kaligopelelo
JF-Expert Member
- Jun 20, 2013
- 2,832
- 4,070
We jaribu jaribu tu huenda bahati ikakuchagua. Ukipewa mwaliko usiogope kukamatwa na wajuba.Ana id gani wajuba tulushe ndoano
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
We jaribu jaribu tu huenda bahati ikakuchagua. Ukipewa mwaliko usiogope kukamatwa na wajuba.Ana id gani wajuba tulushe ndoano
Hatari sana au sioWe jaribu jaribu tu huenda bahati ikakuchagua. Ukipewa mwaliko usiogope kukamatwa na wajuba.
Kwani Faiza fox mnamjua?Hahahah anakaribishwa kuwa memba kabisa,asiogope[emoji120]
Laaaaa,unakosa mengi mazuri.
Katika hotuba yake aliyoitoa huko mjini Moshi, hivi Leo, akiwa mgeni rasmi, katika sherehe ya akina mama, iliyoandaliwa na BAWACHA, Rais Samia, amesema kuwa huwa anapitia Jamii Forums, kujua watanzania wanasema Nini, juu ya Taifa lao.
Bravo Jamii Forums.
Jamii forum ya Sasa imevamiwa na vitoto Fulani havina hoja zaidi ya matusiRais Samia: Hakuna kisichowezekana kwenye mazungumzo, tumesuhudia nchi kadhaa zimeingia kwenye vita hawakupata suluhu, suluhu imepatikana kwenye mazungumzo kwahiyo tuendelee kuzungumza. Najua si rahisi kabisa watu kuja na utamaduni huu mpya ukakubalika mara moja, si rahisi, kwangu kuna vikwazo kwangu kuna vikwazo.
Huwa napitia Jamiiforums naangalia maoni yenu kule ndani, nasoma nnacheka, nasema lakini huu ni utamaduni mpya, si rahisi kukubalika kwa ghafla, kwahiyo pande zote Tanzania nzima si rahisi kukubali utamaduni huu mpya kwa haraka.
.Duh! Kama rais yumo humu hata mawaziri na vigogo wengine wamejaa humu tele na tunanyukana kwa hoja motomoto
Mods, JF imepewa heshima kubwa sana. Kama Rais huwa anapitia humu kupata maoni yetu kama sehemu ya umma wa Watanzania, hakika nawaambieni, hakuna kiongozi ambaye hatapita JF.
Lakini ili maoni yetu yapewe uzito wa kupewa tafakuri ni lazima Mods walinde hadhi ya jukwaa kwa kuwapa adhabu kale wale wote wanaoligeuza jukwaa lionekane ni la wahuni.
Mtu akitukana au kukejeli, apigwe ban hata ya miezi 6 au mwaka mzima. Kuna watu humu, wanashangaza, wanafikia kumtukana kiongozi, unatafakari na kujiuliza JF siku hizi imebeba watu wa namna gani?
Mods, lirudisheni jukwaa kwenye heshima yake ili kiwe ni chanzo muhimu cha habari kwa wasio na habari, liwe ni jukwaa la ushauri kwa viongozi wa Serikali, vyama na taasisi mbalimbali.
Pia waone namna ya kupunguza au kumeneji hizi mada za ngono naapenzi, zimekua nyingi mno na zisizo na mashiko.
Jpm alitamani malaika washuke Jf ifungwe
Kwa hiyo anafuatilia battle ya kataa ndoa na wale wataka ndoa🤣🤣🤣🤣🤣mzabzab Mama anaku zoom tabia zako
Kama kweli Mh. Rais unapitiaga maoni yetu yakiwemo ya kupunguza mfumuko wa bei na kupanda kwa gharama za maisha, tunaomba usiishie tu kucheka, jitahidi kupitia kwa wasaidizi wako kutupunguzia ukali wa maisha ili 2025, usitumie nguvu kubwa kutuomba kura. Achana na usemi wa Waswahili kwamba; "Mwenye shibe hamkumbuki mwenye njaa". Please mama, jitahidi kutulegezea gharama za maisha ili na sisi tukupende toka moyoni na siyo tukupende kwa unafiki au kwa sababu ya kukuogopa kutokana na nafasi uliyo nayo.Rais Samia: Hakuna kisichowezekana kwenye mazungumzo, tumesuhudia nchi kadhaa zimeingia kwenye vita hawakupata suluhu, suluhu imepatikana kwenye mazungumzo kwahiyo tuendelee kuzungumza. Najua si rahisi kabisa watu kuja na utamaduni huu mpya ukakubalika mara moja, si rahisi, kwangu kuna vikwazo kwangu kuna vikwazo.
Huwa napitia Jamiiforums naangalia maoni yenu kule ndani, nasoma nnacheka, nasema lakini huu ni utamaduni mpya, si rahisi kukubalika kwa ghafla, kwahiyo pande zote Tanzania nzima si rahisi kukubali utamaduni huu mpya kwa haraka.
Amani imezidi,Atuambie anatumia ID ipi isije kuwa ndiye anaaandika shaghala bagala.