Rais Samia atoa TZS 35BL Ujenzi wa Musoma Airport kumuenzi Baba wa Taifa

Kwa hiyo kuboresha Uwanja wa Ndege wa Musoma, alikozaliwa Mwalimu sio kumuenzi? Mwendazake alifanya unafiki mkubwa kwa kutoanzisha mradi wowote mpya mkoani Mara, japo alikuwa anajifanya anamuenzi Mwalimu. Mradi pekee aliowazuga watu wa mkoa wa Mara ni kukamilisha (sio kujenga) mawodi mawili matatu ya akinamama wajawazito na watoto kwenye hospitali ya Kwangwa, Musoma zaidi ya hilo hakuna. Hata mradi wa maji wa Bunda aliukuta ukiwa unaendelea tangu enzi za Kikwete. Mama kaamua kutengeneza airport ili kufungua njia nyingine za kiuchumi ikiwemo utalii maana wazungu wakishuka Musoma ni rahisi kwenda Serengeti
 
Mkuu sami huo uwanja kaja kukamilisha tu mradi umeanza enzi za jiwe maan ata fidia watu wamelipwa wakat wake
 
Nyerere haenziwi kwa kujenga viwanja vya ndege bali kwa kuheshimu
Urais ni taasisi Jomba,
Wewe tunajua kuwa ndiwe bi kidude mwenyewe unajisifia kwa majina bandia kwenye mitandao
 
Pesa ya serikali anagawa samia siku hizi. ndugai na bunge lako mnakula hela ya bure
 
Huyo Mama tajiri sana

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Samia ametoa ni pesa ake mfukoni? hizi kodi za wananchi mbaya zaidi yeye hashiriki kulipa kodi mshahara wake haukatwi kodi. Ni dharau kubwa sn kwa wananchi
Tatizo lako ukisikia jina Samia unafananisha na jina la bibi yako kule kijijini!

Jina Samia linawakilisha taasisi ya urais.

Ndio maana Masoud alipoulizwa juu ya kuchora vikatuni vya Samia, alijibu kwamba yeye anachora urais na siyo mtu.

Bavicha mna vichwa vigumu sana.
 
Mkuu sami huo uwanja kaja kukamilisha tu mradi umeanza enzi za jiwe maan ata fidia watu wamelipwa wakat wake
Mtu kwao, hadi kufikia bajeti ya mwaka 2020/2021, hakukuwa na kitu kilichoendelea, kasome utekelezaji wa mpango wa bajeti ya Wizara ya Ujenzi ukurasa wa 57 utaona mradi umeanza kufanyiwa kazi haswa mwezi Aprili mwaka huu na mama Samia ndio kamwaga pesa bilioni 35 cash ili mradi utekelezwe na kampuni kubwa kabisa ya ujenzi ya Beinjing Constructions ya China
 
Sasa hizo pesa Mwaka jana za fidia nani alitoa mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…