Pre GE2025 Rais Samia: Bei ya Sukari Ikiwa Juu Gen Z Wataingia Barabarani

Pre GE2025 Rais Samia: Bei ya Sukari Ikiwa Juu Gen Z Wataingia Barabarani

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema chakula ni siasa na kwamba kukiwa hakuna chakula au sukari ikipanda bei Vijana wa Gen Z hawatotulia bali wataingia barabarani (kuandamana) na kwa kulitambua hilo Serikali inaendelea kulinda maslahi ya makundi yote ikiwemo maslahi ya Wananchi bila kuathiri maslahi ya uwekezaji na viwanda.

Rais Samia amesema hayo leo August 03,2024 baada ya kuzindua Bwawa la Umwagiliaji la Kiwanda cha Sukari Mtibwa Mkoani Morogoro.

“Serikali inatambua umuhimu wa viwanda vya sukari Nchini tunalenga kufika masoko makubwa ikiwemo DRC ambako ni soko kubwa mno, kwahiyo sukari yote itakayozalishwa Tanzania italiwa ndani lakini tutauza Burundi DRC na Nchi nyingine zitakazotaka sukari yetu”

“Jukumu la Serikali ni kulinda na kutetea maslahi ya makundi yote katika Jamii, hivyo inapotokea Serikali inasimamia upande wa kundi lisilo na nguvu ni katika kutimiza jukumu hilo na kutetea maslahi ya makundi yote katika Jamii, hivyo Serikali inaposimama upande wa Wananchi wanaotaka sukari ya uhakika kwa bei himilivu inafanya hivyo kwa msingi huo na sio vingine vyovyote, sio kwamba tuna shida na viwanda au vyovyote vile, tunalinda uwekezaji, tunalinda viwanda lakini lazima tulinde na Wananchi wetu”

“Wanasema chakula ni siasa kukiwa hakuna chakula hapa ile Gen Z haitokaa kitako itaingia barabarani, au ukiwapandishia sukari ikifika kilo elfu 7, elfu 8, elfu 9 hawatotulia wengine wote hawa hawatotulia kwahiyo lazima tulinde maslahi ya kotekote”
Samahani Rais wangu. Kweli hayo yanatoka rohoni?
 
Na ndio maana Bashe alipambana na genge la Mpina lolilotaka kutengeneza uhaba wa sukari, na bado anajenga maghala kuhifadhi chakula.

Yaani awamu ya Samia ni kula kujigalagaza
 
uyu ni moja marais wenye mifano ya ovyo kwenye hotuba zao
 
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akiwa mkoani Morogoro katika uzinduzi wa bwawa la mradi wa upanuzi wa kiwanda cha Mtibwa sugar Ltd amesema Serikali itahakikisha kuwa wananchi wanapata sukari kwa bei nafuu na kulinda viwanda vya ndani kutokana na uwekezaji uliofanyika.

Serikali inavyosimama upande wa wananchi katika kuhakikisha wanapata sukari kwa bei himilivu, ni kwa msingi wa kulinda uwekezaji wa viwanda lakini lazima tulinde wananchi, hatuna shari na viwanda. Ukipandisha sukari hapa leo generation Z wataingia barabarani" - Rais Samia.
Soma pia: Baadhi ya mambo yaliyotokea kwa kusababishwa na Maandamano ya GEN Z Kenya


Kuna mijitu michawa...😂😂😂😂
 
Kwani hao Gen Z wa TZ wana Uchumi wa kunywa bia????
Watafanya chochote ilimradi wanywe ulabu....wataiba,watadanga,watakuwa viben ten,watashkishwa hadi ukuta....Lakini ilimradi Ijumaa aonekane anakunywa...
 
Huyo mama aache unafiki Tanzania hakuna Gen Z na sidhani Kama watatokea. Aache kujifananisha na nchi zinazojitambua.
 
Kenyatta Sr, aliwahi kusema Tanzania kuna maiti na sio binadamu
 
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akiwa mkoani Morogoro katika uzinduzi wa bwawa la mradi wa upanuzi wa kiwanda cha Mtibwa sugar Ltd amesema Serikali itahakikisha kuwa wananchi wanapata sukari kwa bei nafuu na kulinda viwanda vya ndani kutokana na uwekezaji uliofanyika.

Serikali inavyosimama upande wa wananchi katika kuhakikisha wanapata sukari kwa bei himilivu, ni kwa msingi wa kulinda uwekezaji wa viwanda lakini lazima tulinde wananchi, hatuna shari na viwanda. Ukipandisha sukari hapa leo generation Z wataingia barabarani" - Rais Samia.

Soma pia: Baadhi ya mambo yaliyotokea kwa kusababishwa na Maandamano ya GEN Z Kenya


anawabeep naona, au anataka wampigie. Sema vijana wenyewe hawawezi
 
Back
Top Bottom