Rais Samia autengua uteuzi wa Mkurugenzi mpya wa TPDC. Amrejesha Mataragio

Rais Samia autengua uteuzi wa Mkurugenzi mpya wa TPDC. Amrejesha Mataragio

Kwa hiyo alivyoletewa tu akamwaga wino bila kijiridhisha hadi wanajamii forums wamepiga kelele ndo kastuka!?

We unauhakika gani kama anasomo upuuzi uliomo humu kamtengua kwa sababu zake anazijua mwenyewe wala usivimbe macho kwa madai eti kasoma madai ya watu wa jf.
 
Raisi wa Jamhuri ya Muungano kufanya jambo la maana kumuacha Mataragio
 
Panga pangua, labda huyu anajua kula na vigogo wenzake. I can’t believe kila siku tunaapishana what a joke! Panga pangua wakati wa maombolezo huo ni uafrika kweli? She was part of the leadership, so she never okd JPMs appointments? They couldn’t wait 21 days???
 
  • Thanks
Reactions: mmh
TPDC.jpg


Jana Rais Samia Suluhu alimteua Thobias Mwesiga Richard kuwa Mkurugenzi mkuu wa shirika la maendeleo ya petroli nchini (TPDC). Hii ilikua imani kubwa sana kwa vijana kupewa nafasi kubwa kama hiyo.

Thobias kijana wa miaka 34 ni kada wa CCM na mwaka 2017 aligombea uenyekiti wa UVCCM akaangushwa na Heri James. Mwaka 2020 alitia nia ya ubunge huko Nkenge lakini akaangushwa kwenye kura za maoni.

Wakati Thobias na MATAGA wenzie wakishangilia, leo Mama samia katengua uteuzi wake. Kafurushwa TPDC. Yani leo ni siku mbaya sana kwa vijana wa MATAGA.
Kama mnakumbuka mama Samia wakati akiwaapisha mawaziri alisema atakua anaangalia rekodi katika teuzi anazofanya. Na akasema jicho macho yake yamelegea lakini yanaona. Kwahiyo kila mtu rekodi yake itamfuata.

Bila shaka Mama Samia ameangalia rekodi na kukuta Thobias ni moja ya vijana waliowahi kutuhumiwa kuhusika na magenge ya kuteka na kutesa watu. Tarehe 20 January mwaka 2019, aliyekua Mbunge wa Kigoma mjini Zitto Kabwe alitishiwa kuuawa na Thobias.

Akapeleka malalamiko kwa Spika kwamba usalama wake upo mashakani lakini akapuuzwa. Akaenda kuripoti polisi lakini Polisi hata hawakumkamata wala kumhoji Thobias. Baadae Zitto akaamua kuweka wazi taarifa za kijana huyo mtandaoni kwa ajili ya usalama wake.

Zitto akasema Thobias ni afisa wa TISS na amekua akitumia nafasi hiyo kutisha, kuteka na kutesa watu hasa wanaoikosoa serikali. TISS hawakutoa tamko lolote la kupinga au kukubali kama Thobias ni afisa wao. Lakini wakurya husema silence means YES.

Jana Thobias kapewa heshima kubwa sana ya kuongoza shirika kubwa la TPDC. Shirika linaloshughulikia masuala yote ya mafuta na gesi nchini. Lakini rekodi yake imemmaliza mwenyewe, akaishia kufurushwa kabla hata jogoo hajawika.

Hii iwe fundisho kwa MATAGA na vijana wengine wanaotumia nafasi zao kunyanyasa, kudhulumu au kutesa wengine ili waonekane wanaitetea serikali. Zama zimebadilika. Mama hataki huo upuuzi.

Hata wale maDC na maRC mliotumia nafasi zenu kuumiza wengine jiandaeni kisaikolojia. Soon mtanyolewa kama Thobias, maana mama amesema anaangalia rekodi.
 
Kwa hili mama anaonekana ni kivuli kuna wanaume wa shoka wapo nyuma yake wanamuongoza, since day one anaapa mama alionesha wazi viatu vya uraisi ni vikubwa kwake...

Mama hawezi fanya maamuzi ona sasa anaabika kisa teuzi ndogo ndogo kama hizi...

Halafu teuzi nyingi za mama ni za kimehumko na kimajungu zaidi..

Msoga.com
 
Bado yule wa TRA amfute haraka maana ana tuhuma nyingi za wizi hata kama ni mchapakazi
 
Sasa bada mifuko ya kijamii kwani watu wanaodai mafao yao wanaonekana watumwa michango yao .
Wakati ni haki yao
Hawa watu wa Mifuko ile wanajiona Sana. Pesa yetu utadhani tunaomba mikopo wakati ni haki yetu. Njoo kesho hadi sasa imefikis miaka minne watu wanasotea malipo yao. Fikiria mstaafu anayetoka Kagera kwenda Dodoma kufuatilia malipo halafu anaambiwa arudi mwezi ujao, hii ni haki kweli?
 
Hii inaonyesha Rais wetu si mtoa maamuzi,kuna mtu yuko nyuma ya pazia anapanga na kumwambia afanye,sasa mama akienda kulala na first gentlemen akigombezwa akiambiwa amechemka,Akiamka asubuhi kesho yake chakwanza ndio Kutengua kama alivyofanya hapo sasa.

huyu alierudishwa ndio selection ya mama,ila yule aliewekwa alikua kapangwa na wapangaji,Nchi sasa ina marais wawili (seen & unseen) kisha ndio VP.

kwasasa huku mtaani kwangu watu wana imani na VICE PRESIDENT kwa 90% ila imani kwa MAMA ipo 41% tu,kulingana na mtaa wangu.

Kama ni kweli uliosema juu ya hizo asilimia basi wapuuzi mko wengi hapo huyo makamu wa Raisi alipochaguliwa na MAMA pale bungeni machozi yalimtoka hakutarajia kama MAMA angemchagua yeye
Na hiyo inaonyesha umakini wa MAMA katika kuchagua kufuatana na akili yako alie chaguliwa mnapa asilimia 90 aliemchagua mnampa asilimia 41 hapo pana afya mbaya ya akili
 
Hahahaha mkuu Ritz heshima yako.
Mkuu Lusungo nimeamini Tanzania kila kitu kinawezekana. Umeona elimu na CV ya huyu ''muungwana'' aliyeteuliwa na kutumbuliwa? Alipitapitaje ngazi ya uteuzi? Naamini kuna viongozi ambao uwezo wao ni mdogo sana sana. Haya mambo rais Samia akitaka yakome inahitajika katiba mpya haraka iwezekanavyo. Nafasi za uteuzi kama hizi zipitishwe na Bunge kwa kushindanisha watu wenye sifa. Lakini kwanza....... Bunge lenyewe lipatikane kwa demokrasia na utaalam ili wabunge wawe watu wenye uwezo kichwani. Bunge likiachwa liwe la akina Jah People na Babu Tale bado hata majina yakienda bungeni haitasaidia. Halafu ni muhimu sana ''system'' i-encourage bunge liwe na mchanganyika wa vyama. Hili la kufosi wabunge watoke chama kimoja linaturudisha nyuma.
 
Asante kwa taarifa,namshauri Mh SSH atulie kwanza maana anavyofanya anaweza akajitengua hadi yeye.
Mkuu umenikumbusha Mzee wa Pwani aliwahi kusema" Kipindi cha baridi ndege hunyonyoa manyoya yake ili kuwafunika kinda wake kwenye kiota. Lakini ndege yule asipokuwa makini anaweza kujinyonyoa sana hadi akashindwa kuruka kwenda kutafuta chakula chake na kinda wake. Akafa yeye na kinda wake kwa njaa".

Mzee wa Pwani natumaini atamshauri Mama.
 
[emoji3][emoji3][emoji3] Ile CV ilikuwa nyeupe ka unyoya wa kunguru aisee, Mara degree chuo Cha Yohana, hata huko udom, itakuwa alibebwa tu. Aliyefanya uhuni kupenyeza Hilo jina kumharibia Raisi afukuzwe aisee

[emoji28][emoji28]kwakweli aliemfanyia hivi mama samia afukuzwe kamchezea sana nahisi hata yeye alipopitia hio cv alishangaa
Hawa washauri wake wanataka kumfanya mama aonekane hayupo makini
But naamini haitotokea tena.She is smart and she can do it,bado ameanza vizuri [emoji1376]
 
Adui wa mwanamke ni mwanamke mwenzake. Hongera Rosemarie kwa kuthibitisha hilo.

Mwanamke kiumbe dhaifu peke yako usiejiamini usijumuishe wote.

Nikupe mfano tu: Ellen Johnson Sirleaf, Mwele Malecela, Msuya wa UNEP...
Huyo ni pimbi tu kwani anataka kutuaminisha tangu azaliwe hajawahi kuona mwanaume kakosea. Yani anaemkosoa mtu kwa jinsi yake huwa namuona mshamba tu.

Chapa kazi mh mama SSH.
 
Panga pangua, labda huyu anajua kula na vigogo wenzake. I can’t believe kila siku tunaapishana what a joke! Panga pangua wakati wa maombolezo huo ni uafrika kweli? She was part of the leadership, so she never okd JPMs appointments? They couldn’t wait 21 days???

Hata yeye ilibidi aape kabla hata mazishi
Kweli tuko kwenye msiba lakini shughuli za serikali lazima ziendelee
Hata alipofariki balozi Mahiga aliteuliwa waziri Mwigulu ili system iendelee na kazi

Mungu ibariki Tanzania Mungu mbariki rais wetu Samia Suluhu Hassan na wasaidizi wake wote 😍🇹🇿🙏

Rest well our hero President John Pombe Joseph Magufuli 🕊
 
Back
Top Bottom