Rais Samia: Awamu ya 5 heshima iliyokuzwa ni ya uoga kwa sababu kulikuwa na Simba wa Yuda, ukimgusa sharubu anakurarua, hatukukua kivile

Rais Samia: Awamu ya 5 heshima iliyokuzwa ni ya uoga kwa sababu kulikuwa na Simba wa Yuda, ukimgusa sharubu anakurarua, hatukukua kivile

Rais anakosea sana kuponda mazuri ambayo alipaswa kuyaenzi
 
Sahihi kabisa
Kabisa mpaka nimeanza kuogopa.
Kipindi kile kulitokea tetesi Samia alitaka kujiuzulu makamu wa rais nimeanza kuamini.
waliopo karibu na Samia wamshauri.
Magufuli bado ana wafuasi wake watiifu haileti picha nzuri katika taifa linalopigana KUJIPONYA.
 
naona awamu ya 6 watu wananidhamu hadi kutaka uIGP kibabe...
 
Kwa kweli tukisema muacheni Mh Hayati Magufuli apumzike mahali aliko tunashambuliwa eti sisi ni sukuma geg! Jaman marehemu kwa heshima za Afrika huwa tunamwacha apumzike aliko kuliko kumsemea vibaya vibaya.

Leo nimesikia Mh Raisi akisema utawala wa awamu ya Tano ulitengeneza nidhamu ya uwoga kwa watumishi, kwa sababu ulikuwa ni Simba, alikuwa ukizingua anakungata ngwadu!

Sasa kwa Nini ustekeleze unavyotaka. Paspo kumsem mwenda zake?
Hata yeye alikuwa anamuogopa sana tu.ukweli Mama hajiamini bado kama ni Rais.

Sent from my SM-J260F using JamiiForums mobile app
 
Ndio maana nimekuambia uache kujitoa akili, wewe aidha hujui unachoongea ama unaleta ujuaji tu.

Ivi unafahamu kasumba za watumishi kabla ya Magu.
Hii ichi ili hitaji mtu mkali iliafanye adjustiment za nidhamu kwa watumishi, hali ikikuwa mbaya.

Africa tunatakiwa kuwa na style yetu ya kuongozana kulingana na mazingirayetu.

Watu hawafanyi kazi kwa bidii wanapenda mishahara kuliko kile kinacho wafanya wapate hiyo mishahara.
Kifupi hawaheshimu kazizao.

Kama hujatembea nje ya bara hili ndio hutaelewa ninacho maanisha kuhusu nidhamu za kazi.
Mkuu,una hasira kama unaumwa nonda.Itoshe kukueleza nimekuchoka.
 
Nadhani nimeeleweka vizuri.
Kwani huwa hazipitiwi kabla ya kuwasilishwa, maana Simba wa burigi tulikuwa tunajua anaongea bila kusoma sehemu nyingine '' Anapuyanga vibaya sana'
Sasa sijui kuhusu chief.
 
Bora nidhamu ya uoga na utendaji usiokatakata umeme kipumbavu,hii kuwakosea watanzania adaabu
 
Wakati magufuli anatoa maumivu na vilio kwa watu ulikuwa haupo?
Je hapa umejibu swali? Ni vizuri ukajibu swali lililoulizwa kuliko kuharibu mantiki ya swali na mada.

Nami pia namsaidia kuuliza, Je taifa linajiponya kutokana na nini?
 
Nadhani nimeeleweka vizuri.
Kwani huwa hazipitiwi kabla ya kuwasilishwa, maana Simba wa burigi tulikuwa tunajua anaongea bila kusoma sehemu nyingine '' Anapuyanga vibaya sana'
Sasa sijui kuhusu chief.
Anaandikiwa na mzee wa Msoga




Ova[emoji41]
 

"Tunasifiwa kwamba adjustments [maboresho] tuliyoyafanya awamu ya tano kidogo zimekuza heshima ndani ya utumishi wa umma.

“Heshima iliyokuzwa ni ya woga kwa sababu kulikuwa na Simba wa Yuda, ambaye alikuwa ukimgusa sharubu anakurarua. Lakini hata hivyo hatukukua kivile, heshima inayotakiwa iwe ya moyoni, kila mmoja aheshimu mstari wa mwenzie, hicho ndicho tunachokosa Serikalini.

“Kila siku unasikia Waziri kakwaruzana na Katibu…upande wetu tunaenda kuimarisha Chuo cha Utumishi na Chuo cha Uongozi ili kufundisha watu majukumu ya utumishi wa umma, lakini Baraza la Maadili likisimama kwenye sheria na kurekebisha maadili ya watenda kazi wa Tanzania, tutaenda vizuri,"- Rais Samia Suluhu akiwaapisha viongozi watule leo Aprili 2, 2022, Chamwino Ikulu, Dodoma

---

Hakika kila chenye mwanzo lazima kiwe na mwisho.

Kumbe zile sifa za ooo nchi imerudisha heshima kwenye sehemu za kazi ilikuwa ni nidhamu ya uoga tu.

Magufuli alikuwa anawatishia watu na wakawa wanaonyesha heshima ya uoga.


Ukweli unauma lakini Rais ni bora anakuwa mkweli. Cha kushangaza bado kuna watu wanataka Raisi naye asiwe mkweli na kuaminisha watu uongo maana siku hizi Watanzania wengine wanapenda uongo kuliko ukweli. Nakushukuru Raisi kwa kuwa mwazi. Wafanyakazi wa Serikali wanatakiwa kutengeneza heshima ya kazi sio kumuogopa Raisi bali utamaduni wa kazi, heshima, kufuata sheria na kutopenda rushwa
 
Back
Top Bottom