Rais Samia kama haya huyajui, hata tweets za Martin Maranja Masese kuhusu China Civil Engineering Company na kumuhusu Waziri wako Mwigulu huzioni?

Bora mmekuja wenye facts
 
Bora mmekuja wenye facts
Hapo nimeona kuna ukakasi na bahati mbaya wengi tunachangia kwa mihemko na siyo facts...

Unamzungumzia mtu ambayo kwanza anamiezi 13+ kuhusika na kandarasi ya kampuni ambayo ipo kwenye utekelezaji zaidi ya miezi 16+ tena unanasibisha na cheo chake cha sasa!!!!
 
Kichwa cha Mada kinaanza na maneno haya : " Rais Samia, Kama Haya Huyajui...."

Kuna kitu gani kinachomfanya mleta mada hii kufikiri kwamba Waziri anafanya anayofanya, lakini bosi wake awe hana lolote alijualo?

Ina maana gani kuleta mada za namna hii. Huyo bosi yeye hawezi kuamru yafanyike hayo yanayofanywa na waziri?
 
Vitu vya namna hii ni nadra sana siku hizi kuvikuta JF.
 
Duh! Hao CCECC ni hatari. Wameanza siku nyingi, nasikia. Godfather yupo Msoga.
China Civil wapo toka enzi za nyerere wao ndio walikuwa kwenye project ya Tazara iliyoanza late 1960's to 75.
 
Serikali ya huyu Bibi inachosha kabisa.
 
Miradi mingi ya kampuni za serikali ya china huwa niza mikopo isiyokua na Riba na hapo ndio wachina wanapotuweza kwasababu moja hela hatuna, mradi tunautaka na mabepari na world bank hawapo tayari kufadhili mradi, hapo kinachobaki ni kusurrender kwa wachina na tutenda kwa masharti yao....
 
Naona kuna mashindano ya chini chini kati ya Mwigulu na Makamba, wakati Mwigulu akijipigia huko kwa mchina na tender yake, Mqkamba anajipigia kule kwa $30milion za maintanance.

Hawa wote wana sifa moja kubwa, wote wanautaka Urais, sasa kama Samia akimshughulikia Mwigulu, basi lazima amshughulikie na Makamba pia.

Ila kama ataamua kumuacha mmoja, basi na awaache wote, taifa limekosa kiongozi, limepoteza muelekeo, kila mmoja anakula kwa urefu wa kamba yake bila shida.
 
Yaan Taasisi ya URAIS ikae ianze kufuatilia POSTS za Muuza SHANGA?

Wabongo mna matatizo ya akili si kitoto.

Hakuna mtu mwenye taarifa nyingi nchi hii kushinda RAIS wa Nchi.
 
Na gharama za ujenzi ni (Sh.11.1bn) kwa kila 1km. 411km mkandarasi atatumia Shs. 4.6T. Kapewa tender bila ushindani.[emoji17][emoji15][emoji17][emoji17][emoji3064][emoji3064][emoji3064]
 
Itakuwa Mbowe ameshalalamika Ikulu
Ninkwa sababu Mbowe na familia yake ni wazalendo sana tena wa grade one ambao walisaidiana na Nyerere kudai uhuru wa nhinyetu. Mbowe hawezi ona nchi inamumunywa na mchwa wa kuja akakaa kimya.
 
Kama ni kweli Kwa nini Serikali inashiriki rushwa? Kwa nini mnakomaa na kampuni zisizo na uwezo?

Kama mna kampuni zenu ambazo najua kwenye kazi.zote za tenda huwa kuna rushwa basi mtoe tenda kwa kampuni ambazo zina uwezo sio magumashi..

Nafahamu Yapi Merkez ni kampuyya Sukuma gang nayo imepewa lot ya makutopora kwa single source lakini wao wanaonyesha progress sasa vipi hiyo kampuni yenu ya Kichina haioneshi progress na mnakomaa nayo?

Huu utaratibu wa chama kutafuta pesa za kampeni kwa kuibia wananchi kupitia miradi kuongezwa gharama au kutafuta kampuni za kijinga sio sawa..

Tanzania hii ukiwa mtu wa Chini ndio unaumia..

Nafuatilia hili nikikuta kuna ukweli basi ntajua cha kufanya,Rais anajua Sana ila wanamwambia wanatafuta pesa za kampeni 2025.
 
Yale Yale Ya Mlimani City Watu Wamekuja Masikini, Wameondoka Na Utajiri Tele
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…