Rais Samia avunja Bodi ya TRC, atengua uteuzi wa Wakala wa Ndege za Serikali. Aagiza wabadhirifu washughulikiwe

Rais Samia avunja Bodi ya TRC, atengua uteuzi wa Wakala wa Ndege za Serikali. Aagiza wabadhirifu washughulikiwe

Kwa hiyo hao viongozi wa mashirika wana wajibishwa na nani? Kama wao wameelekezwa wawachukulie hatua wa chini yao….wao wana wajibishwa na nani? Katibu kiongozi? Rais hana imani na CAG? Hahahaha kwanini asiwachukulie hatua za kuwwaweka pembeni watu ambao wako kwenye mamlaka yake? Kwanini ana kwepa majukumu yake? CAG amesema uongo?

kama nimeelewa vibaya utanisahihisha
Ina Maana Makatibu wakuu+Wakurugenzi waisome report na kuifanyia kazi!
Ina Maana Kama kuna Makosa/Mapungufu ambayo yanefanya say na Afisa A,Au Meneja fulani,Afisa fulani,Mkuu wa Idara,Mhasibu,Engineer,Afisa ugavi,Mwanasheria,nk nk
hao wakuu waliotajwa wamepewa Rungu wamuwajibishe!
Kwani Kuna Makosa hapo?
Nisahihishe kama Nitakuwa nimekosea kiutendaji!(Protocol)
Instead ya Kuwawajibisha Mawaziri/Makatibu wakuu au wakurugenzi.
Wewe Una mawazo gani na Kwa nini?
Nadhani Kama ulivyosema wakuu hao wa Mashirika Labda hawahusiki moja kwa moja na Utendaji!…Labda kuna wa Chini anaanzisha yeye Anaidhinisha…
sasa Anatafutwa alieanzisha? Kuomba manunuzi fulani Au Sijui nisemeje bt nadhani
Kila kitu kinawnzia chini kwenda Juu!
Kuna Uwajibikaji kwa nafasi hata kama hujatenda(Yaani Kiongozi,Na Kuwajibika kiutendaji…Alietenda say Afisa A.
nisahihishe Mkuu kama nimekosea
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amevunja Bodi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC).

Aidha, Rais Samia ametengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA), Mhandisi John Nzulule.

Katika hatua nyingine, Mhe. Rais amemuelekeza Katibu Mkuu Kiongozi kuhakikisha kuwa Makatibu Wakuu na Watendaji Wakuu wote wa Taasisi za Serikali wanaipitia kwa kina tarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kujibu na kuzifanyia kazi kwa haraka hoja zote zinazogusa maeneo yao.

Vile vile, Mhe. Rais ameelekeza kuwa watendaji wote watakaobainika kuhusika na uzembe au ubadhirifu wachukuliwe hatua za kisheria.

View attachment 2582469
NHIF na hasara ya zaidi ya Bilioni 204 ndani ya mwaka mmoja tu, Mbona bodi haijahuswa? Mama kazi imekuwa ngumu.
 
Inashangaza sana, kwanini Rais anawaagiza makatibu wakuu na watendaji wakuu wahakikishe wanapitia ripoti na kuwawajibisha wale waliohusika na uzembe?

Yeye kama Rais anachukua hatua gani kwa hao wakuu waliosimamia huo uzembe wakiwemo mawaziri? Kama yupo serious angetakiwa kuwaita mawaziri awaulize, wakati huo wizi ukitokea kwenye wizara zao walikuwa wapi? asiporidhishwa na majibu fukuza.

Haiingii akilini, hawa ambao inawezekana wameshirikiana kwenye wizi, unaagiza wachunguzane, huku ni kudanganyana tu, ndio maana kuna wakati Rais nae anatiliwa shaka.

Alichokifanya Rais hapo ni sawa na kufunika kombe mwanaharamu apite, kuhangaika na dagaa huku mapapa wapo tu ofisini, mimi sioni jipya, kapanua magoli tu hao jamaa wapate visingizio.
Sasa hizi si ndio hatua zenyewe! Sio lazima ziwe zile kichwa chako kinatamani
 
Ningetamani siku ripot ya CAG Inasomwa nchi nzima akae isikilize wote wajue nanii wanao kwamisha maendeleo.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amevunja Bodi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC).

Aidha, Rais Samia ametengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA), Mhandisi John Nzulule.

Katika hatua nyingine, Mhe. Rais amemuelekeza Katibu Mkuu Kiongozi kuhakikisha kuwa Makatibu Wakuu na Watendaji Wakuu wote wa Taasisi za Serikali wanaipitia kwa kina tarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kujibu na kuzifanyia kazi kwa haraka hoja zote zinazogusa maeneo yao.

Vile vile, Mhe. Rais ameelekeza kuwa watendaji wote watakaobainika kuhusika na uzembe au ubadhirifu wachukuliwe hatua za kisheria.

View attachment 2582469

Mh. Rais wetu yuko makini sana.. Naona kaanza na Bodi ya TRC na Wakala wa Ndege za Serikali.

Asante sana Mama yetu, Rais wetu, hakika unafanya kazi bora sana kwa nchi yetu, Mungu akubariki sana. Mh. Rais kaagiza wabadhirifu wote washughulikiwe tena kwa haraka kabisa, Mwenyezi Mungu mlinde sana Rais wetu, amen..
 
Inashangaza sana, kwanini Rais anawaagiza makatibu wakuu na watendaji wakuu wahakikishe wanapitia ripoti na kuwawajibisha wale waliohusika na uzembe?

Yeye kama Rais anachukua hatua gani kwa hao wakuu waliosimamia huo uzembe wakiwemo mawaziri? Kama yupo serious angetakiwa kuwaita mawaziri awaulize, wakati huo wizi ukitokea kwenye wizara zao walikuwa wapi? asiporidhishwa na majibu fukuza.

Haiingii akilini, hawa ambao inawezekana wameshirikiana kwenye wizi, unaagiza wachunguzane, huku ni kudanganyana tu, ndio maana kuna wakati Rais nae anatiliwa shaka.

Alichokifanya Rais hapo ni sawa na kufunika kombe mwanaharamu apite, kuhangaika na dagaa huku mapapa wapo tu ofisini, mimi sioni jipya, kapanua magoli tu hao jamaa wapate visingizio.
Hujui governance
 
Kwani hizi anazochukua sio hatua? Kumbuka Rais Huwa hana mihemko na hataki kumuonea mtu.

Ukweli ukibainika wote wataondoka.
Hujaelewa alichokiandika?

What if aliowatuma nao wanahusika?

Wakachunguze nini tena wakati inaeleweka na yeye ndio msemaji wa mwisho?

Nyie kazaneni mihemko sijui kuonea watu wakati Taifa linaangamia
 
Vipi kwa hao wakuu waliosimamia huo uzembe na ubadhirifu, mamlaka yao ya uteuzi na nidhamu ni nani?

Hivi unategemea hao wakuu watakuwa tayari kuwatoa sadaka wasaidizi wao watakaobainika kufanya uzembe?

Sababu kwa akili ya kawaida tu, kama wasaidizi wakibainika kusababisha uzembe, swali litakuja, je, wakuu wao walikuwa wapi hadi huo uzembe kutokea?

Alichofanya Rais hapa ni muendelezo wa kulindana, sioni jipya; wakuu watawalinda wasaidizi wao waliofanya uzembe, kama ambavyo Rais nae anawalinda wakuu wao waliosimamia uzembe, mwishowe mbwa mwitu wataendelea kututafuna kila siku.

Acha ujuaji wee kijana, you are talking nosense. Mh. Rais akichukua hatua anajua sbb za msingi, acha kupiga makelele kama uko bar..
 
Halafu watanzania jamani tuache au tupunguze huku kusifusifu yaani hata kama ndio sehemu yako ya kula duh yaani imekuwa too much.
 
Vipi kwa hao wakuu waliosimamia huo uzembe na ubadhirifu, mamlaka yao ya uteuzi na nidhamu ni nani?

Hivi unategemea hao wakuu watakuwa tayari kuwatoa sadaka wasaidizi wao watakaobainika kufanya uzembe?

Sababu kwa akili ya kawaida tu, kama wasaidizi wakibainika kusababisha uzembe, swali litakuja, je, wakuu wao walikuwa wapi hadi huo uzembe kutokea?

Alichofanya Rais hapa ni muendelezo wa kulindana, sioni jipya; wakuu watawalinda wasaidizi wao waliofanya uzembe, kama ambavyo Rais nae anawalinda wakuu wao waliosimamia uzembe, mwishowe mbwa mwitu wataendelea kututafuna kila siku.

Acha kiherehere i told you..
 
Vipi kwa hao wakuu waliosimamia huo uzembe na ubadhirifu, mamlaka yao ya uteuzi na nidhamu ni nani?

Hivi unategemea hao wakuu watakuwa tayari kuwatoa sadaka wasaidizi wao watakaobainika kufanya uzembe?

Sababu kwa akili ya kawaida tu, kama wasaidizi wakibainika kusababisha uzembe, swali litakuja, je, wakuu wao walikuwa wapi hadi huo uzembe kutokea?

Alichofanya Rais hapa ni muendelezo wa kulindana, sioni jipya; wakuu watawalinda wasaidizi wao waliofanya uzembe, kama ambavyo Rais nae anawalinda wakuu wao waliosimamia uzembe, mwishowe mbwa mwitu wataendelea kututafuna kila siku.
Msifikiri kudukuza serikali ni rahisi rahisi hivyo kuna sheria na taratibu na kama rais amejinasibu ni muumini wa utawala bora basi hana budi kuzifuata.
 
Inashangaza sana, kwanini Rais anawaagiza makatibu wakuu na watendaji wakuu wahakikishe wanapitia ripoti na kuwawajibisha wale waliohusika na uzembe?

Yeye kama Rais anachukua hatua gani kwa hao wakuu waliosimamia huo uzembe wakiwemo mawaziri? Kama yupo serious angetakiwa kuwaita mawaziri awaulize, wakati huo wizi ukitokea kwenye wizara zao walikuwa wapi? asiporidhishwa na majibu fukuza.

Haiingii akilini, hawa ambao inawezekana wameshirikiana kwenye wizi, unaagiza wachunguzane, huku ni kudanganyana tu, ndio maana kuna wakati Rais nae anatiliwa shaka.

Alichokifanya Rais hapo ni sawa na kufunika kombe mwanaharamu apite, kuhangaika na dagaa huku mapapa wapo tu ofisini, mimi sioni jipya, kapanua magoli tu hao jamaa wapate visingizio.
Msifikiri kudukuza serikali ni rahisi rahisi hivyo kuna sheria na taratibu na kama rais amejinasibu ni muumini wa utawala bora basi hana budi kuzifuata.
 
Wanaotakiwa kushuhulikia wabadhirifu wenyewe ndio hivyo tena.

Maskini mama kashaaharibu boxing day ya pasaka
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amevunja Bodi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC).

Aidha, Rais Samia ametengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA), Mhandisi John Nzulule.

Katika hatua nyingine, Mhe. Rais amemuelekeza Katibu Mkuu Kiongozi kuhakikisha kuwa Makatibu Wakuu na Watendaji Wakuu wote wa Taasisi za Serikali wanaipitia kwa kina tarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kujibu na kuzifanyia kazi kwa haraka hoja zote zinazogusa maeneo yao.

Vile vile, Mhe. Rais ameelekeza kuwa watendaji wote watakaobainika kuhusika na uzembe au ubadhirifu wachukuliwe hatua za kisheria.

View attachment 2582469
kweli Mama yuko kazini
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amevunja Bodi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC).

Aidha, Rais Samia ametengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA), Mhandisi John Nzulule.

Katika hatua nyingine, Mhe. Rais amemuelekeza Katibu Mkuu Kiongozi kuhakikisha kuwa Makatibu Wakuu na Watendaji Wakuu wote wa Taasisi za Serikali wanaipitia kwa kina tarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kujibu na kuzifanyia kazi kwa haraka hoja zote zinazogusa maeneo yao.

Vile vile, Mhe. Rais ameelekeza kuwa watendaji wote watakaobainika kuhusika na uzembe au ubadhirifu wachukuliwe hatua za kisheria.

View attachment 2582469
Maagizo si vitendo,tunataka watu wote walioliingizia Taifa hasara wafanyiwe yafuatayo:
1.Wasimamishwe kazi.
2.Wachunguzwe,na ikithibishwa kwamba wameingizia Serikali hasara,wafukuzwe kazi.
3.Wafirisiwe mali walizozipata kwa kuiibia Serikali.

Short of that,Samia bado atakuwa hajafanya kitu.Tunataka Rais anayeuma,mpaka sasa bado.
 
Hii ni sinema tu ya ‘Bi Tozo’ kukimbia wajibu wake wa kuchukua hatua.

Jukumu la kuzuia fraud ndani ya shirika ni MD na senior team, sio auditor yeye anatoa tu taarifa.

Sasa CAG anaposema kuna fraud (jitihada za makusudi kuiba) mfano manunuzi hayana receipt, matumizi hayana ledger entry maana yake hela imetoka bank bila ya kueleweka imeenda wapi rasmi, falsification of documents na mambo mengine ya ovyo ya wizi.

☝️Hizo sio unintentional errors zinazohitaji maelezo ni fraud (wizi) nchi ina sheria ya fraud; hilo tena sio swala la kujadiliana na management ni swala la polisi au sijui TAKUKURU majizi husika yakamatwe na kutupwa lupango kabla ya hapo yatapike hizo hela.

Sio hizi porojo za sijui katibu mkuu asome report na kuchukua hatua. Hapo anatakiwa kamanda wa polisi au TAKUKURU kuhusika sio hadithi za siasa na uzembe wa kuchukua hatua.
 
Back
Top Bottom