Rais Samia: Katiba mpya hadi watu wasome waelewe maana ya katiba hata hii tuliyonayo

Rais Samia: Katiba mpya hadi watu wasome waelewe maana ya katiba hata hii tuliyonayo

Mie japo huwa siuelewi uongozi wake ila kwa namna fulani yupo sawa maana kati ya hawa watz milioni 62 sidhani kama wenye uelewa wa katiba wanafika hata milioni 1...watu wajue hii iliopo inaupungufu gani sio kelele za katiba na wakati hawafahamu hata unahusu nini.
Muda wote walikiwa wapi? Yani kusikia CHADEMA wanataka mchakato wa katiba mpya uanze wamekimbilia single ya kutoa elimu miaka mitatu.
 
Wakina nani watakuwa na wajibu wa kuitoa hiyo elimu ya Katiba?
 
Wewe kwanini unataka katiba mpya?
Nina sababu hamsini. Sababu ya kwanza nimejifunza Madagascar, uchaguzi ukikaribia Rais aliyepo madarakani anajiuzulu kabla ya kampeni kuanza ili asiweze kutumia madaraka yake vibaya kuiba uchaguzi.
 
Umejitahidi kupotosha mkuu,

Alichosema ni kuwa, watu wapewe shule vizuri ya katiba hii tulionayo, na pia kasema vizuri kabisa, katiba ni ya watanzania, hatuwez sema tuchukue maoni ya wanasiasa tu ndio tuunde katiba, lazima kila mtu atoe maoni, na ili kila mtu atoe maoni ni lazima watu waijue hii katiba iliyopo, na yupo sahihi.
Inabidi tutambue jambo moja hata nusu ya watz hawatokuja kuelewa Juu ya vipengele vyote ktk katiba hata baada ya kupata elimu mchakato wa maoni ulishafanyika majority wakatoa maoni yao na pesa nyingi ikatumika wananchi tunaitaji katiba mpya
 
Dude linaloitwa katiba Raisi wa jamhuri ya muungano wa tanzania Samia Suluhu hassan amesema kwamba watu wa nchi hii hakuna anaejuwa maana ya katiba kwa hiyo ni vizuri watu kwanza wafundishwe waelewe maana ya katiba kwani hata tuliyonayo hakuna anayeifahamu.

kuhusu katiba mpya jambo hilo litafanyika hadi pale watu watakapo kuwa wanaelewa hata hii tuliyonayo hii maana yake ni kwamba vyama vya upinzani ingawa vimeendelea kusisitiza kuwepo umhimu wa katiba mpya wajue kuwa kwa sasa hilo suala halipo.

Jambo pekee ambalo serikali inaenda kulifanya ni kuwepo kwa somo la katiba mashuleni na vyuoni pamoja na taasisi zote za dini na serikali kuelemishwa maana ya katiba kwani watanzania hawana uelewa na katiba hiyo.

Ndugu zangu vyama vya upinzani mjue kuwa tunaenda kufanya uchaguzi mkuu bila kuwepo kwa tume huru wala katiba mpya! je mko tayari kwenye mashindano? [emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15][emoji15]
Expecting results from what you know (kutetegemea matokeo kwa jambo unalijua) I like this proverb Ostracism
 
Subirini wananchi wapate elimu kwa miaka mitatu. Katiba sio ya vyama ni ya wananchi.
Kama anasema katiba yenye zaidi ya miaka 50 Watanzania hawailewi.
Hiyo mpya ndiyo itaeleweka katika kipindi cha miaka 3.
Kumbe tume ya Warioba ilikuwa inawahoji Watanzania au Warundi.
 
Kwani ilipoandikwa hii yasasa watanzania walikuwa wanawelewa kuihusu?
Viongozi wa Afrika ni aibu kwa wenye akili na welewa!!
Tume iloundwa na mamilioni waliyotumia kwenye mchakato wa katiba Tena akiwa mwenyekiti ilikiwa nimchezo wakutafuna Kodi zetu?
Ni lini alijua waTz hawaijui katiba naye kama rais Toka aingie ikulu alifanya nini ili waijue??
Kwa ajuavyo otachikuwa miaka mingapi iliwote tuijue alafu tuandike hiyo nyingine??
Tunaviongozi wa ajabu na wa aibu kwelikweli...
 
Tunasema wananchi ndio wanaodai katiba mpya. Rais anasema wananchi wengi hawaijui katiba iliyopo hivyo wanashindwa kuonyesha katiba hii ina kasoro zipi! Dawa ni kutoa elimu kwa wananchi wote kwanza! A major paradox.

Hii ni kuanzisha mchezo usio na mwisho (a vicious circle). Tatizo kubwa la katiba hii ni madaraka yaliyopitiliza ya Rais yanayomuweka juu ya katiba na sheria. Marekebisho ya vifungu muhimu kuhakikisha viongozi wote, serikali nzima na vyombo vya dola vinakuwa na kutenda kazi ndani ya mzingo wa katiba, sheria na kanuni kuu za nchi ndicho kinachotakiwa. Wananchi hawahitaji elimu katika hilo. Wanalijua sana na linaathiri maisha yao ya siku kwa siku. Ukusanyaji wa maoni wa kamati ya Jaji Warioba ulithibitisha hayo na mifano ipo tele.

Rais na makundi yake ndani na nje ya serikali ndio wanaoogopa marekebisho hayo ya katiba na kukimbilia kisingizio cha “ujinga wa wananchi” na “wanasiasa kutaka kujimilikisha katiba”! Vyote si sawa. Anyway, serikali ifanye kama ilivyozoea. Watanzania hawana ubavu wa kuipinga. Lakini ni wazi wengi tunajua hii ni janja janja ya wazi kabisa iliyozoeleka nchini.
 
Jk.alikua na lengo zuri tu mkuu...

Hao wanaomdhibiti samia leo ndio waliomdhibiti jk.

Kuna watu wamekula viapo vya kazi ya kuilinda hii nchi maisha yao yote..

Wakati wewe na Cheo chako cha urais wa miaka mitano unataka kuwaletea msumbuvu katika kazi yao?
Yaani una maana wameapa pia na hao wa vyeo vya miaka mitano watakuwa wanatokea upande wa wananzengo wenzetu tu ??!! 😅😅🙏🙏
 
Tunasema wananchi ndio wanaodai katiba mpya. Rais anasema wananchi wengi hawaijui katiba iliyopo hivyo wanashindwa kuonyesha katiba hii ina kasoro zipi! Dawa ni kutoa elimu kwa wananchi wote kwanza! A major paradox.

Hii ni kuanzisha mchezo usio na mwisho (a vicious circle). Tatizo kubwa la katiba hii ni madaraka yaliyopitiliza ya Rais yanayomuweka juu ya katiba na sheria. Marekebisho ya vifungu muhimu kuhakikisha viongozi wote, serikali nzima na vyombo vya dola vinakuwa na kutenda kazi ndani ya mzingo wa katiba, sheria na kanuni kuu za nchi ndicho kinachotakiwa. Wananchi hawahitaji elimu katika hilo. Wanalijua sana na linaathiri maisha yao ya siku kwa siku. Ukusanyaji wa maoni wa kamati ya Jaji Warioba ulithibitisha hayo na mifano ipo tele.

Rais na makundi yake ndani na nje ya serikali ndio wanaoogopa marekebisho hayo ya katiba na kukimbilia kisingizio cha “ujinga wa wananchi” na “wanasiasa kutaka kujimilikisha katiba”! Vyote si sawa. Anyway, serikali ifanye kama ilivyozoea. Watanzania hawana ubavu wa kuipinga. Lakini ni wazi wengi tunajua hii ni janja janja ya wazi kabisa iliyozoeleka nchini.
Kwakweli !! Lakini mbona TEC hawalizungumzii suala hili kama walivyofanya kwa suala la Bandari ??!
 
Sipati picha.
Hiiyo elimu ya Katina itatolewa kwa utaratibu gani?
Muhtasari wake utakuwaje?
Walimu Gani?
Madarasa yepi?
Nanusa harufu ya upigaji wa Yale mabilioni bila matokeo chanya.
 
Mimi binafsi siungi mkono suala la kufundisha watu katiba, hicho ni kichaka cha kutafuna pesa za umma, katiba bora ni kuwa na viongozi waadilifu wenye uzalendo na moyo wa dhati wa kuwatumikia watanzania. Hata tukija na katiba kutoka mbinguni kama hakuna viongozi waadilifu ni kazi bure tu. Kuna nchi hazina katiba rasmi lakini zimetuacha mbali sana kimaendeleo, kwa katiba tuliyokuwa nayo nyerere angeamua kukaa madarakani mpaka afariki asingeshindwa lakini kwa busara na hekima zake aliona inatosha sasa nikabidhi mwingine aendelee. Leo hii tuna wanasiasa wanaojilimbikizia mali hadi za vizazi vyao vya sita alafu kila siku wanawaambia wananchi wa kawaida wajiajiri. Rubbish. Katiba mpya haiwezi kutuletea mabadiliko yoyote zaidi ya kwenda kutengeneza nafasi za wanasiasa wachache kwenda kuitafuna keki ya taifa kwa mrija bila huruma
Abracadabra !! Ili tuendelee kweri kweri tunahitaji Dikiteta MUADILIFU !!
Hii kuachiana kwa miaka mitano mitano ni kazi bure tu !
 
Sipati picha.
Hiiyo elimu ya Katina itatolewa kwa utaratibu gani?
Muhtasari wake utakuwaje?
Walimu Gani?
Madarasa yepi?
Nanusa harufu ya upigaji wa Yale mabilioni bila matokeo chanya.
Ng’hana ong’wafaza 😍🙏🙏😅😅
 
Sijui priorities za TEC. Pengine hawana interest na masuala ya demokrasia 😳. I really don’t know.
 
Back
Top Bottom