Rais Samia atua Afrika Kusini kushiriki uapisho wa Ramaphosa hapo kesho

Rais Samia atua Afrika Kusini kushiriki uapisho wa Ramaphosa hapo kesho

Ndege ni yetu na ndio maana Rais wetu anaitumia na ataendelea kuitumia na tunataka kuona Rais wetu mpendwa akitumia ndege zetu na siyo zile za kukodi kama alivyofanya Rais wa nchi jirani ..ndio raha ya Taifa lenye maoni kuwa na usafiri wa uhakika wa anga kama ilivyo kwetu watanzania
Ndege za magufuli walizokua wanazibezaa zinatia hasarq taifa
 
Ndugu zangu Watanzania,

Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan ametua kwa kishindo na salama kabisa Nchini Afrika kusini,ambako amekwenda kwa ajili ya kuhudhuria uapisho wa Rais wa Taifa hilo Mheshimiwa Ramaphosa utakaofanyika siku ya kesho.

Hii ni baada ya kupata ushindi wa kura takribani 283 baada ya kuungana na chama cha DA(Demoratic Alliance)zidi ya mgombea wa kutoka chama cha EFF cha Julius Malema.ikumbukwe ya kuwa safari hiyo ni ya muhimu sana kwa Rais wetu kuhudhuria,hasa kwa kuzingatia historia yetu ya kipekee kabisa na Taifa letu na Afrika kusini.

Ndio maana mnakumbuka mwaka 2013 namna Mheshimiwa Daktari Jakaya Mrisho Kikwete namna alivyoshangiliwa kwa kishindo na wa Afrika kusini wakati wa msiba wa hayati Nelson Mandela wakati akitoa historia yetu na yeye na namna Tanzania ilivyo msaidia Nelson Mandela katika masuala mbalimbali,hadi akawatania kuwa alisahau viatu vyake na alikuwa akitumia paspoti yetu.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.

PIA SOMA
- Rais Samia kwenda Afrika Kusini kwenye uapisho wa Ramaphosa

- Rais Samia kwenda Afrika Kusini kwenye uapisho wa Ramaphosa



Mkuu kadri muda unavyoenda unakuwa Mwandishi mahiri, hongera sana kwa kupokea maoni ya wadau na kuyafanyia kazi.

Usikatishwe tamaa na maneno ya watu, binadamu ndivyo tulivyo. Mkuu zingatia kufanya kila jambo kwa kiasi bila kuathiri mtazamo na msimamo wako.

Kama ni chumvi au viungo viwe kwa kiasi. Jitahidi andiko lako liwe linakuwa fupi lenye picha mnato na picha mjongeo pia kama hapo juu.

Epuka kurudia rudia jambo moja kwa maneno mengi tofauti. Jitahidi sana kuburudisha, kushawishi, kuhabarisha, kushaukisha, kukosoa, kuelimisha, kuonya na kushauri kwa kiasi.

Mkuu ni muhimu kutopambana na wanao kukosoa au kutukana maana hao ndio wanaokujenga, tafakari maneno yao, yafanyie kazi na heshimu mitizamo yao. Utakuwa bora zaidi.

Kumaliza ndugu Lucas usiwe shabiki au chawa kipitiliza maana nyakati hubadilika na tawala hupita na huja watu wapya.

Mkuu jitahidi usivunje daraja la kukuunganisha wewe muda wowote na pande zinazo letwa usukani na mabadiliko hayo pindi yatokeapo!!!

Kuna watu wanajuta sasa hivi na hawana msaada kwa sababu walichoma madaraja yao kisa mahaba!!!

Vinginevyo unakuwa vizuri!!!

⚖️4Asimwe#
 
Huyu mama apunguze safari
Unaweza kukuta kaambatana na akina Mwijaku,Steve Nyerere,Baba Levo,Shishi baby...
Ccm ni shida kuu
Mkuu hata hao ni watanzania, nao wanastahili kula keki ya Taifa, chuki dhidi ya watanganyika wenzetu ya nini.

Ndugu Nyabhingi, nguvu Rais kufanya atakavyo na apendavyo tunampa sisi wenyewe kupitia sheria wanazo tunga wabunge wetu.

Tutulie, usilalamikie!!!

⚖️4Asimwe#
 
Ni dhahiri kwamba suala la kupunguza matumizi ya rasilimali za nchi maskini kwa ajili ya safari za viongozi ni la msingi na linahitaji mkakati madhubuti. Baadhi ya mambo muhimu yanayoweza kufanyika ni:

1. Kutunga sheria na kanuni madhubuti zinazoweka mipaka na viwango vinavyoruhusiwa kwa ajili ya safari za kiofisi za viongozi. Hii itawezesha kupunguza matumizi ya fedha na rasilimali kwa ajili ya safari ambazo hazina tija ya kuongeza ufanisi wa serikali.

2. Kuwepo kwa mfumo thabiti wa uwajibikaji na uchambuzi wa thamani ya kila safari iliyofanyika. Hii itawezesha kujua ni safari gani zinazobeba tija na zinahitajika, na kuondoa zile ambazo hazina mchango mkubwa katika maendeleo ya nchi.

3. Kutumia kwa kiasi kikubwa teknolojia ya video conferencing na mikutano kupitia mtandao. Hii itapunguza mahitaji ya kusafiri kimwili, hali inayoweza kuongeza ufanisi na kupunguza gharama.

4. Kutoa mafunzo na kuweka mifumo inayohimiza uwajibikaji miongoni mwa viongozi katika matumizi ya rasilimali za umma. Hii itasaidia kubadili mtazamo na kuwajibisha viongozi kwa matumizi sahihi ya fedha za umma.

Kwa kuchukua hatua hizi, tunaweza kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ya rasilimali, na kuwezesha uelekezwaji sahihi wa rasilimali hizo katika miradi na programu zinazoweza kuimarisha maisha ya wananchi.
 
Katika kutathmini thamani na umuhimu wa kila safari ya Rais, vigezo muhimu vinavyoweza kuzingatiwa ni pamoja na:

1. Malengo na madhumuni ya safari:
- Je, safari hiyo ina lengo la kuimarisha sera, mikakati au programu za maendeleo ya nchi?
- Je, safari hiyo ina mchango katika kutatua changamoto mahsusi zinazowakabili wananchi?

2. Matokeo na tija iliyopatikana:
- Je, safari hiyo imeongeza ushirikiano na nchi/mashirika husika?
- Je, safari hiyo imewezesha kupata rasilimali, uwekezaji au ufadhili muhimu kwa ajili ya maendeleo ya nchi?
- Je, safari hiyo imeongeza uwezo, ujuzi na uzoefu wa viongozi husika?

3. Matumizi ya rasilimali:
- Je, safari hiyo imetumia rasilimali za umma (fedha, watu, muda) kwa njia ya tija na ufanisi?
- Je, kuna uwezekano wa kutumia njia nyingine za kufikia malengo hayo kwa gharama ndogo zaidi?

4. Uwazi na uwajibikaji:
- Je, kuna miripoti na taarifa za umma kuhusu safari hizo?
- Je, kuna mifumo thabiti ya uchambuzi na ukaguzi wa safari hizo?

Kwa kuzingatia vigezo hivi, itakuwa rahisi kutathmini faida halisi na tija ya kila safari ya kiofisi, na kuwezesha uamuzi sahihi kuhusu matumizi bora ya rasilimali za umma.
 
Back
Top Bottom