Rais Samia, bado RC Chalamila na RC Hapi

Rais Samia, bado RC Chalamila na RC Hapi

Ni kweli mkuu na hakuna siku moja tumeona mtu amelalamika kuonewa personal na Chalamila. Lakin watu wanaleta ujuaji wao wa kutaka kila maamuzi ya Chalamila yamfurahishe kila mtu.
Bora charamila,ndy anaweza kuwa na mapungufu lkn huwezi sikia, akiwavamia wafanyabiashara usiku wa manane au kuwapora watu fedha

Ova
 
Sikiliza,. Mimi sio Chalamila na wala sina maslahi ya moja Kwa moja kutoka kwake. Lakini penye ukweli lazima niseme. Tuhuma nyingi Kwa Chalamila kimsingi si tuhuma Bali majungu, ufuata mkumbo na ulimbukeni tulionao watanzania wengi kuzungumzia Mambo ambayo hatuyajui vizuri.
Mkuu peleka jeshi likatoe huduma ya daladala huko Mbeya.
 
Chalamila maneno mengi tu Tantalila za kutosha lakini sidhani kama ana shida kihivyo.Sema alikuwa na Imani kubwa na mwenda zake bado anaamini yupo na mwendazake huenda asimheshimu sana Mama hapo labda ndo inaweza ikawa Sababu ya kumpumzisha
Hana qualities za uongozi kiserikali. Ni mtu wa matamko ya kukurupuka na yasiyo na staha.
 
Sikiliza,. Mimi sio Chalamila na wala sina maslahi ya moja Kwa moja kutoka kwake. Lakini penye ukweli lazima niseme. Tuhuma nyingi Kwa Chalamila kimsingi si tuhuma Bali majungu, ufuata mkumbo na ulimbukeni tulionao watanzania wengi kuzungumzia Mambo ambayo hatuyajui vizuri.
Mkuu si uliwahi kusema Magufuli aanzishe chama kingine na kiitwe, CHAMA CHA MAGUFULI(CCM). Wenye Chama walikuangalia tu kwa mshangao!

Mtavikimbia vivuli vyenu mwaka huu!
 
RC Hapi na Chalamila hawana maadili ya uongozi, wababe, jeuri na taarifa zilizopo wanakesha kwa waganga kuloga maana walijiamini kupitiliza wakati wa JPM
Ujeuri huo ulipelekea RC HApi na Chalamila kumdharau pm na Makamu Rais na zaidi wakawa wasemaji wa serikali
RC Hapi aliwapiga mkwara Rais mstaafu na wastaafu wote kukaa kimya huyo Chalamila akajipa usemaji eti Rais mzima nimeongea naye na hata alipofariki akasema haamin
 
Chalamila ndiye aliyeleta bajaji Mbeya mjini? Hizi ni chuki za kijinga na wivu tu. Mbeya mjini bajaji zimefurika kabla ya ujio wa Chalamila. Pia hata hizo bajaji zipo Kwa ajili ya watanzania hasa tabaka la chini. Hizo gari kubwa unazosema mbona hamzipeleki Isanga?
Mkuu ukiwa mfupi usiwe na akili fupi.
Hiyo ndo tabiia ya Chalamila, badala ya kutatua tatizo la wananchi ,anatafuta ligi ya maneno.Chalamila hatoshi.
 
Katika awamu ya tano kuna vijana viongozi waliotia fora kutumia madaraka vibaya.

Mama Samia amewakonga mioyo watanzania kwa kumuondoa Ole Sabaya, Mkuu wa Wilaya ya Hai, aliyetia fora kwa kuongoza kwa ubabe, uonezi na uporaji.

Sasa bado viongozi wawili, RC wa Mbeya Chalamila, mtu asiye na staha wala karama ya uongozi, na RC wa Iringa, Hapi aliyewahi kuwadhalilisha wazee wa chama, kina Makama na Kinana.

Hawa walikuwa vile vile wanatumika, lazima nao waende zao.
Kawakosha Watanzania gani? Kwani Watanzania wote wanamjua Sabaya? Yetu macho na masikio. Mama umeambiwa wafute kazi na hao akina Api na Chalamila
 
Ndo shida ya wabongo chuki zao binafsi wanazileta kwenye siasa. Mbongo anataka akimchukia mtu bas watu wote wamchukie.
Na wewe ulikuwemo katika mpango wa Chalamila kuanzisha “CCM” Chama cha Magufuli, kama alivyopendekeza ?
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Nyumbu kama watoto wadogo!

Unachapwa kwenzi ukiliaaa unapatiwa pipi ili unyamaze.

Ishu ya DPP Biswaro ndio imetupwa kapuni kama hivyo.

La Sabaya nalo litazimwa na tukio lingine.

Asante ccm.
Kapalilie kaburi majani yameanza kuota
 
RC Hapi na Chalamila hawana maadili ya uongozi, wababe, jeuri na taarifa zilizopo wanakesha kwa waganga kuloga maana walijiamini kupitiliza wakati wa JPM
Ujeuri huo ulipelekea RC HApi na Chalamila kumdharau pm na Makamu Rais na zaidi wakawa wasemaji wa serikali
RC Hapi aliwapiga mkwara Rais mstaafu na wastaafu wote kukaa kimya huyo Chalamila akajipa usemaji eti Rais mzima nimeongea naye na hata alipofariki akasema haamin
Akili za wabongo wengi ni Shida tupu. Sasa mtu kusema Rai's ni mzima ni tatizo? Huelewi kwamba hakuwa na tamko rasmi kuhusu hali ya afya ya rais kipindi Chalamila anayasema hayo? Chalamila Kama mkuu wa mkoa aliwajibika kutoa kauli ya kuondoa sintofaham ili watu waendelee na shughuli zao mpaka pale tamko rasmi litakapotoka.
 
Katika awamu ya tano kuna vijana viongozi waliotia fora kutumia madaraka vibaya.

Mama Samia amewakonga mioyo watanzania kwa kumuondoa Ole Sabaya, Mkuu wa Wilaya ya Hai, aliyetia fora kwa kuongoza kwa ubabe, uonezi na uporaji.

Sasa bado viongozi wawili, RC wa Mbeya Chalamila, mtu asiye na staha wala karama ya uongozi, na RC wa Iringa, Hapi aliyewahi kuwadhalilisha wazee wa chama, kina Makama na Kinana.

Hawa walikuwa vile vile wanatumika, lazima nao waende zao.
Akisoma huu uzi bila shaka atafanya hivyo. Maana anaendeshwa pia na mitandao!
 
Back
Top Bottom