Rais Samia azindua ugawaji wa vitendea kazi kwa maafisa ugani kilimo. Asema Serikali imeongeza bajeti ya utafiti kutoka Tsh 7.35bn hadi 11bn

Rais Samia azindua ugawaji wa vitendea kazi kwa maafisa ugani kilimo. Asema Serikali imeongeza bajeti ya utafiti kutoka Tsh 7.35bn hadi 11bn

Maafisa ugani ni watu muhimu katika kupeleka na kutafsiri matokeo ya tafiti mbalimbali kwa wakulima, wanasayansi tunapofanya tafiti mara nyingi zinabaki kwenye machapisho ambayo yanaishia kusomwa na watafiti wengine, badala ya mapendekezo kupelekwa kwa maafisa ugani wakawaelimishe wakulima. Wizara ya TAMISEMI inatakiwa kuwa na dawati la kupokea mapendekezo mbalimbali ya watafiti yaliyotokana na tafiti zao ili wazisambaze kwa wagani waliopo halmashauri na kuweza kuwaelimisha wakulima.
Huu mtindo wa ugani haufai, niwa ghali sana na hauleti tija...Wagani walitakiwa kuwa sehemu ya uzalishaki kwenye kilimo hii tumepigwa Africa na kitu kizito ili tusitoke kwenyw hii small holder farming
 
Dodoma.
Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amemuomba Rais Samia Suluhu Hassan kumpatia Sh150 bilioni ili aziweke katika benki za biashara kama dhamana (security), hatua itakayowezesha wakulima nchini kuanza kupata ruzuku ya mbolea katika msimu wa kilimo ujayo.

Bashe ameomba fedha hizo leo Jumatatu Aprili 4, 2022 wakati wa hafla ya uzinduzi wa ugawaji wa vitendea kazi kwa maofisa ugani nchini.

Bashe amesema bei ya mbolea katika soko la dunia imepanda kwa zaidi asilimia 300.

Amesema Rais Samia aliielekeza Benki Kuu (BoT) kutenga Sh1 trilioni kwa ajili ya sekta ya kilimo na kumuomba Sh150 bilioni kwa ajili ya kuweka katika benki za biashara kama security.

Amesema hatua hiyo itawezesha kuaanza kutoa ruzuku ya mbolea katika msimu ujao wa kilimo.

“Nakuhakikishia mheshimiwa Rais fedha hii haitapotea. Tumeshafanya hivi katika korosho kwa kugawa ruzuku ya pembeje na tumeongeza uzalishaji tani 40,000,”amesema.


Aidha, Bashe amesema jumla ya maofisa ugani 7,000 watagawiwa pikipiki na vifaa vya kupimia udongo.

“Tumeanza kuwapa elimu maofisa ugani kulingana ekolojia ya maeneo na mazao yanayozalishwa na tutawapa ekari moja kwa kila ofisa ugani, atapewa mbegu bora na mbolea ili akiwafundisha awapeleke shambani,”amesema.

Amesema kuwa majaribio yameanza katika mikoa mitatu ya Dodoma, Singida na Simiyu kwa kutenga mashamba 600 ambapo kila kijiji kitakuwa na shamba darasa ili wakulima wapate elimu stahiki.

Pia amesema maofisa ugani hao watapatiwa vifaa vya kupimia udongo na kwamba hapo mwanzo taarifa za udongo zilikuwa zinapatikana kama za uganga wa kienyeji.

Bashe amesema lengo hadi kufikia mwaka 2025 kila kata iwe na kipimia udongo chake ambapo mkulima atapimiwa udongo na kupewa cheti ambacho kitakuwa na taarifa zote za afya ya udongo wake na aina ya virutubisho vinavyotakiwa.

View attachment 2175655
Aache porojo za kiwaki,mfuko wa mbolea 150,000 bado buster na dawa hazishikiki...hui uharo akaongee na ccm wenzake
 
Watu hata hawahitaji hizo ruzuku. Na jambo hilo lilifanyika na kufeli. Wakulima wanataka uhuru zaidi wa kuuza mazao yao. Mapinduzi ya kilimo China yalifikiwa baada ya serikari kuwaruhusu wananchi wao wauze mazao yao kokote watakako.
 
Alisikika mkulima mmoja baada ya kuuza kangomba na kununua heness
Hatutaki ruzuku tunataka mtutolee kodi kwenye kilimo pia mtu achie tuuze kwa uhuru pia samia ajiuzuru atufufulie,jembe letu ,,.
 
Serikali itafute namna ya kuzalisha mbolea ya kutosha tunapoteza pesa nyingi sana kuagiza, sio lazima kiwe kiwanda cha serikali lakini wanaweza kutoa security/dhamana na subsidies nyingine ili watu binafsi wajenge viwanda vya mbolea, ni muhimu sana kwa food safety ya nchi, tunatumia billions kuagiza mchele,ngano , mafuta ya kula etc vitu ambavyo tungeviweza wenyewe ndani ya nchi
 
"Kwa sasa idadi ya maafisa ugani tulionao nchini ni 6,704, idadi hii ni ndogo ukilinganisha na mahitaji yetu ya maafisa ugani 20,538 nchini, pamoja na idadi hii ndogo, pia kuna changamoto ya ukosefu wa vitendea kazi na mafunzo rejea kwa maafisa ugani nchini"

🎤 Waziri Mkenda

#BajetiYaKilimo2021
Kwa hiyo bashe anatembelea nyota ya Mkenda?
 
Per diem ya watu wote walioenda kwenye hii "circus" , petrol, na lost labour, pesa yote hii ingeweza kununua zaidi ya mara mbili ya hivyo vitenda kazi walivyogawa.

Ongezeko la 3.6bn kwa ajili ya research ni pesa ndogo sana kuleta impact kwenye kilimo.

Huyu waziri wa kilimo hana mikakati yoyote ya kukuza kilimo zaidi ya kutafuta kiki aka msanii
 
Kilichofanyika ni sawa na kuajiri mwalimu kwenye eneo lisilo n shule.

Unaboreshaje maisha ya afisa mmoja huku ukiwakandamiza wakulima ambao ni zaidi ya 60% ya watanzania wote? Huyo mgani anaenda kufanya nini
 
Leo maafisa ugani (extension officers) wanakabidhiwa Pikipiki, vipima udongo na simu janja (smart phone) ili viwawezeshe kutekeleza majukumu yao.

Hii fani ya maafisa ugani ilipoteza umuhimu kuanzia miaka ya 1980s. Hongera Samia kwa kumfanya Hussein Bashe kuwa Waziri kamili wa kilimo.
Asante kwa kunifumbua macho. Toka jana najiuliza hawa maafisa ugni ni watu gani hasa... Kumbe ni extension officers! Now I can happily contribute.
 
Mkulima atafaifika kwa kuhodhi soko? Kuwe na soko huru. Serkali afanye monitoring
 
Ila watanzania mna PhD ya kulalamika na kulaumu asee. Kwanini hamna Jambo jema kwenu?
1. Maafisa ugani wamewezeshwa usafiri na vipima uongo.
2. Mbegu ya alizeti na miche milioni 20 ya parachichi subsidized na hivyo kutolewa bure.
3. Kila Halmashauri kuwa na ofisi ya umwagiliaji inayopimwa performance yake kwa idadi ya ekari za umwagiliaji.
4. Kila afisa ugani lazima awe na shamba lake.
5. Kuanzia mwakani mbolea kupewa ruzuku na kutolewa kwa mkopo kama ilivyo kwenye korosho.
6. Ofisi ya Rais utumishi kupitia muundo Ili kuwezesha kuajiri mtaalam wa umwagiliaji kila halmashauri.
7. Benki zote zote mikopo ya single digit kwenye kilimo ambapo Benki ya CRDB na NMB tayari zimefikia hatua hiyo.
8. Serikali imetafuta masoko kwenye nchi zaidi ya 10 Ulaya na Asia na Afrika.
9. Hakuna mkulima amayepangiwa akauze wapi mazao yake kwa kipindi hiki;
10. Mabwawa kwa ajili ya umwagiliaji kuchimbwa kila Halmashauri yenye uhitaji na inayozalisha;
11. Kuanzisha mfuko wa maendeleo ya kilimo Ili kuwezesha utoaji wa ruzuku kwa mbolea pindi bei ikipanda;
12. Mashamba makubwa yaliyo chini ya msajili wa hazina sasa yazalishe kwa kuyakodisha kea sekta binafsi.
13. Eneo lote baada ya Bwawa la umeme lipimwe mashamba na yagaiwe kwa wawekezaji wakubwa Ili yazalishe kwani maji kwa ajili ya umwagiliaji tayari yatakuwepo.
14. Eneo la bonde la RUBADA lianze uzalishaji kwa njia ya ubia na sekta binafsi.

Pamoja na initiatives nyingi na nyingi. Sasa nyie mlitaka watu wafanye kitu hasa ili msilalsmike?
 
Ila watanzania mna PhD ya kulalamika na kulaumu asee. Kwanini hamna Jambo jema kwenu?
1. Maafisa ugani wamewezeshwa usafiri na vipima uongo.
2. Mbegu ya alizeti na miche milioni 20 ya parachichi subsidized na hivyo kutolewa bure.
3. Kila Halmashauri kuwa na ofisi ya umwagiliaji inayopimwa performance yake kwa idadi ya ekari za umwagiliaji.
4. Kila afisa ugani lazima awe na shamba lake.
5. Kuanzia mwakani mbolea kupewa ruzuku na kutolewa kwa mkopo kama ilivyo kwenye korosho.
6. Ofisi ya Rais utumishi kupitia muundo Ili kuwezesha kuajiri mtaalam wa umwagiliaji kila halmashauri.
7. Benki zote zote mikopo ya single digit kwenye kilimo ambapo Benki ya CRDB na NMB tayari zimefikia hatua hiyo.
8. Serikali imetafuta masoko kwenye nchi zaidi ya 10 Ulaya na Asia na Afrika.
9. Hakuna mkulima amayepangiwa akauze wapi mazao take kwa kipindi hiki;
10. Mabwawa kwa ajili ya umwagiliaji kuchimbwa kila Halmashauri yenye uhitaji na inayozalisha;
11. Kuanzisha mfuko wa maendeleo ya kilimo Ili kuwezesha utoaji wa ruzuku kwa mbolea pindi bei ikipanda;
12. Mashamba makubwa yaliyo chini ya mfuko wa hazina sasa yazalishe kwa kuyakodisha kea sekta binafsi.
13. Eneo lote baada ya Bwawa la umeme lipimwe mashamba na yagaiwe kwa wawekezaji wakubwa Ili yazalishe kwani maji kwa ajili ya umwagiliaji tayari yatakuwepo.
14. Eneo la bonde la RUBADA lianze uzalishaji kwa njia ya ubia na sekta binafsi.

Pamoja na initiatives nyingi na nyingi. Sasa nyie mlitaka watu wafanye kitu hasa ili msilalsmike?
Ndugu maandishi mazuri. Kufikirika! Hadithi za Akajasembamba! Bibi kizee akamlamba matongotongo hahaha!
Miche ya korosho ilikuwa hivyo hivyo, na ulikuwa utawala wa Simba wa Yuda!
4. Nyerere alijaribu Sana, kuhakikisha Hilo likafeli, watu wamesoma wapate ajira siyo walime!
Kulikuwa na benki ya wakulima, benki mikopo ya wakulima wanakuambia hatukopesheki, BIMA premium Kali!

YOTE HAYO YANAENDESHWA KISIASA SIYO KIMFUMO, na ni marudio tu ya Sera za awamu zilizopita,

Watu wameshakula per Diem kazi iendelee, kilimo hakihitaji maonyesho Ka vifaa vya kijeshi!

KILIMO NI KIGUMU
 
Back
Top Bottom