Rais Samia awasili Saudi Arabia kushiriki mkutano unaozikutanisha nchi za Afrika na Saudi Arabia kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano

Mkuu hizo sifa zote za bi samia????
Siku hizi anaitwa simba wa nyika????
 
Ndiyo hivyo....si mnajua ukioa mzaramo lazima ukubali zile safari zake za kwenda kwao ngomani kila uchao....hawa watu wa pwani ni watu wa shughuli na vitu laini laini...kama shughuli haipo nyumbani itatafutwa popote ilipo.
Mzee wa Msoga mpaka aliitwa Vasco da gama.
Huyu ndiyo kwanza anaanza
 
Awamu ya arabuni hii.
Hii ni awamu ya maendeleo kwa Taifa letu ndio maana unaona chini ya uongozi wa Rais samia tumefanikiwa kupata mafanikio katika sekta zote.ndio maana uchumi wetu unaendelea kufanya vizuri,mzunguko wa fedha mitaani ni wenye afya,fursa za ajira kwa ajira zinaendelea kuongezeka kila uchwao pamoja na miradi mbalimbali ya maendeleo inaendelea kuchipuka Nchini
 
Ni lini rais samia ataalika mataifa ya nje yaje tanzania kama huo mkutano wa saudia kumbuka sisi ni matajiri na tuna fursa na raslmali nyingi ili waje kuwekeza na ikibidi tuwakopeshe.
Kwa Uchumi gani wa Mataifa kujikisanya Kwa Ajili ya Tanzania?

Watakuja kama Kiongozi mmja mmja kama ambavyo wamekuwa wanakuja.

Saudia ndio Largest Economy sio tuu ya Waarabu Bali the Middle East yote.
 
Malipo yako kwa hii comment mkuu!!
 
Ila huyu Mama kuna nchi hajaenda?
Kwa hiyo unataka alifungie Taifa letu chumbani?au unafikiri Tanzania ni kisiwa? Kwani kuna mipaka ambako inatakiwa asiende kuliwakilisha Taifa letu? Kwani umesikia kuna vikwazo vya aina yoyote ile ambavyo tumewekewa kama nchi kwa Rais wetu kutokwenda sehemu fulani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…