Rais Samia, hii Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum ina ukakasi kidogo

Rais Samia, hii Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum ina ukakasi kidogo

Amani iwe kwako mkuu wangu wa nchi.

Nimeweka heading hiyo kuweza kukuvutia kusoma usuli wa hoja yangu.

Sote tunafahamu kwa Mujibu wa Katiba kuwa tasisi unayoiongoza imepewa mamlaka ya kuunda, kupangua ama kufuta wizara mbalimbali za serikali hasa kutokana na mahitaji ya nchi kwa wakati husika.

Umeunda wizara mahususi ya kushughulika na hitaji kubwa la ustawi na maendeleo ya kisekta kwa kulenga jamii hususan makundi yaliyo kwenye wskati mgumu kijamii ambayo ni wanawake, watoto na wenye ulemavu. Naongekea wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wanawake na Makundi Maalum. Nimeweka hapa chini screenshot ya banner la wizara lililopo kwenye interface ya tovuti ya wizara
View attachment 2547166

UKAKASI
Nimetafakari jina la Wizara ni kama linaleta ukakasi zaidi kwa muktadha wake.

Je neno JINSIA lilimaanisha nini ama aina gani ya jinsia zilizopo ndani ya neno hilo? Nimeona Jinsia imetajwa kisha mbeleni naona Wanawake wanatajwa nje ya jinsia. Ingesomeka wanaume badala ya jinsia ili kubeba mantiki ya neno wanawake mbeleni hapo.

Neno lingine ni makundi maalumu. Ambapo sisi raia wako tunaamini makundi maalumu ni wanawake, watoto na wenye ulemavu. Najiuliza kama jinsia lipo, wanawake wapo hapo kwenye makundi maalumu tunamaanisha makundi gani?

USHAURI
Nikiulizwa kuwa napendekeza jina lisomekaje nitajibu Jina la Wizara litapendeza likisomeka WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WATOTO NA WENYE ULEMAVU.

Nimetoa hoja

Mimi naona kuwa wanaificha taaluma husika hapo na kuibeza moja hiyo wizara ilitakiwa iwe ya ustawi wa jamii kwasababu makundi maalumu jinsia watoto walemavu wote hao wanafanyiwa kazi au kushighulikiwa matatizo yao na ustawi wa jamii lakini kuiweka maendeleo ya jamii wametukosea sana maendeleo ya jamii ilitakiwa iwe kule kwenye wizara ya fedha na mipango
 
Mimi naona kuwa wanaificha taaluma husika hapo na kuibeza moja hiyo wizara ilitakiwa iwe ya ustawi wa jamii kwasababu makundi maalumu jinsia watoto walemavu wote hao wanafanyiwa kazi au kushighulikiwa matatizo yao na ustawi wa jamii lakini kuiweka maendeleo ya jamii wametukosea sana maendeleo ya jamii ilitakiwa iwe kule kwenye wizara ya fedha na mipango
Mkuu nashukuru sana umeweza kuuweka mjadala sasa kwenye uelewa mpana.

Tukisema Wizara ya USTAWI WA JAMII inabeba nadharia pana zaidi kwa sababu hiyo ya kuanza kutaja constituencies za ndani ya ustawi wa jamii utakuta hatutaweza kumaliza leo.

serikali ikaliangelie hili nalo
 
Vulnerable group sio special needs ni vitu viwili tofauti.

Special needs au kundi la watu wenye mahitaji maalum kwa kiswahili inaashiria walemavu tu (physical disability only)...
Serikali hasa rais aangalie namna ya kukata haya maneno kwa kuiweka wizara hiyo kuitwa ya USTAWI WA JAMII...

mengine tutakuwa tunajenga dhana kila ahsubuhi
 
Mkuu nashukuru sana umeweza kuuweka mjadala sasa kwenye uelewa mpana.
Tukisema Wizara ya USTAWI WA JAMII inabeba nadharia pana zaidi kwa sababu hiyo ya kuanza kutaja constituencies za ndani ya ustawi wa jamii utakuta hatutaweza kumaliza leo.

serikali ikaliangelie hili nalo

Na ndio maana ata katika kufanya kazi tuna banwa swana na hawa maendeleo ya jamii

Unapo ongelea maendeleo ya jamii ina husisha maendeleo yote yanayo husu jamii na wizara yake ingependeza zaidi kuwa kwenye wizara ya fedha na mipango

Ila makundi maalumu jinsia walemavu na watoto hawa baba yao na mam yao ni ustawi wa jamii na siku zote wanaenda huko kutatuliwa laikini kwakuwa hatuna wizara maalumu tuna tanga tanga sana kama watoto yatima mala tuna hamishwa kwenye wizara ya afy mara maendeleo ya jamii sisi kama wana taaluma tuna taka wizara yetu isimame mwenyewe
 
Serikali hasa rais aangalie namna ya kukata haya maneno kwa kuiweka wizara hiyo kuitwa ya USTAWI WA JAMII...

mengine tutakuwa tunajenga dhana kila ahsubuhi
Ndio inavyoitwa nchi nyingi ‘ustawi wa jamii’ (social services), ila ni department tu ya wizara ya afya.

Lakini ata huko kwenye ustawi wa jamii utakuta kuna junior ministers wa watoto, junior minister special needs na junior wanawake na wazee.

Kwa sababu social services ina mambo mengi sana kuweza kuwa wizara independent na sera za hayo makundi hazifanani so either way unaweza badili jina lakini shughuli na majukumu zinabaki vile vile in practice.
 
Ndio inavyoitwa nchi nyingi ‘ustawi wa jamii’ (social services), ila ni department tu ya wizara ya afya.

Lakini ata huko kwenye ustawi wa jamii utakuta kuna junior ministers wa watoto, junior minister special needs na junior wanawake na wazee.

Kwa sababu social services ina mambo mengi sana kuweza kuwa wizara independent na sera za hayo makundi hazifanani so either way unaweza badili jina lakini shughuli na majukumu zinabaki vile vile in practice.

Lakini ushawai jiuiliza kwanini hawataki kuipa wizara yake yenyewe?
 
Namaanisha kuwa wizara inayo jitegemea kama wizara ya afya na isiwe inabebwa bebwa au kutambuliwa kama idara
Ndio mantiki ya kutoa maswala ya wanawake, wazee, watoto, vijana na watu wenye mahitaji maalum chini ya Afya ili wajikite na shughuli za ustawi wa jamii pekee (social services).

Jukumu lao sio kuwawezesha kifedha bali protection of their welbeing (safeguarding) be it they are failing miserably kwa matukio tunayosoma kila siku.

Wakuu shukran kwa mjadala mpaka jioni mungu akipenda. I really have to do other things now huku nikiwa msomaji tu wa JF.

👋
 
Neno JINSIA limeshazua taharuki huko Duniani na limepelekea kamusi zianze kutengeneza tafsiri mpya.

JINSIA linatupeleka kutambua Yale mambo yakishetwani ya sodoma na gomora, nashauri liondolewe itafutwe tafsiri isiyowapa watu wa magharibi mwanya wakupenyeza mambo Yao.

Huku kwao wameanza kuwa so sensitive kwenye haya maneno.....wanahita Haki sawa
 
Mkuu njoo na hoja sahihi kuhusu neno Raisi.

Mimi naongelea jina la Wizara ambapo hubeba majukumu, malengo na matarajio ya sekta husika.

Katika uundaji wa sentensi au aya huwa tunaona kurudiarudia neno ni kukosa ubunifu sahihi na kuishiwa kwa vocabularies
Twende mbele zaidi kidogo. Kama wizara ni ya Jamii, kwani Jamii ni nini!!? Kwanini tuichanganue jamii kwa jinsia badala ya jamii kwa ujumla wake!!? Why tuwe wabaguzi wa Jinsia!!?
 
Ninachoonaga na Wakuu wa Wilaya kuwapa kibali cha kupita kuchangisha michango tu sijui wanafanya nini kama wataalam,hivi chuoni ndivyo mlivyofundishwa?.
Sijui huo utaalamu wenu mnautumia vipi kama hutoajiliwa serikalini?.kama kuna mnayoyafanya tuambie tuwaelekeze wenye shida za kijamii muwatatulie.
 
Twende mbele zaidi kidogo. Kama wizara ni ya Jamii, kwani Jamii ni nini!!? Kwanini tuichanganue jamii kwa jinsia badala ya jamii kwa ujumla wake!!? Why tuwe wabaguzi wa Jinsia!!?
Mhe Dkt Mwijuma anaweza kuwa msaada mzuri kutuelimisha hapa, kwa sababu ni sehemu ya msingi wa hoja yangu pia
 
Back
Top Bottom