Rais Samia: Kama haumpendi Rais aliyeko, penda nchi yako

Rais Samia: Kama haumpendi Rais aliyeko, penda nchi yako

Yeye mwenyewe hana mapenzi na danganyika zaidi ya kule kwenye urojo......ndo maana kapiga pasu pesa ya uviko ikajenge himaya huko.
hamna ushahidi kwenye hili................na hata kama ipo hivyo ni kwa vile tuu Magufuli alimteua kuwa makamu wake na Maraisi wote wamekuwa wakiiamarisha mambo ya kwao hata kwa uchache tukumbuke hata Chato ipo vile kwasababu gani na ni ndani ya miaka mi5 ya kwanza ......ilishapendeza ,mpeni kijiji basi huku bara abadilishe kabila na ubini...........
 

Rais Samia Suluhu Hassan amesema urais sio mtu ni taasisi lakini kikatiba kunakuwa na mtu pale juu. Amewaambia Mawaziri kuwa kama hawampendi Rais aliyepo basi wapende nchi yao

Amesema hata kama haumpendi Rais Samia isiwe kigezo cha kupuuza mambo yote ambayo serikali inafanya. Ameruhusu watu kumchukia lakini sio kuchukia mambo ya serikali

Amewataka kuheshimu viapo vyao kwa kuwa wameapa kwa kushika vitabu vya Imani zao
Mi ni chadema kindakindaki lakini najikuta nampenda Mama automatically.,
 
Mama chapa kazi sie watu wa bara usitusikilize sana, sie ni watu chuki, visasi na ubaguzi, wengi hawana sabb ya kukuchukia isipo kua chuki zao za kijinsia na udini . Huku kwetu ni chuki tupu hatuna mioyo wa kusamehe na kupuuzia mambo mengine, paka tuue ndo turidhike, kuna lijama lilikua linaua watu hata viongozi wa dini yake walishinda kulikemea, we piga kazi tunakuamini tu.
Utakuwa hauko sawa kichwani wewe
 
Watu wanamchukia yeye kwasababu ya mambo ya serikali.

Watu wakipenda mambo ya serikali, “automatically” wanampenda na yeye. Wakumchukia hawawezi kukosekana. Lakini hawatakuwa wengi kama mambo ya serikali yanapendwa.

Hapa rais anaweza kuwa anazungumza kwa “codes” kwamba kuna watu wanamchukia yeye binafsi kwasababu ambazo hazihusiani na mwenendo wa serikali anayoiongoza. Sikubaliani naye. Maana ni yale yale ya kutumia “gender card” pamoja na uzanzibari.

Hata kigezo cha rais kutaka ama kuomba kuchaguliwa tena, kinapimwa na jinsi ambavyo serikali imefanya mambo yanayowagusa wananchi.

Watu wangapi Kati ya 60 m
 
Mama piga kazi, Mtangulizi wako Mh. JPM aliwahi kusema kuwa binadamu mwenye husuda hata kama wewe unaoga maji yeye kwa husuda zake atasema unamtimulia vumbi,wengi ya watanzania wanakuunga mkono mama , worry not.

Binadamu tumejawa husuda ambayo hupelekea upofu ndani ya mioyo ya wengi,hata akifanya jema gani hawaoni.


Wazungu wanasema, jealous is like a sand in your eyes ,it can stop someone from seeing things clearly.

#Kazi iendelee
 
Utakuwa hauko sawa kichwani wewe
Kama unakeleka na utawala wa Samia basi nenda Somalia
4052b00499a8a01d9fbb.jpg
 
Watu wanamchukia yeye kwasababu ya mambo ya serikali.

Watu wakipenda mambo ya serikali, “automatically” wanampenda na yeye. Wakumchukia hawawezi kukosekana. Lakini hawatakuwa wengi kama mambo ya serikali yanapendwa.

Hapa rais anaweza kuwa anazungumza kwa “codes” kwamba kuna watu wanamchukia yeye binafsi kwasababu ambazo hazihusiani na mwenendo wa serikali anayoiongoza. Sikubaliani naye. Maana ni yale yale ya kutumia “gender card” pamoja na uzanzibari.

Hata kigezo cha rais kutaka ama kuomba kuchaguliwa tena, kinapimwa na jinsi ambavyo serikali imefanya mambo yanayowagusa wananchi.
Sawa waendelee ameruhusu WAENDELEE KUMCHUKIA.....

Serikali ipo....
Nchi ipo......

#Siempre JMT🙏
 
Mama piga kazi, Mtangulizi wako Mh. JPM aliwahi kusema kuwa binadamu mwenye husuda hata kama wewe unaoga maji yeye kwa husuda zake atasema unamtimulia vumbi,wengi ya watanzania wanakuunga mkono mama , worry not.

Binadamu tumejawa husuda ambayo hupelekea upofu ndani ya mioyo ya wengi,hata akifanya jema gani hawaoni.


Wazungu wanasema, jealous is like a sand in your eyes ,it can stop someone from seeing things clearly.

#Kazi iendelee
😍
 
Ndio hulka za binadamu,Musa alichukiwa japo aliwatoa utumwani wana wa Israel. Hata Yesu alichukiwa na Wayahudi japo aliwafanyia mambo mengi na miujiza nyingi.
Watanzania nasi ni binadamu na bahati mbaya tumezoea kutawaliwa na mkono wa chuma na mtu mwenye ndevu.Ila huko mbeleni watu wale wale wanaokuchukia leo,miaka mitatu ijayo wanaweza wakakuelewa.
 
Mi nafikiri aendelee kuchapa kazi. Aachie wasaidizi kumjibia au kumtetea.

Wasio mtakia mema wakigundua kila neno anatafuta fursa ya kujibu, watazidisha mashambulizi na wengi wao hawana cha kupoteza.
 
Binafsi simchukii Samia.

Ila kuna baadhi ya mambo yasipokwenda sawa tunakosoa hapa.

Kwa Kikwete nilifanya hivyo.

Kwa Magufuli pia nilikosoa.

Hata kwa samia pia.

Ni mshauri Rais tu kuwa aachane na swala la kutafuta kupendwa .

Yeye afanya mambo sahihi tu akishauriana na washauri yake ila iwe for the National Interest.

Nchi hii ina watu Milioni 60 sio rahisi kila mmoja kumpenda na sio rahisi kila mmoja akaridhika na anachokifanya yeye.

The principle is do what is right always.
 
Back
Top Bottom