Rais Samia ikiwezekana kwepa kuwalenga Wasukuma moja kwa moja kwenye hotuba zako

Rais Samia ikiwezekana kwepa kuwalenga Wasukuma moja kwa moja kwenye hotuba zako

Suzy Elias

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2021
Posts
1,067
Reaction score
6,200
Ni leo tena.

Mheshimiwa Rais amewatupia lawama Wasukuma kwa kuharibu vyanzo vya maji katika maeneo mbalimbali hapa nchini kwa sababu ya ufugaji wao wa ng'ombe wengi.

Nia yangu bayana kwenye andiko langu ni kumshauri Rais ikiwezekana ajizuie kuwataja moja kwa moja Wasukuma kwenye hadhira kwa sababu hali ile pengine inaweza kutafsirika tofauti na walengwa hasa ukizingatia ndani ya muda mchache wa Utawala wake tuhuma nyingi za kubaguliwa walengwa zi bayana.

Ingetosha mheshimiwa Rais angetoka kauli ya jumla tu kwamba wafugaji ni sehemu ya wanaoharibu vyanzo vya maji

Sasa unapowataja Wasukuma moja kwa moja ilhali wapo wamasai na makabila mengine mengi yanayofuga maelfu ya mifugo ni sawa na kuwabagua watajwa

Mungu ibariki Tanzania.
 
Mhe Rais ana ghaflika mno kuwasema tena kwa mabaya haimjengi kwai ni ushauri mzuri anapaswa auzingatie
Bila shaka angezungumzia wafugaji! Maana kauli hii inaweza kupelelea wakuu wa mikoa na askari wanyama pori kuanza kudhulu wafugaji bila sababu za msingi! Ukweli anaujua ni uzembe wa utawala wake ndo maana haya yanatokea!
 
Mikoa ya kanda ya ziwa ni kama ifuatavo Mwanza kiongozi wa kanda, Geita, shinyanga, simiyu, tabora, kigoma, mara na kagera yaani litakaloanzia mwanza kisiasa ujue mikoa tajwa italifuata kwa nguvu moja kabisa,
Kwa kweli mama ameteleza mno kuwananga tena kwa kuwataja kabisa huku akiwa amezungukwa na Maaskofu Wasukuma zaidi ya Saba 🤔 tena wakatoliki!
 
Back
Top Bottom