Acha upotoshaji wa kijinga, hakuna popote watu wanakatazwa kufanya starehe hapa duniani, bali watu wanakatazwa kutenda dhambi, na kufanya starehe sio dhambi.
Unakuta kipindi cha Magu watu walikuwa wanatumia madaraka yao kukomoa watu na mifano ipo wazi, kuna watu waliagizwa wakapore pesa za watu kwenye mabureau De change, watu waliagizwa kupora fedha za watu kwenye mabenki, wakurugenzi walikuwa wanaagizwa kupindisha sheria za uchaguzi, mahakamani watu walifungwa ili kumfurahisha Magufuli. Je utii wa kufanya uhalifu ndio utii sahihi? Tulisikia maneno kuwa watu wa mwanza wasivunjiwe nyumba maana ndio waliompa kura, ila sehemu nyingine wavunjiwe. Je wale waliotii kuvunja nyumba za watu kinyume na amri ya mahakama walikuwa na utii sahihi?