Rais Samia Aufunga Mkoa Wa Tanga Kwa Muda .Watu Wafurika Mkutanoni hata sisiminzi hawezi kupata mahali pa kupitisha Mguu Wake..

Naona pesa za wauza unga, za waliopewa bandari, na mbuga zetu safari hii zinatumika kusafirisha watu bure kwa mabus, na malory ili kuhadaa umma kuwa bi mkojani anakubalika sana.


Hiyo nilishuhudia alivyoenda Ruvuma, watu walipelekewa magari wilaya na vijiji vyote ili wakajae Songea mjini. Watumishi, hasa walimu, ilikuwa ni vilio, waliambiwa kuwa ambaye hataenda atatakiwa kujieleza kwanini asifukuzwe kazi kwa kukosa kuhudhuria mkutano wa Samia, wakati walipelekewa usafiri..

Safari yake huko iliongeza chuki kutokana na watu kulazimishwa kuacha kazi zao ili wakahudhurie mkutano ambao hauna faida yoyote kwao.

Bila shaka hata huko Tanga kutakuwa na wengi waliolazimishwa.

Unafanyika uharamia mwingi katika maigizo ya kutaka kuwahadaa watu kuwa anapendwa sana.
 
Naona pesa za wauza unga, za waliopewa bandari, na mbuga zetu safari hii zinatumika kusafirisha watu bure kwa mabus, na malory ili kuhadaa umma kuwa bi mkojani anakubalika sana.

Naambiwa walimwahidi kuwa watagharamia kampeni yake yote.

Peza yao ya kwanza ilinunua pikipiki zilizosambazwa nchi nzima.

Kwa mara ya kwanza tumempata kiongozi muuza nchi:

Bandari zetu kawauzia waarabu.

Mbuga zetu za wanyama kawauzia waarabu.

Hifadhi zetu za misitu, kawauzia waarabu.

Airport yetu ya KIA kawauzia waarabu.

Lakini machawa punguani, kwa usaliti uliovuka viwango vyote Duniani, wanashangilia wakati kuna uharamia mkubwa unafanywa dhidi ya Taifa lao!!
 
Mabus ya Ratco yamefanya sana kazi ya kusomba watu ili kupata nyomi fake.
 
Uongo tu ndio kazi mmekalia kwa sasa baada ya kuona namna anavyokubalika na kupendwa na watanzania kuwahi kutokea. Mara ya kwanza mlikuwa mnasema hawezi kupata watu wa kuhudhuria lakini saizi baada ya kuona mafuriko ya watu wakimiminika kwenye mikutano yake mmeanza ngonjera na porojo zingine
 
You are absolutely right.
 
Rais wa Tanzania hawezi kukosa mafuriko maana yanatengenezwa kwa nguvu za dola.
 

Unahamgaika kwa kuandika upuuzi!!

Hivi watu kujaa kwenye mkutano wa Rais ambapo watu wanasombwa kwa gharama za Serikali, ni jambo la ajabu?

Ebu niambie, ni Rais gani wa Tanzania ambaye aliwahi kufanya mkutano akakosa watu.

Nikiwa chipukizi, Hayati Mwinyi akiwa Rais, tulisafirishwa na kugharamiwa kila kitu, tena tuliwahishwa siku 5 kabla ya ujio wa Rais. Tulisafirishwa toka wilayani mpaka mkoani, karibia kilometa 290. Kama watu mnasafirishwa kilometa nyingi kiasi hicho, mkutano wa Rais utakosaje watu?

Hata kama mtu una poor reasoning, haitegemewi ushindwi kuelewa hata mambo madogo kama haya.


Ni rahisi zaidi kuwapata watu wachache kwenye mkutano wa Rais anayependwa na raia wake kuliko Rais diktetaanayechukiwa na wananchi wake.

Fuatilia siasa na uongozi wa Stallin, ndiyo utaelewa.
 
Watu wanahudhuria kwa hiyari yao wenyewe bila shuruti. Kwani wewe na akili zako Timamu unaweza kusafirishwa kama mfungwa au mateka bila hiyari au ridhaa yako mwenyewe?
 
Upumbavu huu utaona kwa mtu mweusi.
 
Kwa uzoefu wangu. 100% ya watu waliojaa hapo ni watumishi wa serikali tena an daftari la mahudhurio limehamishiwa hapo. 🤣🤣
 
Kwa uzoefu wangu. 100% ya watu waliojaa hapo ni watumishi wa serikali tena an daftari la mahudhurio limehamishiwa hapo. 🤣🤣
Watumishi wa serikali wapo wangapi mkoa wa Tanga? Na hapo unaona watu wapo kiasi gani? Uwanja wa Mkwakwani Tanga unabeba watu wangapi? Je huoni uwanja umejaa ndani hadi nje na hapo bado wengine wanafuatilia kupitia vyombo vya habari?
 
watumishi wote wanalazimishwa iwe mwenge au kiongozi wa ccm. Na istoshe na attendance register inapelekwa eneo la mkutano. Siku hizi utumishi wa umma ni upumbafu kabisa. Hapo Tanga vikosi vya Jeshi kama 37KJ, Mgambo na SUKUA hapo Kange wange wote wameamliwa kwenda.


Siku hizi ni matatizo tupu. Watumishi na wanafunzi ndio kimbilio la ccm. Hiyo ina reflect kwenye dafyari la wapiga kura, waliojiandikisha ni wachache sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…