Rais Samia atunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu ya Usimamizi ya Utalii na Masoko ya Chuo Kikuu cha Zanzibar (SUZA), leo Desemba 28, 2023

Rais Samia atunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu ya Usimamizi ya Utalii na Masoko ya Chuo Kikuu cha Zanzibar (SUZA), leo Desemba 28, 2023

Ni vyema Rais Samia ungetumia mda mwingi kwenda kuonana na Wapiga kura au kutembelea Maeneo yenye Changamoto kuliko kuhudhuria hafla kama hizo ambazo hazina maana yeyote kwako na Kwa Wananchi.

Pia hayo Mashahada hayajuongezei Tija yeyote Kisiasa badala yake inaonekana unapenda sifa kuliko kufuatilia mambo muhimu.

Ushauri wangu ni vyema ukayapotezea ma hafla yasiyo na Tija Kwako na Kwa Wananchi.

View: https://www.youtube.com/live/dxWYcQ28mrI?si=t3WmJMkDA1brPerd
 
Rais wangu Samia Unaweza ongea Kauli kama hii ukidhani kwamba unaongea jambo zuri na utani ila ukae ukijua kwamba inaondoa Imani Kwa Serikali Kwa chochote ambacho mtakuwa mnaongea au kuwaambia watu.

View: https://www.youtube.com/live/VfjzZ74qGmw?si=UfAP9njAhRl9hbc3

My Take
Kwa staili hii mliochanja mna nini Cha kutushauri ambao hatukuchanja na tunadunda?
 
Hili ni kosa la kiufundi.Kauli ya sebuleni(siri) imeletwa barazani.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akitunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu ya Usimamizi ya Utalii na Masoko ya Chuo Kikuu cha Zanzibar (SUZA) leo tarehe 28 Desemba, 2023, Zanzibar.


View: https://www.youtube.com/live/3ojgVNt8bpA?si=ipW9NnuOK_nJzT1c

View attachment 2855459
Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Viongozi pamoja na wageni mbalimbali mara baada ya kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) kwa kutambua mchango wake wa kuifungua nchi kiuchumi kupitia Sekta ya Utalii

View attachment 2855460Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Rais Mstaafu wa Zanzibar Mhe. Dkt. Aman Abeid Karume katika Ukumbi wa Dkt. Ali Mohamed Shein Kampasi ya Tunguu walipohudhuria Hafla ya Mahafali ya 19 ya Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) tarehe 28 Desemba, 2023.

View attachment 2855461Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, akitunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa kutambua mchango wake wa kuifungua nchi kiuchumi kupitia Sekta ya Utalii wakati wa Mahafali ya 19 ya Chuo hicho yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Dkt. Ali Mohamed Shein Kampasi ya Tunguu tarehe 28 Desemba, 2023.

Zinagawiwa tu bila kufuata vigezo vya kusomea falsafa za taaluma husika, kufanya utafiti unaotatua changamoto katika jamii au kukuza uchumi usio tegemezi kwa misaada. Ajabu sana awamu hii
 
Chagua kwa umakini na uangalifu mkubwa 2025.

Kumbuka, mbali na Halima Mdee au Chacha Wangwe CHADEMA bado hawana Kiongozi aliye na dhamira wala uwezo wa kuendesha serikali.
 
Back
Top Bottom