vexozanzhu
JF-Expert Member
- Mar 1, 2019
- 503
- 615
hamna ushahidi kwenye hili................na hata kama ipo hivyo ni kwa vile tuu Magufuli alimteua kuwa makamu wake na Maraisi wote wamekuwa wakiiamarisha mambo ya kwao hata kwa uchache tukumbuke hata Chato ipo vile kwasababu gani na ni ndani ya miaka mi5 ya kwanza ......ilishapendeza ,mpeni kijiji basi huku bara abadilishe kabila na ubini...........Yeye mwenyewe hana mapenzi na danganyika zaidi ya kule kwenye urojo......ndo maana kapiga pasu pesa ya uviko ikajenge himaya huko.
Halafu hizi Chuki zinatakiwa ziende kwa aliyempa nafasi ya Umakamu nashangaa watu hawalioni kama kweli Mama ni tatizo nadhani watu wanajua wakumlaumu.Mama asiyekupenda wewe atakuwa mchawi, mkabila na mdini,
Uko vizuri mama ila huwezi pendwa na wote
Piga kazi
Mi ni chadema kindakindaki lakini najikuta nampenda Mama automatically.,
Rais Samia Suluhu Hassan amesema urais sio mtu ni taasisi lakini kikatiba kunakuwa na mtu pale juu. Amewaambia Mawaziri kuwa kama hawampendi Rais aliyepo basi wapende nchi yao
Amesema hata kama haumpendi Rais Samia isiwe kigezo cha kupuuza mambo yote ambayo serikali inafanya. Ameruhusu watu kumchukia lakini sio kuchukia mambo ya serikali
Amewataka kuheshimu viapo vyao kwa kuwa wameapa kwa kushika vitabu vya Imani zao
Utakuwa hauko sawa kichwani weweMama chapa kazi sie watu wa bara usitusikilize sana, sie ni watu chuki, visasi na ubaguzi, wengi hawana sabb ya kukuchukia isipo kua chuki zao za kijinsia na udini . Huku kwetu ni chuki tupu hatuna mioyo wa kusamehe na kupuuzia mambo mengine, paka tuue ndo turidhike, kuna lijama lilikua linaua watu hata viongozi wa dini yake walishinda kulikemea, we piga kazi tunakuamini tu.
Alichaguliwa na Mwenda zake awe Makamu wake nadhani pia kwa chochote kutokea pia aliona anafaa, na kwakuwa Mzee alikuwa ni Jembe nadhani machaguo yake yalikuwa sahihi.Kwa kuweweseka huku, nadhani huyu nae alitokea kuleeeee walikomkuta Propesa Kabundi.
Ni kumchukia bure hawezi kujenga nchi na pesa zake mfukoniAmeshajuq hapendwi kwa Tozo zake
Watu wanamchukia yeye kwasababu ya mambo ya serikali.
Watu wakipenda mambo ya serikali, “automatically” wanampenda na yeye. Wakumchukia hawawezi kukosekana. Lakini hawatakuwa wengi kama mambo ya serikali yanapendwa.
Hapa rais anaweza kuwa anazungumza kwa “codes” kwamba kuna watu wanamchukia yeye binafsi kwasababu ambazo hazihusiani na mwenendo wa serikali anayoiongoza. Sikubaliani naye. Maana ni yale yale ya kutumia “gender card” pamoja na uzanzibari.
Hata kigezo cha rais kutaka ama kuomba kuchaguliwa tena, kinapimwa na jinsi ambavyo serikali imefanya mambo yanayowagusa wananchi.
Kama unakeleka na utawala wa Samia basi nenda SomaliaUtakuwa hauko sawa kichwani wewe
Sawa waendelee ameruhusu WAENDELEE KUMCHUKIA.....Watu wanamchukia yeye kwasababu ya mambo ya serikali.
Watu wakipenda mambo ya serikali, “automatically” wanampenda na yeye. Wakumchukia hawawezi kukosekana. Lakini hawatakuwa wengi kama mambo ya serikali yanapendwa.
Hapa rais anaweza kuwa anazungumza kwa “codes” kwamba kuna watu wanamchukia yeye binafsi kwasababu ambazo hazihusiani na mwenendo wa serikali anayoiongoza. Sikubaliani naye. Maana ni yale yale ya kutumia “gender card” pamoja na uzanzibari.
Hata kigezo cha rais kutaka ama kuomba kuchaguliwa tena, kinapimwa na jinsi ambavyo serikali imefanya mambo yanayowagusa wananchi.
😍Mama piga kazi, Mtangulizi wako Mh. JPM aliwahi kusema kuwa binadamu mwenye husuda hata kama wewe unaoga maji yeye kwa husuda zake atasema unamtimulia vumbi,wengi ya watanzania wanakuunga mkono mama , worry not.
Binadamu tumejawa husuda ambayo hupelekea upofu ndani ya mioyo ya wengi,hata akifanya jema gani hawaoni.
Wazungu wanasema, jealous is like a sand in your eyes ,it can stop someone from seeing things clearly.
#Kazi iendelee
Kweli kabisa. Siri ya mtungi ajuae ni kata. Panafuka moshi ndani ya Chama tawala.Mpaka kusema hivyo kutakuwa na kitu hakiko sawa