Tetesi: Rais Samia, kama kuna upendeleo huu wa kielimu kwa Wasichana utaliangamiza Taifa

Tetesi: Rais Samia, kama kuna upendeleo huu wa kielimu kwa Wasichana utaliangamiza Taifa

Hii dunia inapoelekea mwanamme anenda kupata tabu sana. Cha ajabu hayo mambo yanafanyika huku baadhi ya mijanadume ikiwa ndani ya hizo projects.

Siku hizi hata ma bank company ikiwa na wanawake ina possibility kubwa ya kuwa na advantages nyingi tu kwenye suala zima la mikopo.

Hawa mashetani lengo lao ni kuwa hii dunia itawaliwe na wanawake. na kuna mipuuzi kibao bado inaendelea kusapoti hayo mambo utawaona wengi humu wakichangia.
Ambaye husapoti si unaona hapa kwanini uchukui action na wewe unasema ni mwanaume?
 
Au wakilazimisha mtu awe Engineer wa ndege vipi siku akiangusha ndege?
Hakuna mtu yeyote analazimishwa kuwa chochote na serikali. Serikali inachofanya ni kuondoa au kusahihisha vikiwazo vya kimfumo "systematic" kwa wale wanaotaka kuwa engineer, Doctor, au chochote. Nyie local Andrew Tates mna hoja zilizo mufilisi sana.
 
Kwa sababu haina uwezo wa kuwafuatilia na kuwabeba wote, kwa sababu hivyo ndivyo serikali inavyofanya na inavyotakiwa kufanya mambo yake, kwa vipaumbele. Ndio maana unaona kuna sehemu zinapewa kipaumbele cha miradi mipya ya maji, umeme, barabara, hospitali n.k na maeno mengine hawapewei hivyo vipaumbele kwa sababu serikali inaona wako katika hali nzuri, sasa itashangaza mbunge mwenye kata 9 kati ya 10 zenye maji akianza kulalamika kwa sababu mwenzake mwenye kati 2 kati ya 10 ameongezewa miradi mipya ya maji katika kata zake nyingine 2.
Sasa mbona serikali yako tukufu imechukua maamuzi ya kuwabeba wasichana kabla ya kufanya upembuzi yakinifu na wewe unashangilia? Naona sasa umeanza kujipinga wewe mwenyewe. Bado kidogo tu utanielewa.
 
Bandiko zuri kabisa hili

Wanawapendelea Mabinti Kwny mitihani

Afu matokeo yakitoka wanasema wasichana ndo wameongoza kwa ufaulu[emoji848]
 
Shule nyingi sasa zina mabweni kwaajili ya wasichana.
Wavulana ni kama hawaangaliwi sasa.
Hata mwalimu mmoja wa sekondari aliniambia sasa ni too much.
Wasichana wamekuwa kama special group
 
Mazingira ya shule hayaanzii darasani, usiwe kilaza. Kusoma vizuri darasani na ufaulu unategemea zaidi mazingara ya nyumbani, kijijini au mtaani.

Kama shule iko mbali na makazi na watoto wote wanatembea kwenda shule ni wazi watakaoathurika zaidi ni watoto wa kike.

Kwenye jamii nyingi watoto wa kike ndio wanaofanya kazi za nyumbani kupika, kufua, kuosha vyombo, kutafuta kuni, kuchota maji n.k.

Miaka michache tu hapo nyuma ukeketaji ulikuwa ni tatizo kubwa lililowafanya watoto wengine wa kike kukimbia kwao. Kuna watoto wa kike wanasoma wakiwa na mawazo kichwani wazazi wao wanataka kukatisha masomo na kuwaoza mapema. Watoto kama hawa unawafidiaje kuwasadia darasani darasani??

Kuna suala la hedhi ambako sehemu nyingine za vijijini hao watoto wa kike waliobalehe wanapoteza hadi wiki nzima kutokana na kukosa pedi na mazingira mengine magumu ya shule wakiwa katika hali hiyo.

Hapa hatajuzangumzia hata kama mazingira yangekuwa sawa, mtoto wa kike akiishia kidato cha 4 na hana muelekeo kupata mimba ni dakika 0 tu, mwanaume hapati mimba na anaweza kufanya kazi nyingi zaidi kuliko mwanaume.

Kipi ambacho hamuelewei nyie local Andrew Tates??
Kwa namna umeongea umenikumbusha kuhusu story moja ya mashindanonya wanyama ambapo, zoezi la kwanza ilikuwa ni kukwea mti mrefu sana na mshindi apatikane.

Washiriki walikuwa ni tembo, nyani, samaki, nyoka, pundamilia na wengineo. Sasa jiulize hapo hili shindano lilikuwa linalenga nini maana hawa wanyama hawafanani hata kimaumbile na hata mazingira yao je wangeza kufanya jambo moja perfectly?

Jibu ni hapana.

Jamii ya sasa inaamini katika mfumo wa elimu bila hata kiquestion mfumo wa elimu umekuwa structured vipi. Je unaendana na mahitaji yetu, mwisho wa siku unatimiza malengo tunayotarajia.

Je huu mfumo walengwa wake ni akina nani by nature?!

Hivi mfano ukitangaza chuo cha urembo, mapambo ya kike, upishi, na fashion utategemea tuwe na 50/50 registration ya wanafunzi wa jinsia ya kiume na kike. Nini itakuwa target yetu?

Leo tunawaforce hawa mabinti kwenda shule katika mazingira ambayo hata wao hayawa accommodate, ili baada ya miaka 20 tupate nini, and tunawekeza mabilioni ya pesa katika hizi project hasara.

Sio kwamba tunakosea kulazimisha mtoto wa kike apitie trainings zile zile kama wa kiume ili tutegemee matokeo yale yale kwa mtoto wa kike na wakiume?

So mtoto wa kiume anapata hedhi for at least 5 days in a month, plus mtoto wa kike anatakiwa kukeep up na majukumu ya nyumbani sababu ni sehemu ya kumuandaa kijamii kuwa mwanamke, asipofanya hivi hata akimaliza shule unataka kunambia hatokuja kuwa mke wa mtu au mama wa familia so ni wapi wanatoa hayo mafunzo au kumuandaa kwa hilo?!

Kuna sehemu tunakosea aisee. Inabidi huu mfumo wa elimu ufumuliwe tujue tunakosea wapi. Pengine watoto wa kiume na wakike hawatakiwi kusoma at the same system maana kuwaweka sehemu moja why inaonekana kama wakike analazimika kusaidiwa ili awe kama wa kiume why isiwe naturally tu wa kike na wa kiume kuwe na vitu wawe wana click by nature sio human force au society Pressure?

Ina maana kama watoto wa kike wanatakiwa kupewa sapoti na empowerment it means this system kwao sio match they have to deal with another system for them.
 
Kwasababu wasichana wapo more vulnerable kuliko wanaume.

Msichana akipata elimu jamii nzima inaendelea.

Nitaeleza kidogo.

Kwa mfano, ikiwa watoto wote wawili wa kike na kiume wakaishia form 4, unadhan yupi ataathirika kwa haraka zaid kuliko mwingine? Hasa linapokuja suala la uzazi? Na hivyo kuongezea serikal mzigo wa kulea watoto mapema.

Lakini pia, kazi na ajira nyingi semi skilled zinambeba zaid mtoto wa kiume kuliko wa kike.
Ufundi, Udereva, Umachinga, Ubaharia, uvuvi, kufuga, kulima, misitu nk

Nadhani uamuzi huo ni wa busara sana.
Ukimpa kazi mwanaume ujue kuna wanawake kibao wananufaika kwanzia atakaeolewa plus wale michepuko sasa mpe ajira mwanamke kwanz hawatak tena kuolewa nakuna mwanaume atanufaika zaid yamchungaji
 
Wewe unasema nini wewe. Hivi mtu achaguliwe kindezi ndezi huku chini halafu aje kuwa na best performance huku juu inawezekana?!
Inawezekana sana tu, hasa kwa course za sayansi, nawajua wengi walilamba 2 na 3 na wakatoka na First class au Upper second with Honors ..
 
Ukimpa kazi mwanaume ujue kuna wanawake kibao wananufaika kwanzia atakaeolewa plus wale michepuko sasa mpe ajira mwanamke kwanz hawatak tena kuolewa nakuna mwanaume atanufaika zaid yamchungaji
Hizo ni personal choices, lakini ni vizur kama taifa tukakuza usawa wa kijinsi na kijinsia kwa manufaa ya kesho.
 
Sasa hapo Kwa hoja yako itakuwa unadahili wanafunzi kwa uwezo wao au kwa kuwaonea huruma. Na je nini matokeo ya kuwaonea huruma?
Ufikirie ufaulu wanafunzi katika mfumo "range" zilikubaliwa na sio "absolutes".

Yani C-A(C, B, B+, A), III-I badala ya F na A tu, au 1 na 0 tu. Kama umefikia chuo unaelewa maana ya GPA, ina range.

Mitihani ya wanafunzi wote huwa inasahihishwa kwa usawa, hakuna ambaye huwa anaongezewa au kupunguziwa maksi.
Utafauti huwa unakuja katika kuwachagua kwenda shule au vyuo, hapo ndipo watasema mwenye III kati ya jinsia mbili mwanamke atapewa kipaumbele, mwenye III kati ya mlemavu, albino na mtu asiye mlemavu hao walemavu ndio wanapewa kipaumbele.

Ni hivyo kwenye mikopo ya HESLB pia japo ni mkopo unaolipwa, ila siku serikali ikiwa na pesa za kuwapa wote wanaotaka hakutakuwa na hivyo vigezo sijui nyumba yenu ni ya makuti, bati au vigae, yatima n.k.
 
Tofauti na hoja ya viti maaluma huna hoja nyingine yoyote ya msingi.

Kuhusu wanawake kupata nafasi za upendeleo katika masomo ni sahihi kwa sababu jamii nyingi hasa za vijijini hazikuthamini masomo kwa mtoto wa kike kwa muda mrefu hivyo serikali inachofanya ni kusahuhisha hiyo injustice ya muda mrefu. Kuna visa vya watoto wa kike wanaambiwa wafeli mitihani ya darasa la saba makusudi ili waolewe.
Kwa hiyo unatengeneza taifa lenye madokta wa kupendelewe?
 
Kwasababu wasichana wapo more vulnerable kuliko wanaume.

Msichana akipata elimu jamii nzima inaendelea.

Nitaeleza kidogo.

Kwa mfano, ikiwa watoto wote wawili wa kike na kiume wakaishia form 4, unadhan yupi ataathirika kwa haraka zaid kuliko mwingine? Hasa linapokuja suala la uzazi? Na hivyo kuongezea serikal mzigo wa kulea watoto mapema.

Lakini pia, kazi na ajira nyingi semi skilled zinambeba zaid mtoto wa kiume kuliko wa kike.
Ufundi, Udereva, Umachinga, Ubaharia, uvuvi, kufuga, kulima, misitu nk

Nadhani uamuzi huo ni wa busara sana.
Na wewe ni mama? Basi taifa lina hasara?
 
Inasikitisha. Nchi jhii imaelekea mahali pabaya sana. Miaka michache iijayo kila jamii itakuwa multilineal. Ni shida kubwa!
Marekani na western world sasa wanaanza kulipia. matriarchal society huwa inazalisha vijana dhaifu na very emotional.

Sasa ukute mwanaume wa miraba minne halafu awe soft ndio wale maisha yakiwa magumu anashika gun anakwenda kumiminia risasi watu katika shopping centers au movie theaters, or worse anakuwa Serial killer.

Plus crime rates zinakuwa juu sana katika matriarchal society. Tazama marekani watoto wanaolelewa na familia ambazo ukitrace uzao wao unakuta ni generation ya single mothers kutoka bibi watatu nyuma. Matokeo watoto wanakuwa under disciplined na kuwa na jamii ya hovyo kupigana shaba nje nje, madawa ya kulevya, ubakaji, sodomy, na children molestations plus alot of jailed male members wa familia.

Haya tutakuja yaona hata hapa kwenye jamii hii ya sasa kwasababu ndicho kinachokwenda kutengenezwa na hii serikali pamoja na hawa wanaosapoti kila upumbavu.

Kwasasa wimbi la kwanza limeanza kuzaa hovyo bila Ndoa so its official ndoa imeanza kuwa myth kwa watoto wengi wa kike na wa kiume wameshakata tamaa wanafanya tu ngono na kuzaa ili wasipoteze jina la ukoo basi ndoa ni kero.

Ushoga ndio huo sasa mnaona umesambaa kila mkoa. Matendo ya ulawiti wa watoto tazama taarifa ya habari utajionea uhalisia.

Uhalifu nadhani sote tunajua Panya road tunaona balaa lake. Yote haya in the Span of just 10 and not more than 30 years.

Sasa ipo siku ndipo mtakuja sema Vitabu vya Dini vilikuwa sahihi kuwa mwanamke ni wa kuongozwa na mwanaume na mwanamke anatakiwa kutumia muda mwingi zaidi nyumbani kulea watoto na sio kutanga tanga huko nje akikimbizana na ndoto za alinacha za kuwa tajiri namba moja wa kike.

Upuuzi tu.
 
Niseme tu kuwa hili suala lilikuwepo tangu zamani ingawa miaka ya hivi karbuni liliondolewa km siyo kupungua. Mfano mzuri ni kwa Walimu. Huko nyuma kabla ya kufuta division 4 km kigezo Cha kujiunga na chuo kwa elimu ya Ualimu shule za Msingi (cheti aka certificate) utaratibu ulikuwa hivi;
1) Jinsia ya kiume walitakiwa wawe na division 4 ya point 26 kurudi chini.
2) Jinsia ya kike walitakiwa wawe na division 4 ya point 28 kurudi chini.

Hivyo kwa Mfano huo tu hapo juu ni dhahiri hili siyo jambo geni ingawa linatia ukakasi. Baada ya kuweka limit kuwa Ualimu wa shule za Msingi mwisho iwe division 3 ya point 25 kidogo ndiyo ikaleta usawa. Hata hivyo hadi sasa wanaochukiliwa wengi kuendelea na certificate ya Ualimu shule za Msingi ni tofauti na idadi ya Vijana wa kiume. Mfano, kwa sasa wote mnaweza kuwa na division 3 ya point 23, msichana atachukuliwa kwenda certificate hiyo na wewe mvulana utaachwa iwapo nafasi ni chache.

Hata mimi shule niliyosoma (ilikuwa shule binafsi ya Dini-RC) kwa wanafunzi wa O-level wavunana walitakiwa kufikisha wastani wa 48 wakati wasichana ilikuwa wastani wa 45 ili uweze kutoka darasa moja kwenda lingine. Kwa A-Level ilikuwa ni wastani wa 50 kwa wote bila kujali jinsia.

Mifano ipo mingi sn. Ila kumekuwa na sababu kadhaa zinazotolewa. Zingine unaweza kuona km zina materialize na zingine ni km they don't hold water.
Kwa mantiki hii tusishangae ni kawaida tu.
 
Hivi ni vitu gani unaandika wewe mbona kama haujatumia hekima hata kidogo ingawa unataka kuonekana mwenye hekima?!

Sasa nikuulize swali la kikuda, unataka kuniambia kwasababu kuna changamoto za kijamii zinazosababisha watoto wa kike kushuka kielimu basi suluhu ni kuwawekea vigezo legezi ili wapitishwe lengo likiwa ni kuonyesha matokeo chanya katika makaratasi ya wizara ila vipi uhalisia wa matokeo ya kiufanisi?

Wewe umeambia taaluma zinataka watu wanaobebwa?! Mfano mtu anatamani kuwa daktari ila hana uwezo wa kushika masomo ya udaktari nini unategemea kitokee hapo?!

Si ndio mwisho wa siku tunapata watu wanaokalia taaluma ambazo hawana weledi nazo?!

Kitu ambacho watanzania tumekuwa na vichwa vizito kujifunza ni kutokujifunza na makosa.

Miaka ya nyuma wizara ya elimu waliamua kwa makusudi kushusha vigezo vya watu kusomea Ualimu. Wakaweka vigezo vya chini kabisa kwamba mtu akiwa hata na division 4 atapata kazi ya Ualimu na mkopo juu.

Fast Forward leo hii. Hivi unaona namna elimu inavyozidi kudidimia sababu ya maamuzi ya kipumbavu kama yale. Na watu walikemea sana lile jambo wakasema kwann tusilimi watu kwenda ualimu mwisho iwe division 2. Watu wakatoa sana kauli za kishujaa bila kuwazia hatima ya taifa miaka 100 ijayo.

Leo miaka hata 20 haijapita tumeanza kuvuna hasara. Idadi ya walimu imekuwa kubwa kupita uwezo wa serikali kuajiri.

Walimu wenyewe wengi wanapata udahili kwa vigezo vya chini na matokeo skills zao ni questionable.

Leo serikali inalazimika kutengeneza shule nyingi ili kuajiri walimu ambao kiuhalisia haiwezi wamudu kuwalipa kwa wingi wao.

Impact ipo wapi tukitazama wanafunzi wetu wa sasa unaweza linganisha na wale wa miaka hiyo ya nyuma. Wanafunzi wa sasa wana low but very poor academic performances.

Haya ni matokeo ya maamuzi ya kipumbavu ambayo hayalengi kufanya maboresho bali ni kutokana na upotofu wa akili.
Afadhali umekuja mkuu Zemanda unisaidie kuwaelimisha hawa viumbe. Mwanzoni mtihani wa form II passmark ya kwenda form III ilikuwa marks 30. Baada ya wanafunzi wengi kuonekana wanafeli, serikali ikashusha marks hadi 21 lakini matokeo yakazidi kuwa mabaya. Ndipo wakashusha tena hadi marks 18 na bado wanafunzi wakaendelea wanafeli. Baadaye wakaona isiwe taabu.....waliofeli wote waendelee tu na masomo ya form III. Matokeo yake sasa wanafunzi hawajitumi tena kusoma kwa kuwa hawaogopi chochote......upass, ufell, unaenda form III. Hatimaye sasa mtihani wa FTNA hauna maana tena na watoto wamerelax hawasomi. Ndio maana utashangaa watoto wakienda sekondari wakiwa hawajui kusoma wala kuandika kwa sababu ya ujinga huu wa kulegeza mambo katika elimu kwa misingi ya kijinsia na kutafuta kiki za kisiasa.

Na kwa kuwa sasa wamezoea kubebwa tutegemee kupata digriii nyingi za chupi na hawo wanawake wakipatahizo digrii za chupa watakuja hapa mtaani kutusumbua na wengine wataenda kazini na ku-undeperform na hatimaye kushusha productivity. Na matokeo haya sharti yatamgusa kila raia, hata wale ambao wanashabikia upumbavu huu hii leo. It is just a matter of time. Namsubiri mkuu Mpwayungu Village aje atie neo hapa maana ana ujuzi mkubwa kwenye masuala ya elimu
 
Wakati wanaume wanapendelewa Taifa halikuangamia ila litaangamia baada ya wanawake kupewa kilicho Chao? [emoji2957][emoji2957]
Wewe unavyoona hali ya ustawi wa jamii miaka ya uhuru na sasa ni sawa?! Hebu tumia akili kidogo au ndio wale madogo wa kuzaliwa 2000 unabishana na watu tulioshuhudia babu akiwa na nguvu zake.
 
Back
Top Bottom