tanzania itashangaa. Tumpe nafasi Mama


E91CD2E7-1474-4814-8870-5D9950A53EEB.jpeg
 
Jiwe ndio hivyo tena. Dr. Samia anatosha.
 
Rais anajopo la washauri inavyoonekana mwanzoni hakuwa anawaamini ndiyo maana walimuacha aamue kila anapowabishia, sasa kaanza kujionea mwenyewe na bado inawezekana akaja kuwa mkali zaidi ya Dkt Magufuli na Tanzania itashangaa. Tumpe nafasi Mama
hahahahaha, Wasiwasi wangu ni kua unaweza kuwa unasubiri meli stendi ya mabasi!

Sent from my SM-A135F using JamiiForums mobile app
 
Mwanasiasa makini na mwerevu hawezi kum-discredit mtangulizi wake ili kujitwalia sifa binafsi. Ni mwanasiasa mpumbavu pekee atawashusha wenzie ili ajitwalie sifa yeye! Hope umeelewa.
Kabisa, hii tabia wamerithisishana, alianza Mwinyi, akaja Mkapa akaja JK na Dkt Magufuli, sasa Rais Dkt Samia, na kibaya afadhali kwa wenzake walikuwa hai na tawala tofauti ila ya kwake ni bosi wake na kafa na tena alipaswa azuie dhihaka ila yeye ndiyo anakomelea as if alimuua ili apande.

Yaani Rais Dkt Samia angepata neema ya kutambua japo kidogo tu madhara ya kauli zake na wateule wake zilivyomfanya aonekane hafai kabisa kuongoza hakika angeenda kuomba msahama kwenye kabuli la Dkt Magufuli na kuhakikisha anatubu.

Watanzania wanaumia mno maana mfumuko wa bei wanalalamika halafu yeye anasema afadhali wakati huo huo wizi anakili umeongezeka na wakato mwanzoni yeye huyo huyo alimdhihaki Dkt Magufuli kusema watu walikuwa na nidhamu ya uoga hahaha
 
Kufuatia Ripoti ya CAG 2021-2022; Rais Samia inaonyesha hatoshi kugombea urais kupitia ccm 2025.

Iwapo atagombea urais na ikatokea akashinda wanyonge wajiandae kufika 2030 wakiwa hawapati mlo wa siku na wachache watakuwa na fedha kuliko serikali jambo ambalo ni hatari kubwa....
Mimi naona andoke tu hapo aeleke kibanda maiti huko
 
Kuna usemi kwamba "Ya kale ni dhahabu. Model ya Magufuli itakumbukwa daima" Mama alipochukuwa nchi alisema hataki watu kuonewa akawaachia huru mafisadi waliowekwa ndani na serikali ya Magufuli (japo ela za Plea Bargaining zilizokuwa kwenye subira ya mchakato wa kisheria kuliwa nyuma ya Magufuli kufariki).

CAG Assad alipumzishwa kwa ripoti kama hizi hizi za CAG Kichere. Sijajuwa kama Kichere ataendelea kuvumiliwa hadi lini.

Mama hata kama hapendi mafisadi walio kwenye ripoti ya Kichere kushughulikiwa (kuonewa) lakini tayari CCM kimeshindwa kuvumilia na kuagiza serikali kuwachukulia hatua wahusika wote.

Pasina kujali udhaifu wa Mhimili wa Mahakama yetu lijapo suala la rushwa katika kufanya maamuzi ya mashauri, ni dhahiri kwamba mama sasa ana kigugumizi cha ni kwa vipi nilitoa mafisadi jela alafu leo tena niwarudishe jela ama wale wale au hata kama ni mafisadi wapya!

Huu ni mfupa mgumu kwa mama na huenda hata kwa CCM kilichompa maagizo kuwachukulia hatua za kisheria.

Dondoo chache kwenye ripoti ya CAG 2022 - 2023:

1. TTCL imekopesha watu wasiojulikana 21 bl.

2. Mkurugenzi Mkuu na maafisa wengine waandamizi wa TPA ambao wote waliondolewa kazini kwa utendaji mbovu bado wanaendelea kuidhinisha malipo kwenye mfumo wa TPA.

3. Takriban V8 mpya 40 za serikali zilizoagizwa zimeyeyuka bandarini.

4. CAG hakusaini (alirukwa) baadhi ya mikataba ya manunuzi makubwa ya kimkakati ughaibuni kama sheria inavyotaka.

Kwa ripoti hii ya CAG Kichere nchi inaenda wapi wakati wapigakura wanakula mlo mmoja? Mchele mbovu (chenga 3,100/)

Tujadili kwa ustaarabu kwa kujifunza kitu siyo kwa kushindana maana nchi ni yetu sote.
Screenshot_20230407-183154.jpg
 
Back
Top Bottom