Rais Samia: Awamu ya 5 heshima iliyokuzwa ni ya uoga kwa sababu kulikuwa na Simba wa Yuda, ukimgusa sharubu anakurarua, hatukukua kivile

Nakwambia huyu bibi anaropokaga tu, yuko hapo ili amfunike Magufuli aonekane yeye ni bora lakini muda ni mwalimu mzuri.
... mbona kwa mwaka mmoja tu madarakani ameshamzidi jamaa aliyetawala 5+ yrs? Ubabe haujawahi kuwa mojawapo ya sifa za kiongozi bora.
 

Ndio maana nimekuambia uache kujitoa akili, wewe aidha hujui unachoongea ama unaleta ujuaji tu.

Ivi unafahamu kasumba za watumishi kabla ya Magu.
Hii ichi ili hitaji mtu mkali iliafanye adjustiment za nidhamu kwa watumishi, hali ikikuwa mbaya.

Africa tunatakiwa kuwa na style yetu ya kuongozana kulingana na mazingirayetu.

Watu hawafanyi kazi kwa bidii wanapenda mishahara kuliko kile kinacho wafanya wapate hiyo mishahara.
Kifupi hawaheshimu kazizao.

Kama hujatembea nje ya bara hili ndio hutaelewa ninacho maanisha kuhusu nidhamu za kazi.
 
Ni ukweli mtupu ilikuwa nihofu tupu tulikuwa tunaogopana wenyewe kwa wenyewe
 
... uko sahihi. Kuna wajinga wanalazimisha bango aliloacha Magufuli lisomwe upande mmoja tu; hawataki kabisa upande wa pili wa bango lake uonekane. That's very wrong!
 
Kabisa mpaka nimeanza kuogopa.
Kipindi kile kulitokea tetesi Samia alitaka kujiuzulu makamu wa rais nimeanza kuamini.
waliopo karibu na Samia wamshauri.
Magufuli bado ana wafuasi wake watiifu haileti picha nzuri katika taifa linalopigana KUJIPONYA.
... taifa linapigana kujiponya na nini?
 
Kwa hii Kauli Yake basi Kila kwezi Atakuwa Anabadiri Mawaziri hadi waishe sasa.

Tanzania Sijui Lini tutakuja Kupata mkuu wa Nchi mwenye akili.
 
Wakati magufuli anatoa maumivu na vilio kwa watu ulikuwa haupo?
... alichofanya Rais ni sehemu ya dozi; tuache kuficha ukweli jamaa alikuwa katili. Ukweli utatuweka huru; Samia amesema sehemu ya ukweli uliofichwa.
 
alafu akitoka kumnanga mzee wa watu aliye lala usingizi wa milele anawakusanya wanafki ma CCM menzake waliokuwa wanachekelea mipasho yake, wanakwenda chatto kumjulia hali mjane, sijui watajisikiaje pale mjane akiwafukuza
 
DOZI kuua wenzio?
... alichofanya Rais ni sehemu ya dozi; tuache kuficha ukweli jamaa alikuwa katili. Ukweli utatuweka huru; Samia amesema sehemu ya ukweli uliofichwa.
 
Hiyohiyo nidhamu ya uoga ndio ilikua inafanya tunapata huduma vzr na haraka kuliko sasa hivi, ile kufanya kazi kwa mazoea imerudi tena wateja wa huduma tunapuuzwa 😟
 
Huyu ni ndumilakuwili,mbona aku step down

Tuseme tu ukweli umejaribu kwenda kwenye taasisi za serikali ukaona huduma zao zikoje ukifananisha na simba wa chato huduma ilikuaje.
Najaribu kuwaza tu hivi polisi aliyeogopa rushwa wakati wa Magufuli akisikia hiyo kauli ya Samia atachukua hatua gani? Na daktari aliyetibu bila rushwa wakati ule ataanza tabia gani akimsikia Samia?
 
Mpaka Sasa mama anaupiga mwingi mpaka nje ya uwanja

Na refa anasema tuendelee

Kwa mbali mashabiki wanasema mechi imeuzwaa

Muhindi wa kampuni fulani ka fix match
 
Huyu mama anataka uwachekee watumishi wa umma.

Heshima ya moyoni hiyo haipewe serikalini, hiyo inatolewa nyumbani.

Huyu mama ni kimeo.
Juzi ametoa bei elekezi ya bidhaa, leo anaturidisha kwenye kutokujali na utovu wa huduma sekta ya umma.

Vv
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…